Natamani Dr. Slaa aje aniambie haya!

a4afrika

JF-Expert Member
Apr 13, 2012
1,384
1,314
Tukishampa nchi 2015 (japo tunaweza hata kesho), atawafanyaje watu hawa!

Wenye majumba ya thamani hali jirani zao wanalala nje!
Wenye kumiliki magari makali hali jirani zao hawana uwezo wa kununua hata ndala!
Wenye kulimbikiza fedha benki hali jirani alala njaa?
Wenye kuishi Masaki na Osterbay hali kuna wa Tandale na Manzese!
Wenye kuona ni haki kuzunguka misuru ya magari hali hospitali zetu hazina gari za wagonjwa, na shule na walimu wake hoi kwa mazingira yaliyokosa vitendea kazi.
Wenye kuhodhi aridhi kubwa kwa manufaa ya watoto wao!
Wageni wanaochota rasilimali zetu hali twabaki kapuku!
Wenye kula na kusaza hali jirani na watoto wake wanashindia uji!
Uwepo wa high class mahosptalini na kule kwetu sie.
Uwepo wa special schools hali na St. Kayumba zetu.
Hata uwepo wa Dar na Mwanza hali kuna Lindi na Singida.
Na mengine kama hayo yaashiriayo UBINAFSI.

Mungu wetu anaita!
 
Wakati wa kampeni haujafika tuliza kipila muda wa kampen ukianza atafunguka usimsababishie Offside ya kijinga!
 
Tukishampa nchi 2015 (japo tunaweza hata kesho), atawafanyaje watu hawa!

Wenye majumba ya thamani hali jirani zao wanalala nje!
Wenye kumiliki magari makali hali jirani zao hawana uwezo wa kununua hata ndala!
Wenye kulimbikiza fedha benki hali jirani alala njaa?
Wenye kuishi Masaki na Osterbay hali kuna wa Tandale na Manzese!
Wenye kuona ni haki kuzunguka misuru ya magari hali hospitali zetu hazina gari za wagonjwa, na shule na walimu wake hoi kwa mazingira yaliyokosa vitendea kazi.
Wenye kuhodhi aridhi kubwa kwa manufaa ya watoto wao!
Wageni wanaochota rasilimali zetu hali twabaki kapuku!
Wenye kula na kusaza hali jirani na watoto wake wanashindia uji!
Uwepo wa high class mahosptalini na kule kwetu sie.
Uwepo wa special schools hali na St. Kayumba zetu.
Hata uwepo wa Dar na Mwanza hali kuna Lindi na Singida.
Na mengine kama hayo yaashiriayo UBINAFSI.

Mungu wetu anaita!
Mkuu, kosa si kuwa na utajiri bali kosa ni njia ulizozitumia kuupata huo utajiri ni halali?
 
...Mawazo ya Kimaskini...

...Kila mwananchi ana haki ya kumiliki pesa, ardhi, majumba, kupata huduma za hospitali na shule za kiwango akipendacho ilmuradi havunja sheria, suala la kuwasaidia maskini wanaomzunguka ni hiari yake na katu hawezi kulazimishwa kufanya hivyo...
 
Tumwombe Mungu 2015 tufike salama ili tukishuhudie kiama cha mafisadi.

...Ukiondoa viongozi wachache wa sasa wanaokula kupitia mfumo wa kiserikali na viongozi wapya watakaopata mchongo wa kula serikali baada ya uongozi kubadilika, kwa asilimia kubwa safu ya wenye kufaidi maisha,kwa mantiki ya matajiri, itabakia vilevile kwa sababu utajiri kwa mtu ni skills, na kwa yeyote aliye na skills hizo pesa zitamfuata tu, kuendelea kusubiri ni dalili za kutokuwa na uwezo huo...
 
