Mtambuzi
Platinum Member
- Oct 29, 2008
- 8,810
- 15,398
Bila shaka hata wewe umeshawahi kukutana na kauli kama hii kutoka kwa wanaume, wengi wao wakiwa ni wale ambao umri unazidi kusonga lakini wakiwa bado hawajapata wenza wa kuoa na kujenga familia. Wengi huamini kwamba, kuna mwanamke mahali, ambaye hana kasoro na atakuja kutana naye siku moja.
Wengine wana hofu ya majukumu, hasa ya kulea watoto. Kutokana na malezi yao au kile wanachokijua kuhusu watoto, baadhi ya vijana huamini kwamba, kulea watoto ni jambo gumu sana. Lakini wengine wanaamini kwamba, hata mke anapaswa kulelewa kama ilvyo kwa mtoto. Hivyo wanaamua kutafuta kwanza uwezo ambao haupatikani kiurahisi. Kuna wengine, ambao wamefundishwa au kuelekezwa na mila na desturi zao kwamba, kabla hawajaoa, ni lazima wawe na nyumba kwanza , tena kwao. Kwa hiyo, hawa hadi waje wapate uwezo wa fedha wanakuwa wameshachelewa. Kwa baadhi ya wanaume, maisha bila ya ndoa wanayaona kuwa ndiyo bora kuliko yale ya ndoa.
Zamani, kuoa ilikuwa ni kama lazima na mtu ambaye angefikisha umri fulani bila kuoa angelaumiwa na kulaumiwa sana na jamii. Hata kuaminika kwake kungekuwa ni kwa mashaka. Siku hizi suala hili ni la mtu binafsi, siyo la jamii tena. Kwenye miaka ya 1970 wanaume wote wenye umri wa miaka 25 walikuwa tayari wameoa. Siku hizi, umri wa kuoa umefikia miaka kati ya 28 dadi 30. Hata wanaooa katika umri huo, ni chini kabisa ya nusu.
Wale wanaokaa pamoja kwa muda mrefu kama wapenzi , imebainika kwamba, huwa hawaji kuoana baadaye. Kinachotokea ni mwanaume kuoa mwanamke mwingine. Tafiti zinaonesha kwamba,wanawake wengi hivi sasa huishi kwanza na hawara au rafiki zao wa kiume kabla hawajaolewa. Kisa ni kwamba, wanaume hao wanaoishi nao, wanajaribu ndoa, au kufanya ndoa ya majaribio kama wanavyoita.
Wanapoishi pamoja bila ndoa, kichwani kwa mwanamke kuna kitu kinamwambia kwamba, 'huo ni ushindi, kwani ndoa itafungwa,' wakati kwa mwanaume anajua basi, maisha ndiyo hayo na hakuna haja ya ndoa tena.
Wengine wana hofu ya majukumu, hasa ya kulea watoto. Kutokana na malezi yao au kile wanachokijua kuhusu watoto, baadhi ya vijana huamini kwamba, kulea watoto ni jambo gumu sana. Lakini wengine wanaamini kwamba, hata mke anapaswa kulelewa kama ilvyo kwa mtoto. Hivyo wanaamua kutafuta kwanza uwezo ambao haupatikani kiurahisi. Kuna wengine, ambao wamefundishwa au kuelekezwa na mila na desturi zao kwamba, kabla hawajaoa, ni lazima wawe na nyumba kwanza , tena kwao. Kwa hiyo, hawa hadi waje wapate uwezo wa fedha wanakuwa wameshachelewa. Kwa baadhi ya wanaume, maisha bila ya ndoa wanayaona kuwa ndiyo bora kuliko yale ya ndoa.
Zamani, kuoa ilikuwa ni kama lazima na mtu ambaye angefikisha umri fulani bila kuoa angelaumiwa na kulaumiwa sana na jamii. Hata kuaminika kwake kungekuwa ni kwa mashaka. Siku hizi suala hili ni la mtu binafsi, siyo la jamii tena. Kwenye miaka ya 1970 wanaume wote wenye umri wa miaka 25 walikuwa tayari wameoa. Siku hizi, umri wa kuoa umefikia miaka kati ya 28 dadi 30. Hata wanaooa katika umri huo, ni chini kabisa ya nusu.
Wale wanaokaa pamoja kwa muda mrefu kama wapenzi , imebainika kwamba, huwa hawaji kuoana baadaye. Kinachotokea ni mwanaume kuoa mwanamke mwingine. Tafiti zinaonesha kwamba,wanawake wengi hivi sasa huishi kwanza na hawara au rafiki zao wa kiume kabla hawajaolewa. Kisa ni kwamba, wanaume hao wanaoishi nao, wanajaribu ndoa, au kufanya ndoa ya majaribio kama wanavyoita.
Wanapoishi pamoja bila ndoa, kichwani kwa mwanamke kuna kitu kinamwambia kwamba, 'huo ni ushindi, kwani ndoa itafungwa,' wakati kwa mwanaume anajua basi, maisha ndiyo hayo na hakuna haja ya ndoa tena.