Nataka kwenda China kununua nguo na kuleta Dsm, Naombeni ushauri.

MORIAH

Senior Member
Aug 13, 2012
103
51
Heshima yenu wakubwa.
Wakubwa nina mil 10 ya kwenda kununua nguo china na kuja kuuza hapa mjini. Yupo rafiki yangu ambaye nyumba zetu zimepakana ameahidi kwenda na mimi na kunisadia huko China na mpaka tunarudi nitaweka nguo kwenye stoo yake palemwenge kwa muda na kuziuza kwa wateja wake hapa dsm ambao ni wateja wake wa zamani.

Huyu jamaa ni rafiki yangu sana hata watoto wake watatu wanakaa sana kwangu na mtoto wangu anachezna kwake.wanasoma shule moja. Sote tunaishi mbezi Tangi mbovu.

Yeye ni mfanyabiashara alianza na nguo akaja simu sasa yuko kwenye magari. Fedha zimemkubali. China anaenda mara mbili au tatu kwa mwezi. Anachukua vitu tofauti tofauti sana. Ana wateja wengi wa kila bidhaa.

Sasa naombeni ushauri wenu mtu ambaye watoto wetu ni marafiki, mimi na yeye na marafik, wake zetu ni marafiki nyumba zetu zimepakana na tuna miaka zaidi ya 6 kama majirani anaweza kunitapeli kweli? Au naombeni mnishauri risk ambazo zinaweza kunikuta ktk biashara hii. kwa wazoefu.Nimewahi kwenda nje ya bara la afrika lakini siyo kwa biashara. Asanteni kwa msaada wenu.
 
:confused2::confused2::confused2::confused2::confused2::confused2::confused2::confused2::confused2::confused2::confused2:

USIPIME MAENDELEO YA WATU KIHIVYO NA UKATAKA KUIGA.......HUKO CHINA SIKU HIZI KUNA BIASHARA ZA HATARI SANA.....FANYA UTAFITI WAKO MWENYEWE KANDO NA USHAURI NA USHAWISHI WAKE.......NA IWAPO MTASAFIRI USIKUBALI AKUPE "EXTRA" BAGGAGE UMSAIDIE MAKILO KWENYE KUCHECK IN........HAPO NDIO UNABEBESHWA BWIMBWI BILA KUJUA
 
:confused2::confused2::confused2::confused2::confused2::confused2::confused2::confused2::confused2::confused2::confused2:

USIPIME MAENDELEO YA WATU KIHIVYO NA UKATAKA KUIGA.......HUKO CHINA SIKU HIZI KUNA BIASHARA ZA HATARI SANA.....FANYA UTAFITI WAKO MWENYEWE KANDO NA USHAURI NA USHAWISHI WAKE.......NA IWAPO MTASAFIRI USIKUBALI AKUPE "EXTRA" BAGGAGE UMSAIDIE MAKILO KWENYE KUCHECK IN........HAPO NDIO UNABEBESHWA BWIMBWI BILA KUJUA

Nashukuru mkuu,
Lakini mimi ndiye ninayemwomba yeye na siyo yeye ananishawishi. Yeye wala hana interest ya kwenda mimi. Mimi ndo namwomba kwa sababu mimi nataka kubadilisha biashara. Nimechoka na biashara ndogo ya duka la nguo hapa mwenge.
 
Kaka nina amini kwamba kama kweli ni jirani yako na marafiki kiasi hicho hatakutapeli. Kinachotakiwa wewe si umesoma na utakwenda kwenye maduka naye na baadae ukiishazoea maeneo ya kununua nguo au bag au viatu utakuwa unakwenda mwenyewe na kurudi mwenyewe.
Uwe na imani japo kweli mara nyingi nimeshuhudia hata ndugu anamchukulia mzigo ndugu ambaye amemuomba amletee ngu na anamleta mbaya ajabu lakini zake ni nzuri na ni huyo ninayezungumza hapa ni ndugu yangu mtoto wa shangazi yangu alimfanyia hivyo nduguye. Katoa hela nyingi nanguo zikaletwa mbaya haziuziki.
Lakini wewe unakwenda naye so kwa vile wenzetu kule ni waaminifu nina imani hawatakubali kushawishiwa kubadilisha bei wewe uuziwe juu kwa kushawishiwa na jirani yako. Kama jirani yako amefanikiwa kiasi ulichoeleza basi usihofu hatakutapeli.

Funga siku moja kwa maombi maalumu na muombee na familia yake na kisha ondoka na jirani na rafikiyo, Mungu atakuinua kaka yangu.
Tuambie ukirudi umeleta nini na kisha tuleteee vitu tutakuunga mkono kwa kunua simu yangu ni 0713 68 96 65.
Asante na nakutakia safari njema
 
Kaka nina amini kwamba kama kweli ni jirani yako na marafiki kiasi hicho hatakutapeli. Kinachotakiwa wewe si umesoma na utakwenda kwenye maduka naye na baadae ukiishazoea maeneo ya kununua nguo au bag au viatu utakuwa unakwenda mwenyewe na kurudi mwenyewe.
Uwe na imani japo kweli mara nyingi nimeshuhudia hata ndugu anamchukulia mzigo ndugu ambaye amemuomba amletee ngu na anamleta mbaya ajabu lakini zake ni nzuri na ni huyo ninayezungumza hapa ni ndugu yangu mtoto wa shangazi yangu alimfanyia hivyo nduguye. Katoa hela nyingi nanguo zikaletwa mbaya haziuziki.
Lakini wewe unakwenda naye so kwa vile wenzetu kule ni waaminifu nina imani hawatakubali kushawishiwa kubadilisha bei wewe uuziwe juu kwa kushawishiwa na jirani yako. Kama jirani yako amefanikiwa kiasi ulichoeleza basi usihofu hatakutapeli.

Funga siku moja kwa maombi maalumu na muombee na familia yake na kisha ondoka na jirani na rafikiyo, Mungu atakuinua kaka yangu.
Tuambie ukirudi umeleta nini na kisha tuleteee vitu tutakuunga mkono kwa kunua simu yangu ni 0713 68 96 65.
Asante na nakutakia safari njema

Asante sana, nikirudi nitakupigia. Nitaleta ama nguo ama simu. Hii ni baada ya kupata oder. Yeye mwenyewe atanizungusha kwa wateja wake wa zamani halafu kulingana na mahitaji yao ndo nitaleta vitu hivyo. Nashukuru kwa kutangaza kuniunga mkono. Nimechukua naomba yako asante sana.
 
Pia hakikisha kweli huyu unaeenda naye ni mwenye upendo asiye na chuki! nasema hivyo kwa kuwa kuna watu wengi tumeshuhudia wakifika kule wanawaacha wenzao wageni kutowaonyesha/ au kuwaelekeza kwa haraka haraka ukizingatia wenzao ni wageni, hivyo ni bora uwe unamfahamu vizuri tabia yake.
 
Pia hakikisha kweli huyu unaeenda naye ni mwenye upendo asiye na chuki! nasema hivyo kwa kuwa kuna watu wengi tumeshuhudia wakifika kule wanawaacha wenzao wageni kutowaonyesha/ au kuwaelekeza kwa haraka haraka ukizingatia wenzao ni wageni, hivyo ni bora uwe unamfahamu vizuri tabia yake.

Sijawahi kutofautiana naye. Yeye mwenyewe alipelekwa china na mtu mwingine mara tatu tu. Baada ya pale aliachwa peke yake na alianza na mil 5. Ameahidi kwenda na mimi mara tatu tu pia. Baada ya hapo ameniambia ataanza kunichaji hata hiyo stoo ninayoweka nguo zangu.
 
Sijawahi kutofautiana naye. Yeye mwenyewe alipelekwa china na mtu mwingine mara tatu tu. Baada ya pale aliachwa peke yake na alianza na mil 5. Ameahidi kwenda na mimi mara tatu tu pia. Baada ya hapo ameniambia ataanza kunichaji hata hiyo stoo ninayoweka nguo zangu.

:confused2::confused2::confused2::confused2::confused2::confused2:
 
Sa mbona mie unaniambia nianzishe airtel money, tigo na mpesa kwa kiasi hicho hicho cha fedha? Au tuwasiliane tujue cha kufanya??
 
Kwa maoni yangu hii biashara haiwezekani kwa sababu huna uzoefu.

acha umang'aaaa chaliii angu eti,!! Hii coment yako ni ya kitoto sana,uzoefu gan unaozungumzia?yeye ana uzoefu na aanuza nguo mwenge ila ananunulia hapa bongo,sasa anataka azifute huko huko wanakotoa wenziae acha woga jombaaa !
 
Bora uende naye mwaya na uwe makini yalionikuta yale ya kuagiza usisubutu kumpa pesa atauwe unalala naye kitanda kimoja rafiki anaweza akakugeuka ukajutaaa niliulize mimi nalia mpaka keshoooooooooo na nguo sijapata
 
Mi nakushauri nenda nae ila inabidi kuwa mwangalifu,watu wanajali pesa siku izi sio utu.

Ondoa hofu kila kitu sa ivi ni kurisk,lasivyo utajikuta huna maendeleo kwa uoga.

Good luck
 
Asante sana, nikirudi nitakupigia. Nitaleta ama nguo ama simu. Hii ni baada ya kupata oder. Yeye mwenyewe atanizungusha kwa wateja wake wa zamani halafu kulingana na mahitaji yao ndo nitaleta vitu hivyo. Nashukuru kwa kutangaza kuniunga mkono. Nimechukua naomba yako asante sana.

I wish you all the best. kumbuka ulete vitu kwenye December week ya kwanza na ya pili hivi ndio nitakuwa na hela
 
mkuu anza hiyo biashara inalipa sana mimi nilishawai msindikiza mtu bangkok thailand akanunua nguo na pochi nzuri tu kule cheap sana,na leo yuko mbali sana,endelea usikate tamaa
 
Nenda ukapate uzoefu wa hiyo biashara ila kuwa makini sana na pesa yako usimkabidhi yeye akushikie ila muombe akuelekeze kila kitu ufanye mwenyewe ili siku nyingine uweze kwenda mwenyewe bila ya tatizo lolote. Usiache kumuomba Mungu maana ndiye atakayekuwezesha.

Nakutakia kila la kheri ndugu!!!
 
Back
Top Bottom