kiraza
JF-Expert Member
- Jun 6, 2016
- 353
- 480
*Mimi ni kijana wa umri wa miaka 25, naishi dar es salamm Bado sijaoa.
Dhumuni la kuja hapa jukwaani mbele yenu leo hii ni kuomba msaada wa kuujua Uchawi/Nguvu za kiroho ziliyo na matokeo ya wazi katika maisha haya.
ONYO.
Katika thread hii sitapenda kusikia kabisa habari za Mungu,
Sababu za kutopenda kusikia neno hili ni kwa sababu nimeshaishi sana
maisha ya kumuomba na kumtumaini bila mafanikio, Kwangu mimi Mungu amekuwa kimya
kabisa na hajajibu lolote tangu nilipoanza kumuomba zaidi ya kuzidi kupata
changamoto na mikosi lukuki.
Hivyo kwa kwa mshauri yoyote hapa nitaomba anipe na anifunze habari labda za Mungu mwingine mwenye nguvu za wazi akiombwa kwa dhati., na si hii Miungu iliyo Maarufu katika jamii hizi tunazoishi.
Kwa ufupi mambo fulani yaliyonisukuma kuja kuomba msaada huu na yafuayo ni baadhi.
1. Bila kuwa na nguvu yoyote ya kiroho huwezi kuishi kwa raha na amani maishani mwako
zaidi utakuwa ukiwasindikiza wenye uwezo fulani wa kiroho.
2. Katika uchunguzi wangu nimebaini kuwa wanadamu wengi wenye roho ambazo hazina huruma kirahisirahisi, mazulumati, waonezi wa wanyonge ndio wenye mafanikio makuu kimaisha.
ukilinganisha na watu wa kawaida wanaochakaa kwa dhiki huku wenye ahueni
wakipambana na shida, hasa ya Pesa na magonjwa
3. Watu wengi wenye mafanikio ni watu wasiri ambao hawana pupa kwenye kila jambo na hata kwenye kutoa msaada, watu hawa huwa hawatoi misaada hovyo hovyo, huwa wanatoa misaada kwa sababu maalum, tofauti na mtu wa kawaida anavyopita Kariakoo na kuwagawia ombaomba
hela kidogo aliyonayo.
Hivyo kwa sababu hizo na nyingine lukuki nilizonazo kichwani nimeamua kuchukua Uamuzi huu wa,KUTAFUTA JINSI YA KUPATA ELIMU YA UCHAWI/NGUVU ZA KIROHO.
Maana katika kufikiria nimepata wazo kuwa Nguvu za kiroho ndizo zinazofanya mabadiliko ya mwili.
Hivyo kwa mtu yoyote ambaye anadhani ana uwezo wa kunisaidia kuhusu kunifunza elimu hizi naomba sana msaada wake, nipo radhi hata kupotea kwa miaka na kurudi huku nikiwa nimekamilika kimwili na kiroho ili niweze kuishi na hizi nafsi za wanadamu kwa raha.
NB: Elimu ninayoilenga sio ya kuitoa familia yangu sadaka, maana familia yangu hasa ndiyo lengwa kwenye mafanikio yangu.
Kwa yeyote anayeweza kunisaidia naomba aniPM.
ASANTE
Dhumuni la kuja hapa jukwaani mbele yenu leo hii ni kuomba msaada wa kuujua Uchawi/Nguvu za kiroho ziliyo na matokeo ya wazi katika maisha haya.
ONYO.
Katika thread hii sitapenda kusikia kabisa habari za Mungu,
Sababu za kutopenda kusikia neno hili ni kwa sababu nimeshaishi sana
maisha ya kumuomba na kumtumaini bila mafanikio, Kwangu mimi Mungu amekuwa kimya
kabisa na hajajibu lolote tangu nilipoanza kumuomba zaidi ya kuzidi kupata
changamoto na mikosi lukuki.
Hivyo kwa kwa mshauri yoyote hapa nitaomba anipe na anifunze habari labda za Mungu mwingine mwenye nguvu za wazi akiombwa kwa dhati., na si hii Miungu iliyo Maarufu katika jamii hizi tunazoishi.
Kwa ufupi mambo fulani yaliyonisukuma kuja kuomba msaada huu na yafuayo ni baadhi.
1. Bila kuwa na nguvu yoyote ya kiroho huwezi kuishi kwa raha na amani maishani mwako
zaidi utakuwa ukiwasindikiza wenye uwezo fulani wa kiroho.
2. Katika uchunguzi wangu nimebaini kuwa wanadamu wengi wenye roho ambazo hazina huruma kirahisirahisi, mazulumati, waonezi wa wanyonge ndio wenye mafanikio makuu kimaisha.
ukilinganisha na watu wa kawaida wanaochakaa kwa dhiki huku wenye ahueni
wakipambana na shida, hasa ya Pesa na magonjwa
3. Watu wengi wenye mafanikio ni watu wasiri ambao hawana pupa kwenye kila jambo na hata kwenye kutoa msaada, watu hawa huwa hawatoi misaada hovyo hovyo, huwa wanatoa misaada kwa sababu maalum, tofauti na mtu wa kawaida anavyopita Kariakoo na kuwagawia ombaomba
hela kidogo aliyonayo.
Hivyo kwa sababu hizo na nyingine lukuki nilizonazo kichwani nimeamua kuchukua Uamuzi huu wa,KUTAFUTA JINSI YA KUPATA ELIMU YA UCHAWI/NGUVU ZA KIROHO.
Maana katika kufikiria nimepata wazo kuwa Nguvu za kiroho ndizo zinazofanya mabadiliko ya mwili.
Hivyo kwa mtu yoyote ambaye anadhani ana uwezo wa kunisaidia kuhusu kunifunza elimu hizi naomba sana msaada wake, nipo radhi hata kupotea kwa miaka na kurudi huku nikiwa nimekamilika kimwili na kiroho ili niweze kuishi na hizi nafsi za wanadamu kwa raha.
NB: Elimu ninayoilenga sio ya kuitoa familia yangu sadaka, maana familia yangu hasa ndiyo lengwa kwenye mafanikio yangu.
Kwa yeyote anayeweza kunisaidia naomba aniPM.
ASANTE