Nataka nikaonane na Rais wetu mara baada wizara ya utumishi kuninyima hali yangu ya uhamisho

Nyankuru Wankuru

JF-Expert Member
Apr 22, 2018
1,199
1,346
Wadau mm kwa takribani mwaka nimekuwa nikihangaika kufuata familia yangu kwa kuomba uhamisho.

Taratibu zote za maombi zimefanyika

Cha ajabu nimejibiwa majibu yasiyokuwa na huruma na kibinadamu.

Sasa nimeamua kufanya maamuzi magumu kabisa.

Jumanne ya tarehe 9.4.2019 nitatembea kutoka mkoani pwani hadi Ikulu ya Rais jijini dar es salaam kwa lengo la kumuomba Rais wetu mpendwa kuingilia kati suala hili.

Wakuu naombeni ushauri wenu , niende ikulu kwanza au nianze kwa katibu mkuu.

Mimi nataka nikamwambie Rais wetu yote yanayotendeka pale utumishi.

Watumishi wa umma wananyanyasika sanaa na hawa watu wachache wasio kuwa na huruma na familia za watumishi.

Mtu anaomba uhamisho na anasema atajigharamia wao wanamuandikia barua isiyofuata taratibu za kiutumishi.

Sasa nimeamua kumfuata Rais wetu kumueleza yote. Na kumuambia manyanyaso watumishi wanayopata kutoka kwa mkurugenzi wa utumishi kurugenzi ya utumishi na uhamisho kwa watumishi.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kila la kheri,ila beba vifuatavyo
1.kitambulisho cha kazi
2.barua zako zote ulizoandika na ulizojibiwa
3.kitambulisho cha taifa
4,barua ya ruhusa
5,passport size 4
mwisho kabisa ondoa woga,pale getini kwa mkulu,urambe vizuri,kama unalo shato jeupe na tai,itapendeza zaidi
mwisho wa mwisho usisahau kutujuza yatakayojiri huko,viambata nilivyokwambia ni muhimu kwa usalama wako binafsi.
Kila la kheri mkuu.
 
Moja ya sehemu zenye nyodo, ukiritimba katika kazi na upendeleo wa wazi wazi kabisa ni huko Utumishi.

1. Hawaingizi au hawawarudishi watumishi kwenye payroll na pia kulipa arrears za mishahara kwa wakati hata kama taratibu zote za wao kufanya hivyo zimekamilishwa na taasisi ajiri ya mtumishi anaetakiwa kuingizwa au kurudishwa kwenye payroll.
3. Barua zinazotoka kwenye taasisi ajiri au watumishi wenyewe kwenda huko ujibiwa baada ya miezi kadhaa pale wanapojisikia. Kuhudumia watumishi nchi nzima siyo excuse ya kuchelewesha huduma kwani kama kazi ni nyingi waongeze watoa huduma na/au kuimarisha mifumo ya kutolea huduma.
4. Inapotokea mtumishi amepitishiwa barua za kuhamia sehemu fulani wanayoitamani wao basi wanachokifanya ni kutumia mwanya huo kuwahamishia huko kwenye nafasi ndugu, jamaa na marafiki zao. Hali hiyo umfanya mtumishi aliyepitishiwa barua yake na mwajiri anapotaka kuhamia kuachwa solemba kwa kujibiwa kwamba huko anakotaka kuhamia hakuna nafasi kwa vile ilishajazwa.

Hayo ni kwa uchache tu.

Utumishi ni taasisi iliyo chini ya ofisi ya rais lakini madudu yao yanayofanyika pale utadhani haipo chini ya hiyo ofisi kubwa kabisa. Tunamwomba rais apamulike vizuri hapo Utumishi ili kuondoa haya malalamiko ya muda mrefu kwani pamoja na ofisi hiyo kuhamia Dodoma hakuna la maana na la kujivunia waliloliboresha.
 
