Nataka Nimshirikishe Mke Wake!!

chakii

JF-Expert Member
Sep 15, 2013
19,666
22,674
Habari zenu wana-MMU!!

Kuna rafiki yangu ambaye naweza kumuita kaka pia maana tangu tukiwa wadogo tumeishi pamoja ila kadri muda ulivyokwenda kila mtu aliekea kule ambapo alipotegemea kujenga maisha yake,.

Huyu rafiki yangu tunaheshimiana sana nikimaanisha wote tumetokea mtaa mmoja tangu tukiwa wadogo hivyo tunaelewana kwa undani zaidi,

Tumekutana mjini na kuendeleza urafiki wetu tangu tukiwa wadogo, mara kwa mara tumekuwa tukijumuika pamoja kupata hata vinywaji huku tukijikumbushia mambo ya utoto kule kijijini,.

Lengo la kuanzisha hii thread

Huyu rafiki yangu amekuwa akinishirikisha matatizo yake mara kwa mara na pale ninapokuwa na uwezo huwa ninamsaidia maana naamini hata mimi kuna siku nitapata shida na nitaomba msaada wake,.

Mke wa huyu rafiki yangu alipata ujauzito na siku ya kujifungua huyu rafiki yangu hakuwa na fedha za kumgharamia mke wake hivyo aliniomba nimsaidie kiasi fulani cha fedha ambacho nisingependa kukitaja ili aweze kugharamia huduma hiyo huku akiniahidi kurejesha kiasi hicho muda si mrefu,.

Cha ajabu takriban miezi mitano imeshapita mpaka sasa hajanirejeshea fedha zangu pamoja na mimi kumsamehe nusu ya kiasi nilichomsaidia,.

Kila ninapompigia simu analia shida ilhali mimi najua kweli mtu huenda mambo yakawa bado hayajamuwia vizuri lakini nashangaa kwa nini hata nusu ameshindwa baada ya kumsamehe sehemu ya deni hilo,.

Kwa sasa nazihitaji hizi fedha ili na mimi niweze kuendesha mambo yangu lakini naona Jamaa hana dalili za kurejesha fedha zangu hata nusu,..

Mke wa rafiki yangu tunafahamiana maana Jamaa alishanitambulisha kwake mimi kama mdogo wake,.


Wana-MMU mnaonaje nikamshirikisha Shemeji labda huenda akanirejeshea fedha zangu!!

Je nimueleze vipi mke wake kuhusu deni hili?

Je nimwambie kwamba hizi hela nilimkopesha mume wake wakati yeye anajifungua?


Ushauri wenu ni muhimu kwangu wadau,..
 
Kama hataki kurudisha mgegedee mke wake mmalizane kwa7 zilichukuliwa kwa ajili yake.
 
Kama ni rafiki yako kweli bila shaka unajua financial status yake ikoje, issue sio kukulipa nusu au deni lote, kama yuko vibaya kiuchumi sioni hata kama ukimwambia mkewe unaweza kupata msaada, twambie, kiuchumi yukoje? Anafanya kazi ipi ya mshahara upi, au unafanya biashara gani?
 
Jaribu kumwambia kuwa utampa taarifa mkewe uone atasemaje..ila vizuri mkamalizana wenyewe..
 
Kama ni rafiki yako kweli bila shaka unajua financial status yake ikoje, issue sio kukulipa nusu au deni lote, kama yuko vibaya kiuchumi sioni hata kama ukimwambia mkewe unaweza kupata msaada, twambie, kiuchumi yukoje? Anafanya kazi ipi ya mshahara upi, au unafanya biashara gani?

mkuu financial status yake haiwezi kumzuia kunilipa deni langu!!

Anaingiza hela nzuri tu,.
 
Kama kweli ni rafiki yako kama ulivyosema huna haja ya kumdhalilisha kwa mkewe. Jiulize, kwani ukimwambia mkewe ndio hela zitapatikana???? Siku nyingine ukimsaidia mtu msaidie tu kwa kiwango kile ambacho hakitakuumiza incase mambo yake hayakwenda fresh kwa wakati.
 
Jaribu kumwambia kuwa utampa taarifa mkewe uone atasemaje..ila vizuri mkamalizana wenyewe..

nimeshamwambia mkuu na hajanijibu chochote mpaka sasa!!

Wakati mwingine hata simu hapokei!!
 
Wanaume Tunalindana hata iweje, sasa wewe kumuhusisha Mke wake sio uanaume huo..

Cha kufanya jitaidi uonane na jamaa face to face umpe vidonge vyake kwamba anachofanya sio nawe una shida na hela uone atasemaje?

Ni bora kuhusisha marafiki wenzenu wa kiume wakamchane jamaa anazingua kuliko kumhusisha mke wake..

Wanawake hawatakiwi kujua mambo yote ya mumewe maana wenyewe tu hawajielewi. Achelewi siku kulianzisha na kuanza kumpiga madongo mumewe ana Kupa kopa kwa watu na kulipa halipi..

Kumwambia mkewe unakuwa ujamsaidia jamaa, wala kujisaidia mwenyewe zaidi ya kumdhalilisha rafiki yako wa siku nyingi..

Mda mwingine unafumba macho tu unasamehe.. Pesa kitu gani bwana, tunahonga sh ngapi kwa mwaka, Kunywa bia Bar, michango ya harusi etc..
 
Mi ndio ningekuwa mke wa huyo jamaa ningekushangaa sana kama ungekuja kusema hayo madai yenu, unles in tens of millions. Kweli urafiki gani that you are considering sacrificing all your old friend na kwenda kutangaza.

Mwambie rafiki yako una shida na hiyo hela, kama harudishi basi jaribu kukaa kimya, ipo siku fadhila yako itarejeshwa na Mungu.
 
Mi ndio ningekuwa mke wa huyo jamaa ningekushangaa sana kama ungekuja kusema hayo madai yenu, unles in tens of millions. Kweli urafiki gani that you are considering sacrificing all your old friend na kwenda kutangaza.

Mwambie rafiki yako una shida na hiyo hela, kama harudishi basi jaribu kukaa kimya, ipo siku fadhila yako itarejeshwa na Mungu.

mkuu hata kama ingekuwa shilingi kumi its means alot to me,.


Kuvunja urafiki kwa ajili ya deni its better maana i can't etertain such a thing,..
 
Wanaume Tunalindana hata iweje, sasa wewe kumuhusisha Mke wake sio uanaume huo..

Cha kufanya jitaidi uonane na jamaa face to face umpe vidonge vyake kwamba anachofanya sio nawe una shida na hela uone atasemaje?

Ni bora kuhusisha marafiki wenzenu wa kiume wakamchane jamaa anazingua kuliko kumhusisha mke wake..

Wanawake hawatakiwi kujua mambo yote ya mumewe maana wenyewe tu hawajielewi. Achelewi siku kulianzisha na kuanza kumpiga madongo mumewe ana Kupa kopa kwa watu na kulipa halipi..

Kumwambia mkewe unakuwa ujamsaidia jamaa, wala kujisaidia mwenyewe zaidi ya kumdhalilisha rafiki yako wa siku nyingi..

Mda mwingine unafumba macho tu unasamehe.. Pesa kitu gani bwana, tunahonga sh ngapi kwa mwaka, Kunywa bia Bar, michango ya harusi etc..

yeah, kweli mkuu,.

But if the guy angekuwa faithfull kutimiza ahadi yake hope evrthing would have gone smoothly,.



Jamaa hata simu yangu hapokei nowadays, hata meseji hajibu pia!!

Kama angeona urafiki wetu una thamani asingefanya anachokifanya sasa,..
 
unajua kwenye maisha, there is always NEXT TIME....mi naona achana naye we muache tu km ameamua kuingia mitini, ila naamini atakuja kukwama tena na bila haya atakutafuta..hapo sasa ndio umkumbushe hilo deni lako...pole sana mkuu.hiyo ni opsheni ya kwanza, ya pili mtishie kuwa utamwambia mkewe kuhusu suala hilo uone atafanyaje..
 
Habari zenu wana-MMU!!

Kuna rafiki yangu ambaye naweza kumuita kaka pia maana tangu tukiwa wadogo tumeishi pamoja ila kadri muda ulivyokwenda kila mtu aliekea kule ambapo alipotegemea kujenga maisha yake,.

Huyu rafiki yangu tunaheshimiana sana nikimaanisha wote tumetokea mtaa mmoja tangu tukiwa wadogo hivyo tunaelewana kwa undani zaidi,

Tumekutana mjini na kuendeleza urafiki wetu tangu tukiwa wadogo, mara kwa mara tumekuwa tukijumuika pamoja kupata hata vinywaji huku tukijikumbushia mambo ya utoto kule kijijini,.

Lengo la kuanzisha hii thread

Huyu rafiki yangu amekuwa akinishirikisha matatizo yake mara kwa mara na pale ninapokuwa na uwezo huwa ninamsaidia maana naamini hata mimi kuna siku nitapata shida na nitaomba msaada wake,.

Mke wa huyu rafiki yangu alipata ujauzito na siku ya kujifungua huyu rafiki yangu hakuwa na fedha za kumgharamia mke wake hivyo aliniomba nimsaidie kiasi fulani cha fedha ambacho nisingependa kukitaja ili aweze kugharamia huduma hiyo huku akiniahidi kurejesha kiasi hicho muda si mrefu,.

Cha ajabu takriban miezi mitano imeshapita mpaka sasa hajanirejeshea fedha zangu pamoja na mimi kumsamehe nusu ya kiasi nilichomsaidia,.

Kila ninapompigia simu analia shida ilhali mimi najua kweli mtu huenda mambo yakawa bado hayajamuwia vizuri lakini nashangaa kwa nini hata nusu ameshindwa baada ya kumsamehe sehemu ya deni hilo,.

Kwa sasa nazihitaji hizi fedha ili na mimi niweze kuendesha mambo yangu lakini naona Jamaa hana dalili za kurejesha fedha zangu hata nusu,..

Mke wa rafiki yangu tunafahamiana maana Jamaa alishanitambulisha kwake mimi kama mdogo wake,.


Wana-MMU mnaonaje nikamshirikisha Shemeji labda huenda akanirejeshea fedha zangu!!

Je nimueleze vipi mke wake kuhusu deni hili?

Je nimwambie kwamba hizi hela nilimkopesha mume wake wakati yeye anajifungua?


Ushauri wenu ni muhimu kwangu wadau,..

Hauna haja ya kumwambia mke wake, mvumilie tu ndugu yangu, huenda amekwama kweli.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom