The Monk
Platinum Member
- Oct 12, 2012
- 19,239
- 42,837
Mimi sio mtata Mkuu wala sina chuki yeyote
Ila ukweli usemwe, huyo ni binadamu wa kawaida km sisi
Sasa mnapoficha yale mabaya yake mnakusudia nini?
Hata kama unaswalia msikiti wake, jua tu mwamba alikuwa monster
Na wala sio vipodozi
Sijaelewa hasa unachotaka ni kitu gani kwenye huu uzi mkuu. Umeuliza kila unapoandika watu waseme ukweli kuhusu biashara yake, kwanini unataka kulazimisha mambo ya habari za kusikia? Wewe kama unauelewa ukweli kuhusu biashara yake si uuweke hapa hadharani?
Watu wanaongelea yale waliyoyasadiki, kuyashuhudia na kuyaona. Hizo habari za kusikia hata wewe kuna watu wanasikia mengi kukuhusu lakini kwa vile ni kusikia wanapotezea.
mrangi amekupa ushuhuda wa jinsi alivyomfaham na alivyompa msaada kupata biashara ya kuagiza maziwa.
Mie nakwambia nimepanga na kuishi miaka zaidi ya 9 kwao Msasani na alikua akija kumsabahi Bibi yake karibia kila wiki. Kasaidia watu wengi kwa misaada inayoonekana. Wameenda hija na Mama yake waliporudi kaja kugawa zawadi kwa wote majirani na jamaa zake.
Kwa kuwa umeuliza, subiria wanaoujua kuhusu biashara wakujibu, ila kuendelea kumtuhumu mtu kwa habari za kusikia sio sawa.
Jifunze kuwatendea wengine kama ambavyoungependa wao wakutendee wewe.