Kila la kheri,ila beba vifuatavyo
1.kitambulisho cha kazi
2.barua zako zote ulizoandika na ulizojibiwa
3.kitambulisho cha taifa
4,barua ya ruhusa
5,passport size 4
mwisho kabisa ondoa woga,pale getini kwa mkulu,urambe vizuri,kama unalo shato jeupe na tai,itapendeza zaidi
mwisho wa mwisho usisahau kutujuza yatakayojiri huko,viambata nilivyokwambia ni muhimu kwa usalama wako binafsi.
Kila la kheri mkuu.
Jitahidi pengine wewe utasikilizwa maana kila Bin Adam na nyota yake!

Mie ninao mfano.
Kaka yangu alistaafu mwaka 2008 na kugundua alikuwa amepunjwa.

Akaanza kufuatilia kwa DED na hatimaye akaandika barua kwa Mh. Rais na kusambaza nakala kwa wahusika wote. Hivi niandikavyo hajajibiwa.

Usikate tamaa, nenda tu bwana.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wadau mm kwa takribani mwaka nimekuwa nikihangaika kufuata familia yangu kwa kuomba uhamisho.

Taratibu zote za maombi zimefanyika na kule ninakotaka kuhamia wamenijibu nafasi ipo kabisa na nimeomba wameniruhusu.

Barua ikawa imetumwa utumishi ili wapitishe nihame.

Cha ajabu mkurugenzi wa utumishi akanijibu majibu yasio ya kiutumishi kabisa bila kujua kuwa kuna siku waziri mkuchika alikemea watumishi wanaokwamisha uhamisho wa watumishi. Na kusema kuwa mtumishi anaweza kufanya kazi sehemu yeyote ile nchini kwa hiyo hakuna haja ya kuwanyima uhamisho kwani wakiomba kibali cha kuajiri mbadala watapata kwa kuwa Serikali ndio ina ajiri.

Sasa nimeamua kufanya maamuzi magumu kabisa.

Jumanne ya tarehe 9.4.2019 nitatembea kutoka mkoani pwani hadi Ikulu ya Rais jijini dar es salaam kwa lengo la kumuomba Rais wetu mpendwa kuingilia kati suala langu.

Wakuu naombeni ushauri wenu , niende ikulu kwanza au nianze kwa katibu mkuu utumishi ( dkt ndumbalo)?

Vile vile yule mkurugenzi amekuwa akitoa uhamisho kwa upendeleo kabisa.

Mimi nataka nikamwambie Rais wetu yote yanayotendeka pale utumishi.

Watumishi wa umma wananyanyasika sanaa na hawa watu wachache wasio kuwa na huruma na familia za watumishi.

Mtu anaomba uhamisho na anasema atajigharamia wao wanamuandikia barua ya hovyo hovyo isiyofuata taratibu za kiutumishi.

Sasa nimeamua kumfuata Rais wetu kumueleza yote. Na kumuambia manyanyaso watumishi wanayopata kutoka kwa mkurugenzi wa utumishi kurugenzi ya utumishi na uhamisho kwa watumishi.

Sent using Jamii Forums mobile app
Huna maadili ya utumishi wa uma.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Pole sana, nasikitika kukwambia kuwa uhamisho ni maalum kwa makada wa chama chetu tu
 
Usinikatishe tamaa mkuu, kuna mtu alienda majuzi kuhusu mafao, leo hii ana injoy mafao yake.

Kitendo cha Mimi kuonekana ikulu tu na vyombo vya habari kunimulika ni ujumbe tosha kwa viongozi waliopewa dhamana wajitathimini.

Kama wewe ni mtumishi wa umma, basi fuata chain of command.

Kwa tatizo hilo Ikulu hutapata access, utaishia kuliona gate tu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu mimi sijakitatisha tamaa, nimekupa ushauri kama ulivyoomba.

Una kila haki ya kukubali au kukataa. Pia usipende kupewa ushauri unaoendana na mapendekezo yako pekee, maana kama ni hivyo basi usiongeomba ushauri badala yake ungeomba tukutie moyo kwenye huo uamuzi wako.
Usinikatishe tamaa mkuu, kuna mtu alienda majuzi kuhusu mafao, leo hii ana injoy mafao yake.

Kitendo cha Mimi kuonekana ikulu tu na vyombo vya habari kunimulika ni ujumbe tosha kwa viongozi waliopewa dhamana wajitathimini.



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom