nataka kuongea na mwenye mbwa na sio mbwa!

Jakubumba

JF-Expert Member
Mar 5, 2011
1,624
500
Wanajf nina jirani yangu kwa kweli ananikera sana kwa matusi yake nje na ndani ya familia yake mwenyewe! Najua hata humu watu kama hawa wapo hivo tuwape somo waachane na matusi.
Jirani ana watoto watatu na majina yao anayajua lakini anawaita majina ya wanyama;
mtoto wa kwanza anaitwa juma......huyu akimhitaji utasikia anasema wewe mbwa kuja haraka!
mtoto wa pili anaitwa Alli......akimhitaji utasikia anasema wewe nyani kuja haraka
mtoto wa tatu anaitwa anaitwa rose....huyu utasikia wewe nyang'au uko wapi?

Kilichotokea sasa! Juma alipigana na mtoto wa jirani yetu, kwa kweli jirani yetu alikasirika sana na akamfuata mama yake juma kumueleza amkanye mwanae, gafla akakutana na juma mlangoni, juma akamjibu vibaya sana ndo na yeye akaudhika akamwambia nataka kuongea na mwenye mbwa na sio mbwa. Kumbe mama yake juma anamesikia...Ulikuwa ni ugomvi mkali sana kwa nini mwanae aitwe mbwa!

Jamani wanajf tuwaitewatoto wetu majina tuliyowapa tusiwabatize majina kutokana na midomo yetu michafu!
 
Sijui kama ni kweli .. Niliwahi sikia kama ukiwa unamwita mwanae majina ya wanyama wakiwa wadogo huwa wanakuwa na tabia kama zao .... siamini hili ..
 
Afadhali umenena hili...tuchunge sana maneno ya kinywa chetu kwa kua kuna leo na kesho...nilipata kuitwa mbwa na jirani wa sehemu fulani ambayo nilikua nafanya kazi na km hilo halitoshi akataka nimpe mawasiliano ili aongee na aliyenifuga!...
 
Haya mambo yapo kwenye jamii nyingi tu, hasa matusi kwa watoto wetu kutumia majina ya wanyama. Jamani hii tabia si nzuri
 
Pamoja na majina ya wanyama kama hayo ya mbwa, nguruwe, ngombe, mbuzi...vile vile nimesikia watoto wakiiitwa jini,shetani, firauni, , ibilisi...majina ya viumbe waliolaaniwa. Sio vzuri hata kidogo kumlaani mtoto.
 
huyo Mama Mwenye watoto nae atakuwa ushuzi tu.
Kwanza wanawe wawili kazaa na muislamu kisha huyo wa mwisho kazaa na Mkristo.
So nachelea kusema huyo ni muuza nyama tu...asikupotezee Muda kumfikiria, ana stress za maisha.
 
Back
Top Bottom