Nataka nianzishe kitu kuendana na kipaji changu naombeni ushauri

Mimi ni kijana mdogo tu nipo chuo Dar es salaam nmemaliza certificate saivi naingia diploma one. Kiukweli kitu nachokisomea nasomea tu kwa sababu nmekifaulia kwenye masomo yangu ya kidato cha nne na ni kitu nilichokifatilia nikakielewa nikabidi nikisome lakini ninapenda sana na ninajua kuchezea mambo ya computers na simu hizi mara nyingi zikipata matatizo mtaani kwetu ata kila sehemu nitayoenda kuishi, mimi ndio huwa nakuwa mjuzi wa kutengeneza tatizo lolote ( tatizo sio la kwenye mitambo yani kufungua nati na kuanza kutengeneza ila ni kutengeneza mifumo ya umo umo ndani ya simu au computer ) najaribu kutengeneza graphics designing na najikuta naziweza kama mtu niliesomea graphics designing. Nakipaji cha kuchora pia. Sasa nafikiria kuanzisha kitu chochote kutumia ujuzi na kipaji changu kiweze kuniingizia pesa maana naona kabisa ninao uwezo wa kufanya vitu vikubwa kutumia kipaji changu na nikawa kama mtu niliesomea. Naombeni ushauri wenu kwa hili. Na nishamaliza mwaka wa kwanza bado miwili ya kukaa Dar es salaam kwenye fursa. Asanteni!
Mifumo ipi unatengeza au unafanya setting??
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom