Nataka kupima ngoma

KAKA,KAMA VIPI usiende!
naona kama ITAKUSUMBUA

...nimeshtukia watu wengi ukiwaambia unataka kupima ngoma wanashabikia, "kapimee, kapimee!" ...kulikoni? au ndio burudani kumuona mwenzenu 'anaishi kwa matumaini' ? :D
 
Mkuu Kafara, is this a fact?

Mkakati usio wa kidaktari maana yake nini? tuwe serious wazee, najua kuna watu kibao humu ndani wanaface same issue kama Yo Yo na wameuchuna huku wakifuatila kila ushauri unaotolewa hapa.

So, tell us more...nipo interested na hii

nipo siriasi kwa sana tu. neno "simpo" lisikuzenguae ila zingatia tahadhari niliyoweka kwamba si mkakati wa kidaktari.

mkakati usio wa kidaktari=usio wa kitaalamu. sipendi kusema usio wa kisayansi kwani naamini ni wa kisayansi ila tafsiri yangu ndio inaweza kuwa imekwenda kombo.

ni hivi. kama mtu upo fit na hakuna matatizo ya kiafya ya wazi yanayokukabili ukipima mkojo na ukaona hizo white blood cells ni nyingi basi ujue uwezekano mkubwa afya yako inamgogoro. sasa mgogoro huo unaweza ukawa hiv au kitu kingine ambacho bado hakijajitokeza. ndio maana nikauita mkakati wa kukupa ujasiri wa kwenda hatua nyingine yani kupima kama utakuwa umeona white blood cell zipo kiwango cha kawaida. natumaini umenipata.
 
uongo kabisa.

uongo kabisa kwa nini?
kwani si kweli kwamba white blood cells zikiwa
nyingi kwenye mkojo haziashirii tatizo la kiafya?
kumbuka sikusema ukipima mkojo utajua status yako
ya hiv bali nimesema itakupa ujasiri wa kupima hiv.
 
mkakati simpo (usio wa kidaktari) wa kupata ujasiri wa kupima ngoma ni kwa kuanza na kupima mkojo. ukiona white blood cells zipo nyingi ujue uwezekano wa ngoma upo juu lol halafu mkojo unaweza pima hata home tu.

Du hii kali...white blood cells in urine shows presence of lentivirus !!!! this should be a nature paper. Hii ni ya kuongea kwenye karata, madraft, mabao na kwenye vijiwe..
 
uongo kabisa kwa nini?
kwani si kweli kwamba white blood cells zikiwa
nyingi kwenye mkojo haziashirii tatizo la kiafya?
kumbuka sikusema ukipima mkojo utajua status yako
ya hiv bali nimesema itakupa ujasiri wa kupima hiv.
kuna matatizo elfu moja ya kiafya yaweza kusababisha kuongezeka white blood cells kwenye urine, kwa hiyo kisa cha kufikiria ngoma?! na sio UTI au hizo conditions zingine 998?
 
Du hii kali...white blood cells in urine shows presence of lentivirus !!!! this should be a nature paper. Hii ni ya kuongea kwenye karata, madraft, mabao na kwenye vijiwe..

hahahah wataalamu bwana! yaani wewe unakimbilia kusema mambo ya karata
wakati mie nimesema masuala ya white blood cells? labda useme kwenye mkojo
hakuna hayo ya whiteblood cells!

unanikumbusha ile habari ya mtaalamu wa masuala ya anga alipokwenda camping na binamu yake ambaye "shule haikupanda sana" usiku wakaweka hema wakalala. usiku wa manane binamu anashtuka na kumuamusha mtaalamu na kumuuliza kama kuna tofauti yoyote aliyoiona, mtaalamu akaanza kueleza mpangilio wa nyota ambao anauona nk. nk. yule binamu akamwambia "mkuu
tumeibiwa hema!" hahahahahaa
 
Last edited:
kuna matatizo elfu moja ya kiafya yaweza kusababisha kuongezeka white blood cells kwenye urine, kwa hiyo kisa cha kufikiria ngoma?! na sio UTI au hizo conditions zingine 998?

haya ndio maneno. sio kusema tu "uongo kabisa" kwa herufi nyekundu.
si unaona unanielimisha kwamba uti na condizions nyingine zote zinaweza
kukupata wakati wewe mwenyewe mwili bado upo fit.

aidha maneno yangu sio uongo kabisa kwani ngoma ni mojawapo ya
hizo conditions 1000.
 
haya ndio maneno. sio kusema tu "uongo kabisa" kwa herufi nyekundu.
si unaona unanielimisha kwamba uti na condizions nyingine zote zinaweza
kukupata wakati wewe mwenyewe mwili bado upo fit.

aidha maneno yangu sio uongo kabisa kwani ngoma ni mojawapo ya
hizo conditions 1000.

Teh teh teh, nilikuwa naweka msisitizo kwa sababu hiyo itapoteza watu.
Anyways, tuko pamoja, PEACE AND LOVE!
 
uongo kabisa kwa nini?
kwani si kweli kwamba white blood cells zikiwa
nyingi kwenye mkojo haziashirii tatizo la kiafya?
kumbuka sikusema ukipima mkojo utajua status yako
ya hiv bali nimesema itakupa ujasiri wa kupima hiv.

...Kafara, una uhakika unazungumzia (WBC count) kwenye mkojo, na sio kwenye damu?

...kwa ufahamu wangu, (basic) wawezajua White Blood Cell, na Red Blood Cell counts kwenye ESR test, (erythrocyte sedimentation rate).

...ukikuta chembe za damu kwenye mkojo, huenda kuna athari kwenye kibofu, figo...nk... (au kichocho!) :)
 
Du hii kali...white blood cells in urine shows presence of lentivirus !!!! this should be a nature paper. Hii ni ya kuongea kwenye karata, madraft, mabao na kwenye vijiwe..
Shem hii ni bongo kila kitu kinawezekana....

...bado nafikiria kupima......dadako wa kisukuma analazimisha sana....nishazua safari zisizo rasmi ili kukwepa lakini kazidi kukomaa....
 
Shem hii ni bongo kila kitu kinawezekana....

...bado nafikiria kupima......dadako wa kisukuma analazimisha sana....nishazua safari zisizo rasmi ili kukwepa lakini kazidi kukomaa....

Kumbe ulikuwa na sababu maalum! Hapo huna ujanja ... kubali yaishe.
 
Kumbe ulikuwa na sababu maalum! Hapo huna ujanja ... kubali yaishe.
kama sitaki hata zije lori 800 za fidifosi sipimi....dadake masanilo kakomaa kinoma wiki hizi 2 kanifanya nikose raha....
 
kama sitaki hata zije lori 800 za fidifosi sipimi....dadake masanilo kakomaa kinoma wiki hizi 2 kanifanya nikose raha....
Kubali yaishe mapema kuliko kujipa pressure. Nenda peke yako kwanza kama una wasiwasi sana. Mambo yakiwa fresh ndio unaenda naye kwa mara ya pili kama anataka ku-confirm.
Ukigoma kabisa atajua 100% uliuza timu, hapo sasa na yeye kuuza inakuwa nje nje, halafu kama mlikuwa hamjaingia kwenye gridi ndio kwanza mnajitega wenyewe kwenye network.
 
Shem hii ni bongo kila kitu kinawezekana....

...bado nafikiria kupima......dadako wa kisukuma analazimisha sana....nishazua safari zisizo rasmi ili kukwepa lakini kazidi kukomaa....

Hahahah pima baba na matokeo tuyaone bwana....
 
Sio kichekesho hicho we pwagu wewe. Yo Yo akikutwa ana kinga ya asili basi aendeleze kufanya mapenzi "dry...mbichi mbichi" aeneza mdudu na kuua, kwa vile yeye ana kinga, unadhani utani huo? Halafu unajichekesha. Mijitu mingine sijui imejaa mataputapu na turkey stuffing ndani ya fuvu?

LOL...:):) Mkuu Dilunga Yo Yo akikuta kuwa yeye aathiriki atawaambukiza vipi ambao hawajaambukizwa...:rolleyes:Ninawafahamu baadhi ya watu ambao wenzi wao wamekufa kwa AIDS lakini wao wanadunda na wameolewa na wao ni negative upo?
I REMAIN
 
...Kafara, una uhakika unazungumzia (WBC count) kwenye mkojo, na sio kwenye damu?

...kwa ufahamu wangu, (basic) wawezajua White Blood Cell, na Red Blood Cell counts kwenye ESR test, (erythrocyte sedimentation rate).

...ukikuta chembe za damu kwenye mkojo, huenda kuna athari kwenye kibofu, figo...nk... (au kichocho!) :)

mbu wbc zinapatikana kwenye urine sio lazima damu.
ila kama alivyoeleza mtaalamu saikosis hapo juu hii inaweza
kusababishwa na maradhi mbali mbali. kwa hiyo kama wajiona upo
fit lakini hizo wbc zimekutwa kwenye mkojo ndo ujue wewe iko gonjwa na unahitaji vipo zaidi. sasa ukikuta count ya wbc zipo chini (kama kipo kiwango
kinachokubalika) basi wewe waweza anza mbele na kipimo cha ngoma lol
 
Back
Top Bottom