Tanganyika1
JF-Expert Member
- May 10, 2011
- 422
- 86
Jamani wana jf nawapenda sana na natambua uwepo wenu katika harakati za mapambano dhidi ya matatizo tulionayo watanzania.
Binafsi napenda kutoa rai kuwa ajira imekua tatizo kubwa hapa tanzania hasa kwa vijana baada ya matatizo ya malaria, vifo vya watoto na wa mama wajawazito, bila kusahau ajali za barabarani.
Katika kutafakari kwa muda nimegundua kuwa tunaweza kujikwamua kwa kugawana muda wa kufanya kazi. Ni kawaida kwa watu kwenda kazini kila asubuhi na kurejea majumbani mwao jioni kwa mapumziko....sasa nadhani ingekua ni jambo jema na la busara kama baadhi ya watu ambao hawana kazi lakini sifa za kufanya kazi wanazo basi serikali na mashirika binafsi yange ongeza muda wa kufanya kazi na hivyo basi kuruhusu watu wafanye kazi usiku na kwa kufanya hivyo itasaidia kupunguza tatizo la ajira kwa vijana wetu............ni mtazamo tu waungwana.
Binafsi napenda kutoa rai kuwa ajira imekua tatizo kubwa hapa tanzania hasa kwa vijana baada ya matatizo ya malaria, vifo vya watoto na wa mama wajawazito, bila kusahau ajali za barabarani.
Katika kutafakari kwa muda nimegundua kuwa tunaweza kujikwamua kwa kugawana muda wa kufanya kazi. Ni kawaida kwa watu kwenda kazini kila asubuhi na kurejea majumbani mwao jioni kwa mapumziko....sasa nadhani ingekua ni jambo jema na la busara kama baadhi ya watu ambao hawana kazi lakini sifa za kufanya kazi wanazo basi serikali na mashirika binafsi yange ongeza muda wa kufanya kazi na hivyo basi kuruhusu watu wafanye kazi usiku na kwa kufanya hivyo itasaidia kupunguza tatizo la ajira kwa vijana wetu............ni mtazamo tu waungwana.