Elli
Platinum Member
- Mar 17, 2008
- 55,180
- 85,338
Wapendwa Wapwa zangu,
Nimepitia historia nyingi za kikwetu (Afrika), zinaonekana kuwa Wazee wetu walikua na Kitu kinaitwa NGUVU UHAI ambayo iliwasaidia sana katika maisha yao ya kila siku kwa nia njema hasa kupigana na maadaui zao. Nilipokuwa mdogo nilisimuliwa sana habari za Ndugu Paulo, Osale Otango na wengineo wengi na nikabahatika kwenda kupaona mahali ambapo Osale Otango alikua akijificha. Nimesoma vitabu vya Fasihi za Kiswahili na zile za Kigeni, nyingi ya hizo zinazungumzia na kutaja nguvu uhai hii. Leo hii naamini hii kitu haipo kabisa na kama ipo basi haitumiwi kwa manufaa waliyoyatumia watangulizi wetu.
Ombi langu; naombeni msaada ni wapi naweza kwenda kujifunza taaluma hii ili nipambane na udhalimi uliokithiri kwenye jamii yetu? Iila kama itawezekana nataka iwe modernized sitaki hii ambayo naskia kuna kuuwana, no. Mfano, mwana siasa anaoongopa jukwaani basi kwa kutumia hii njia anajikuta tu anakuwa bubu kwa muda, kama kuna mtu anaibia Taifa au wanachi basi tunamfuatilia na hatimae anajikuta tu amerudisha hizo fedha na mali......Nisaidieni jamani kwa nia njema kabisa
Nimepitia historia nyingi za kikwetu (Afrika), zinaonekana kuwa Wazee wetu walikua na Kitu kinaitwa NGUVU UHAI ambayo iliwasaidia sana katika maisha yao ya kila siku kwa nia njema hasa kupigana na maadaui zao. Nilipokuwa mdogo nilisimuliwa sana habari za Ndugu Paulo, Osale Otango na wengineo wengi na nikabahatika kwenda kupaona mahali ambapo Osale Otango alikua akijificha. Nimesoma vitabu vya Fasihi za Kiswahili na zile za Kigeni, nyingi ya hizo zinazungumzia na kutaja nguvu uhai hii. Leo hii naamini hii kitu haipo kabisa na kama ipo basi haitumiwi kwa manufaa waliyoyatumia watangulizi wetu.
Ombi langu; naombeni msaada ni wapi naweza kwenda kujifunza taaluma hii ili nipambane na udhalimi uliokithiri kwenye jamii yetu? Iila kama itawezekana nataka iwe modernized sitaki hii ambayo naskia kuna kuuwana, no. Mfano, mwana siasa anaoongopa jukwaani basi kwa kutumia hii njia anajikuta tu anakuwa bubu kwa muda, kama kuna mtu anaibia Taifa au wanachi basi tunamfuatilia na hatimae anajikuta tu amerudisha hizo fedha na mali......Nisaidieni jamani kwa nia njema kabisa