Mungu wetu ametuumba na kutuwekea msingi mkuu wa namna ya kuishi, yaani UTU, ambao upo nafsini mwa kila mtu..., na kutouishi ni sawa na kujisaliti na kujinafiki mwenyewe, umejikataa kabla ya kukataliwa na jamii. Katika mantiki ya UTU, maisha ni hatua, hakuna UHALALI wa kuwa na hatua ya 5, kwa wenye 0 au 1, ukishapata 1 ni haki na wajibu wako kumsaidia jirani yako kuifikia hiyo moja, akishaifikia tafuta ya 2 sasa. Yaani kusiwe na 2 kama hakuna 1 na 1, au 3 kama hakuna 2 na 2. Najua kuwa mimi na wewe ni vigumu kushuhudia hili, lakini tusiache kusimika misingi ya kufikia hili, na mifupa yetu aridhini, italoweshwa kwa maji ya mito ya machozi ya furaha kutoka machoni mwa watoto au vitukuu vyetu, na hiyo ndiyo upendo wetu wa dhati kwao, na ndio kuishi hata baada ya kifo chetu. Tusijidanganye na mnazoziita haki za binadamu, zimekosa mantiki. Je, ni haki kushindanishwa kiwete na mzima katika mbio, au kumuacha msituni ajitetee? Hatuoni huko? Mtu makini huongozwa na mantiki na si mifumo iliyowekwa kwa maslahi ya watu fulani, MANTIKI huweza kubadilisha mfumo, lakini si mfumo kwa mantiki. Tukisema muda bado, kutakuwa ndio kushindwa kwetu, wajukuu wetu watakumbwa na haya haya ya leo, labda wao waje kuwafanyia wajukuu zao na lawama ziwe juu yetu. Maisha ni furaha, kama haipo basi ni upuuzi, na hakuna furaha ya mtu ila watu! SI SAHIHI KUNGOJA, NA TUANZE KUISIMIKA SASA, hata kwa mahubiri kabla ya nguvu!
Labda mimi jinga, niongozeni kwa hoja, msitukane jamani wanaafrika wenzangu wa Tanzania.
Mungu wetu anaita!
 
Hisia zako kali,umemaanisha unachokitetea,inaonesha una nia na dhati na usawa katika jamii,keep it up.LAKINI,Je turudi katika misingi ya ujamaa?
 
Tukishampa nchi 2015 (japo tunaweza hata kesho), atawafanyaje watu hawa!

Wenye majumba ya thamani hali jirani zao wanalala nje!
Wenye kumiliki magari makali hali jirani zao hawana uwezo wa kununua hata ndala!
Wenye kulimbikiza fedha benki hali jirani alala njaa?
Wenye kuishi Masaki na Osterbay hali kuna wa Tandale na Manzese!
Wenye kuona ni haki kuzunguka misuru ya magari hali hospitali zetu hazina gari za wagonjwa, na shule na walimu wake hoi kwa mazingira yaliyokosa vitendea kazi.
Wenye kuhodhi aridhi kubwa kwa manufaa ya watoto wao!
Wageni wanaochota rasilimali zetu hali twabaki kapuku!
Wenye kula na kusaza hali jirani na watoto wake wanashindia uji!
Uwepo wa high class mahosptalini na kule kwetu sie.
Uwepo wa special schools hali na St. Kayumba zetu.
Hata uwepo wa Dar na Mwanza hali kuna Lindi na Singida.
Na mengine kama hayo yaashiriayo UBINAFSI.

Mungu wetu anaita!

Maswali yako yote niliyo highlight hayana maana wala mashiko kwa Tanzania ya leo na Yeyote atakayeenda huko amefilisika kisiasa. Ulichotakiwa kuongezea ili maswali yako yawe relevant ni kuwa 'Wenye kuwa na vitu hivyo kwa kuvipata kwa njia zisizo halali'

Nafikiri tusitishie kuadhibu hard working ili kuwa please wengine cha muhimu ni kuweka mazingira ya kila mtu kufikia vitu hivyo provided atafanya kazi kwa bidii. Lets fight for lifting up everybody not bringing down the lawful success.

 
Maswali yako yote niliyo highlight hayana maana wala mashiko kwa Tanzania ya leo na Yeyote atakayeenda huko amefilisika kisiasa. Ulichotakiwa kuongezea ili maswali yako yawe relevant ni kuwa 'Wenye kuwa na vitu hivyo kwa kuvipata kwa njia zisizo halali'

Nafikiri tusitishie kuadhibu hard working ili kuwa please wengine cha muhimu ni kuweka mazingira ya kila mtu kufikia vitu hivyo provided atafanya kazi kwa bidii. Lets fight for lifting up everybody not bringing down the lawful success.


Nakupa 'like' kama mia tano hivi. Unajua muanzisha thread yawezekana ni mpambanaji mzuri ila anasahau kuwa CDM hawana chuki na mtu yeyote. Naomba kumwambia huyu jamaa pamoja mie sio msemaji wa CDM kuwa; tunategemea wale wa masaki na o'bay watakaa walipokuwa allocated kisheria, waliopata utajiri kihalali au kwa njia zinazokubaka hawatabugudhiwa ila kiufupi maslahi ya nchi na wanyonge yatawekwa mbele. Yasipofanyika haya una uhuru wa kuchagua chama au mtu yeyote after 2015. Karibu sana.
 
Hisia zako kali,umemaanisha unachokitetea,inaonesha una nia na dhati na usawa katika jamii,keep it up.LAKINI,Je turudi katika misingi ya ujamaa?

Kama ndiyo mantiki iliyomo nafsini mwet, basi hatuna budi kuanza kuisimika hiyo, japo ni sawa kwa afukiaye mbegu ya mkangazi kuvuna mbao, lakini tumaini analo si kama yule aliyeacha, hata isipoota wapo watakaona umuhimu wa ulichotaka kufanya, watafanya wajukuu wao watavuna mbao, huko ndiko kuishi hata baada ya kifo chako. Nyerere alisema "...ujamaa ni imani....", tukiihubiri inavyostahili, watoto wetu wataiishi. Tupindue nafsi zetu, kwani hata siku moja haiwezi kutokea afrika ikawekeza magharibi, NEVER. Sasa kwanini tung'ang'anie kupinga ukweli? Ndoto gani tunazoota, au ndio bora liende tu hali tunachezewa sharubu? Mpumbavu ni yule anayefananisha thamani ya maisha yake, na yale ya taifa zima!
Nimemtaja Dr. Slaa, kama mtu anayeweza kunielewa na mwenye ushawishi mkubwa kwa watu, kati ya wanaogombea nafasi ya kutuongaza katika hiyo furaha. Sina maana tofauti Kiboko Yenu, labda unifikirie tena, ila utakuwa unanionea ukiamini hvyo, japo siogopi. Ndicho nachoamini, upeo wangu umeona hilo nafsini mwangu, ndio MANTIKI KUU NAFSINI MWANGU, UTU!
Sisi tulishazikwa kaburi na tumeshaoza, tuwafikirie watoto wetu wajao nao wasifukiwe hai kama sisi. Mungu wetu anaita, umoja na kuthubutu ndiyo nguvu yetu, yu tayari kutushindia.
 
Usisahau kumuuliza na haya:

Salama Ndugu wana JF,

NI muda sasa hatujawekana sawa juu ya uozo, Madudu yanayofanywa na viongozi wa juu wa Chadema hasa Dr.slaa, Licha ya uzuri alionao kwenye siasa za nje ya chama(kwenye majukwaa) lakini huyu ni mtawala hatari sana ndani ya chama, Na kama sekretarieti ya chama na Kamati kuu ya chama itaendelea kumfumbia macho nadhani huyu mzee si muda mrefu tutasikia pale makao makuu damu imemwagika au viongozi muhimu wameachia ngazi na hawataki tena kufanya kazi na Dr.slaa.

Naomba kuwaletea baadhi tu ya upuuzi wa Dr.slaa ambao hadi nakwenda mtandaoni hana pakuweka sura yake baada ya kutoka Kwenye kikao cha kamati kuu kilichomalizika usiku wa manane pale Mbezi garden.

1.Huwezi kuamini kama kweli huyu ndiye Dr.slaa amefanya tukio hili..Ni tukio linalo husiana na Uchaguzi wa mwenyekiti wa Chadema mkoa wa Iringa uliofanyika mwaka jana ambapo Mbunge wa viti maalumu CHIKU ABWAO alishinda nafasi ile ya uchaguzi na kutambulika kama mwenyekiti wa chama mkoa wa iringa.

Lakini unajua ilikuwaje hadi limefika mezani mwa kikao cha kamati kuu?
Wakati wa uchaguzi ule wa mwenyekiti wa mkoa wa Iringa ambao Msingwa alikuwa ndiye mwenyekiti hapo awali, Chadema kupitia katibu mkuu wa chama Dr.slaa walimkopa Tsh.Million tano ndugu CHIKU ABWAO(ndivyo ilivyo wala usidout, inakuwaje chama kikope million 5 wakati kinaruzuku na misaada kibao?) kwaajili ya kusafirisha wajumbe kufika kwenye uchaguzi ule pale iringa makao makuu ya chama...

Baada ya kokopa fedha hizo kwa CHIKU ABWAO, Dr.slaa akamteua CHIKU ABWAO kuwa msimamizi mkuu wa uchaguzi ule pale iringa(mwenyekiti Taifa alikuwa hajui hilo)....Wakati huohuo tena Dr.slaa akamshawishi CHIKU ABWAO kuvuta fomu ya kugombea nafasi hiyo ya uenyekiti pale iringa(kwa maana hiyo,msimamizi mkuu wa uchaguzi ule naye alikuwa mgombea wa nafasi tajwa,Unategemea nini hapo?)..Kimsingi huu ni ukiukwaji wa Demokrasia na nimambo ya kitoto ambayo Dr.slaa nayafanya na wabunge wake wa viti maalumu(sijajua kilichonyuma ya pazia)...

Mshindi wa uchaguzi ule alikuwa ni CHIKU ABWAO ambaye alikuwa ni msimamizi mkuu wa uchaguzi ule.Na Dr.slaa bila aibu akamtambua Chiku kama mwenyekiti wa mkoa wa iringa.Hii kiti imewagawa kabisa wabunge wawili wa chama kimoja(msingwa na Chiku) Msigwa analalamika imekuwaje lafu kama hii ifanywe kwa msaada wa katibu mkuu tena anayejiita Mtu makini?...

Kusema kweli kamati kuu ulishikwa na Butwaaaaa kusikia mchezo huo, Huku chiku Abwao akitumbuka macho kwa aibu ndani ya kikao kile.

Nauliza umakini wa Dr.slaa upo wapi? Anaendesha chama kihunikihuni hivi kama anaendesha kampuni yake!!!!!

2.Jambo la pili lililo onesha ni namna gani Dr,slaa hafai hata kuwa karani wa hospitali,Ni ule ugomvi wake na watendaji flani wa pale makao makuu ambapo anataka Mchumba wake Josephine apate nafasi ya kazi pale makao makuu..Hakika Dr.slaa anaugomvi mkubwa sana Na Miwgamba pamoja na Anton komu(anashughulika na mambo ya fedha pale makao makuu) amemjengea chuki,kisilani na anamuundia zengwe la kila aina ili tu Mwigamba atoke pale makao makuu.

Ndani ya kikao cha kamti kuu,Dr.slaa alitoa kali ya mwaka baada ya kusimama na kusema simtaki mwigamba na nimeshamwambia anikabidhi ripoti ya Arumeru kisha aondoke zake,Na nukuu"ndugu wajumbe unaweza kuishi na mtu miaka mitatu usijue fani yake..kumbe Mchumba wangu Josephine ni mzuri sana kwenye mambo ya IT anaweza kutusaidia kufanya kazi za kukagua fedha hapa makao makuu baada ya mwigamba kuondoka" wajumbe wakamati kuu walilipuka kwa mshangao huku wakiuliza inakuwaje Mwigamba aliyeajiriwa kwa taratibu leo anafukuzwa bila utaratibu?

Kwani wewe Dr.slaa ninani hapa? mwigamba endelea na kazi,hatutaki makahaba ndani ya chama chetu,Huyo kimada wako aishie hukohuko nyumbani kwako...walisikika wajumbe baadhi.

Kusema kweli Dr.slaa anafanya kila namana kumuingiza Mchumba wake pale makao makuu,Anajaribu kila njia,Alijaribu kumfukuza ANton komu akakwama kwa sababu ya Gazeti la mwanahalisi pili kwa sababu Mwenyekiti na Anton Komu ni maswahiba.

Mwigamba kusema kweli amekuwa msaada sana wa kuzuia upotevu wa pesa katika chaguzi mbalimbali kiasi kwamba kwenye kikao cha Sekretarieti wajumbe wote walimpongeza kwa ripoti safi ya Arumeru.

Nauliza Dr.slaa anataka kuleta mdudu gani ndani ya chama<mbona mke wa mbowe hajihusishi na mambo ya chama? Mbona Obama hamleti mke wake kwenye chama? Josephine amekupa dawa gani Dr.slaa unataka kuuua chama?

3.Kama ulikuwa hujui Dr,slaa,anaye wahi kupeleka ripoti au kesi yoyote ndiye aliyeshinda kesi kwa mijibu wa akili yake..Huwa hawezi kusikiliza pande zote mbili,yeye anahukumu bila kisikiliza..Ameshafukuza madiwani wengi kwa sababu hana utashi wa kusikiliza,Ameshafukuza Viongozi wa serikali za mitaa wengi wa chadema bila kusikiliza maoni yao.yeye anasema anaye wahi kuleta kesi ndiye mshindi.(nitawataja viongozi aliowatimua kanda ya ziwa,na sehemu mbalimbali bila kuwasikiliza..na nitawataja wale aliotunishiana nao misuli akawashindwa)nasubiri anijibu.

Mwisho naomba kuhoji UWEPO WA GODFREY LEMA kwenye kikao cha KAMATI KUU kilichomalizika jana,kimsingi ameshapoteza sifa ya kuwa mjumbe wa kamti kuu tangu alipotenguliwa ubunge..Lakini Dr.slaa ulimwita kuhudhuria kikao kama nani?

Naomba kwa leo niishie hapa,japo nina mengi sana ila "Miruzi mingi humpoteza mbwa mwelekeo" naomba tujadili haya kwanza then mengine ya ndani zaidi yatakuja.

Dr.slaa popote ulipo naomba uje ujibu hapa,kanusha madudu yako hapa!!!majibu yako yawe ya wazi na yanayoeleweka sio nusu nusu kama tulivyo kuzoea.

Mnakaribishwa mtukane,mtumie lugha mbaya...lakini mwelevu atajua ukweli wa mambo haya na atakosoa mwenendo huu wa Dr.slaa iliajirekebishe tujenge chama chetu.

By Tuntemeke...Mwakipande(mkinga halisi).

 
Mkuu, kosa si kuwa na utajiri bali kosa ni njia ulizozitumia kuupata huo utajiri ni halali?
haswaa! kwa jinsi nilivyomsoma mtoa uzi naona anataka dr aanzishe jihad dhidi ya wenye mali hata kama wamejinyima na kujituma kuzipata!!
 
tukishampa nchi 2015 (japo tunaweza hata kesho), atawafanyaje watu hawa!

wenye majumba ya thamani hali jirani zao wanalala nje!
wenye kumiliki magari makali hali jirani zao hawana uwezo wa kununua hata ndala!
wenye kulimbikiza fedha benki hali jirani alala njaa?
wenye kuishi masaki na osterbay hali kuna wa tandale na manzese!
wenye kuona ni haki kuzunguka misuru ya magari hali hospitali zetu hazina gari za wagonjwa, na shule na walimu wake hoi kwa mazingira yaliyokosa vitendea kazi.
Wenye kuhodhi aridhi kubwa kwa manufaa ya watoto wao!
Wageni wanaochota rasilimali zetu hali twabaki kapuku!
wenye kula na kusaza hali jirani na watoto wake wanashindia uji!
uwepo wa high class mahosptalini na kule kwetu sie.
uwepo wa special schools hali na st. Kayumba zetu.
hata uwepo wa dar na mwanza hali kuna lindi na singida.
Na mengine kama hayo yaashiriayo ubinafsi.

Mungu wetu anaita!

uko sahihi laki,ni tatizo lako umeshindwa kuelewa shida si mtu kumiliki vitu hivyo shida ni njia anazotumia kujimilikishia vitu hivyo,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,,kama mtu anaweza kumiliki mali kihalalia ni vizuri sana na tunataka taifa la aina hiyo lakini kama ni njia za wizi kama wafanyavyo wengi ndiyo wanatakiwa wasakwe....
 
watajichimbia chini hawa wala nchi maana hawataweza kuhimili hasira za wananchi ambazo mpaka sasa zimeshaanza kuvuja
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom