Nataka kumuachisha mke wangu kazi. Naombeni ushauri katika hili

Nipo kwenye ndoa na mke wangu kwa muda wa miaka 5 sasa, mke wangu amekuwa nami bega kwa bega kwa kipindi chote hicho japo changamoto za hapa na pale ni kitu cha kawaida kwenye maisha.

Nimebahatika kujaliwa watoto wawili na mke wangu, wa kwanza akiwa na miaka saba na wiki Ana miaka miwili sasa, na ninamshukuru Mungu watoto wanaendelea vizuri.

Sababu ya kumuachisha mke wangu kazi ni moja tu, mke wangu ni muajiriwa serikalini na hivi majuzi alipata uhamisho wa kushtukiza kwenda Njombe kama kituo chake cha kazi, juhudi mbalimbali zimefanyika ili angalau ahamie karibu imeshindika. Mshahara wake ni wa kawaida.

Nimepanga kukopa mahali hela kama 50M ili nimfungulie biashara kama vile Duka la vipodozi, Vifaa vya ujenzi na Umeme au nimnunulie coaster ambayo itakuwa inamletea kipato kila siku huku akijishughulisha na biashara ndogondogo za hapa na pale hapa nyumbani. Hii ni baada ya kuona mwanamke akiwa mbali na familia uwezekano wa familia hiyo kupotea hususani watoto ni mkubwa kwani asilimia kubwa wanalelewa na dada wa kazi.

Naomba ushauri wenu tafadhali nipo njia panda.
Ninakuunga mkono, kukaa mbali na familia ni kuongeza mzigo wa maisha na hatari ya ndoa kuyumba.
Utalazimika kuwa na mchepuko uvumilivu ukikudhinda au hata yeye kuchepuka.
Lakini wazo la coaster halifai
 
Kwanini wewe usianzishe mradi kuliko ku force mwenzako aache kazi
Msome vizuri jamaa, mleta uzi.
Wala hana nia ya 'kumforce' mke wake aache kazi, bali ameomba ushauri juu ya namna ya kumshawishi wife wake aachane na uhamisho wa kazi ya mbali kuokoa ndoa (family).

Nyie mmeenda mbali sana, mara mseme wazazi wenu wamewasomesha ili muwasaidie, mara what.. hamkumbuki mpo ndani ya mkataba wa ndoa.
 
Wewe unaleta nadharia wenzako tupo field tunalia na nafaka zetu

Tena huko hiyo biashara usifanye kabisa kama kilo ni 900 kumbe afadhali ya huku tunauza 1200, 1300 1400 super 1700

Na faida yake imepungua sana ni 50 to 100 per kg na mzigo hauendi haraka yaani ni majanga mchele mtaani ni mwingi

Kama unabisha jitose kwenye hii biashara utanipa mrejesho.

Sent from my SM-A107F using JamiiForums mobile app
Huyo ni motivational speaker ana mu mislead mwenzake huyo apoteze milion hamsini
 
Msome vizuri jamaa, mleta uzi.
Wala hana nia ya 'kumforce' mke wake aache kazi, bali ameomba ushauri juu ya namna ya kumshawishi wife wake aachane na uhamisho wa kazi ya mbali kuokoa ndoa (family).

Nyie mmeenda mbali sana, mara mseme wazazi wenu wamewasomesha ili muwasaidie, mara what.. hamkumbuki mpo ndani ya mkataba wa ndoa.
Huyo mwanaume na wewe unaye support mtu aache kazi Zama hii hamna jema Wala,Kuna watu wako kazini na miradi yao tele tele na Mambo yanaenda, hafu kwanini utake mke aache kaxi, siaache yeye mwanaume, Mimi Kama mwanamke siwezi acha kaxi na nina watoto na sijui kesho ikoje wanaume wenyewe hamtabiriki nikiacha watakaoteseka ni watoto
Bora aache mwanaume maana kikibuma anaweza kubeba zege, na nyie Mambo yakiwa magumu hukimbia familia. Pia biashara inahitaji uzoefu sasa wewe uchukue 50 milion chah, namwomba Mungu mke wa mleta mada amgomee ujinga wa mumewe Bora waachane
 
Unaweza kuwa na maamuzi ila yasiwe sahihi ndio maana ya kuomba ushauri hapa kwani hapa tunatofautiana mambo mengi sana
Msome jamaa hapa
Msome vizuri jamaa, mleta uzi.
Wala hana nia ya 'kumforce' mke wake aache kazi, bali ameomba ushauri juu ya namna ya kumshawishi wife wake aachane na uhamisho wa kazi ya mbali kuokoa ndoa (family).

Nyie mmeenda mbali sana, mara mseme wazazi wenu wamewasomesha ili muwasaidie, mara what.. hamkumbuki mpo ndani ya mkataba wa ndoa.

Tumeenda mbali kwa sababu kuacha kazi kwa mkewe kutagusa hadi huko mbali unakodhani tumeenda
 
Yani mwanaume anayekupenda ataku support aisee, sasa huyo anaacha kaxi, vipi hao watoto kuanzia bima, Ada za shule biashara ikibuma, au mwanaume akaoa mke mwingine, nadhani kazi akiacha mwanaume inapendeza maana wao kutelekeza familia huwa ni rahisi na hawana uchungu kabisa
Na biashara zilivyo ngumu inakufia muda wowote.
Halafu si kila mtu anaweza biashara.
 
hafu kwanini utake mke aache kaxi, siaache yeye mwanaume, Mimi Kama mwanamke siwezi acha kaxi na nina watoto na sijui kesho ikoje wanaume wenyewe hamtabiriki nikiacha watakaoteseka
Ok mentality yenu ni kwamba neno 'Kazi' ni ile ya kuajiriwa either government or at a certain company yenye high security ya kutokuachishwa, so nikikuambia resign hiyo kazi tuanzishe mradi huu utakataa na utaona sikutakii mema.

I'm your husband,since when nisitake ustawi wa kiuchumi katika familia yangu.? Otherwise kama tunaishi 'kisela' urakuwa na haki ya kukataa na kufanya hivyo unavyosema.
 
Nipo kwenye ndoa na mke wangu kwa muda wa miaka 5 sasa, mke wangu amekuwa nami bega kwa bega kwa kipindi chote hicho japo changamoto za hapa na pale ni kitu cha kawaida kwenye maisha.

Nimebahatika kujaliwa watoto wawili na mke wangu, wa kwanza akiwa na miaka saba na wiki Ana miaka miwili sasa, na ninamshukuru Mungu watoto wanaendelea vizuri.

Sababu ya kumuachisha mke wangu kazi ni moja tu, mke wangu ni muajiriwa serikalini na hivi majuzi alipata uhamisho wa kushtukiza kwenda Njombe kama kituo chake cha kazi, juhudi mbalimbali zimefanyika ili angalau ahamie karibu imeshindika. Mshahara wake ni wa kawaida.

Nimepanga kukopa mahali hela kama 50M ili nimfungulie biashara kama vile Duka la vipodozi, Vifaa vya ujenzi na Umeme au nimnunulie coaster ambayo itakuwa inamletea kipato kila siku huku akijishughulisha na biashara ndogondogo za hapa na pale hapa nyumbani. Hii ni baada ya kuona mwanamke akiwa mbali na familia uwezekano wa familia hiyo kupotea hususani watoto ni mkubwa kwani asilimia kubwa wanalelewa na dada wa kazi.

Naomba ushauri wenu tafadhali nipo njia panda.
Wazo zuri kumfungulia mtaji ila sikushauro kuchukua mkopo kisha kufanya unayotaka fanya, mkopo unachukuliwa kuendeleza biashara iliyopo ila kuanza nayo biashara mpya ni bonge la risk, utapatwa na msongo wa mawazo soon. Kama hamna njia nyingine muache aende kazini huku mkopanga la kufanya. Najua hofu ya kuchapiwa ni kubwa.
 
Ok mentality yenu ni kwamba neno 'Kazi' ni ile ya kuajiriwa either government or at a certain company yenye high security ya kutokuachishwa, so nikikuambia resign hiyo kazi tuanzishe mradi huu utakataa na utaona sikutakii mema.

I'm your husband,since when nisitake ustawi wa kiuchumi katika familia yangu.? Otherwise kama tunaishi 'kisela' urakuwa na haki ya kukataa na kufanya hivyo unavyosema.
Wewe ndo una hyo mentality kuwa kazi ni lazima tu kuajiriwa si kweli, na mazingira ya nchi hii Mambo yasivoekeweka huko government Kuna kaunafuu.
Hafu kuwa husband haimaanishi kuwa uko sahihi pia kwanini usianzishe miradi ikishasimama na muwe wazoefu ndo muache kazi,maana kesi ya jamaa hapo bado hajielewi anakopa milion hamsini hajui chakufanyia anaomba ushauri huku Mara sijui daladala Mara vipodozi KWA msingi huu lazima biashara ife na hawajakulia mazingira ya biashara, why amu force mke, naona hapo jamaa anakaribisha umaskini tu.
 
Na biashara zilivyo ngumu inakufia muda wowote.
Halafu si kila mtu anaweza biashara.
Biashara watu huanza nayo kidogo kidogo na kukua ndo huongeza mtaji. Huyu mwanaume ni mawivu yanamsumbua tu.
Wooi hafu awamu hii jinsi biashara zimedoda kila corner, akianzisha daladala haifikishi mwezi anafilisika
 
Rafiki yangu aliniomba ushauri kama huu wako nilichomshauri hakukifuata,nusura ndoa ivunjike......ongea naye kwanza kama story tu na kujifanya unapanga kuwa na biashara hizo,halafu jifanye unawaza wa kusimamia nani......fanya hesabu zako nayeye ona ni kiasi gani kinaweza kupatikana kwa mwezi,kama mnafanya bega kwa bega anaweza kushauri mwenyewe aache kazi.

Rafiki yangu alimwambia live mkewake hela yako haina mchango kwenye familia,mtiti wake ulikuwa hatari.....bahati nzuri ni watu wangu wa karibu,mkewe direct alinifuata mm......kuna mengi yalitokea ila mkewe amebaki na kazi maisha yanaendelea.......cos mkewe aligundua akiacha kazi mmewe atamnyanyasa kwasababu ya vijisent vyake.
Eti hela yako haina mchango kwenye familia dahh..kwa kweli haikua kauli nzuri
Very wrong assumption
Mtu anaejishughulisha atajinunulia japo mahitaji binafsi na baadhi ya vitu ndani

si sawa na ambae hata chupi na lotion akuombe wewe
 
Zungumza na mkeo mustakabali wa maisha yenu na ndoa yenu, matumizi ya mshahara wake na muwekee mezani maono yako haya uliyoandika, jadilianeni kwa uwazi pasipo wewe kutumia mabavu nae atasema nini yuko hiari nacho, Kama hana kipaji cha biashara usimlazimishe tembeza rushwa asipate uhamisho, Kama anaweza kufanya biashara kwa kuacha kazi akwambie Ni biashara gani ataiweza kuifanya,

Kuna watu humu wanajiandikia tu hata maisha hawayajui, kwa mwanamke graduate asie na ajira je wanaishije? Je kwa wasiokuwa na hata hiyo elimu? Ama je ukipunguzwa kazini ndo mwisho wa maisha?
 
  • Thanks
Reactions: Cyb
Rafiki, unajua kuna vitu vinaenda na umri. Nimepunguza uteja wa Jf, kwa sasa nalea wajukuu rafiki. Ukimuona Kaveli mtolee salamu. Mwambie mimi ni bukheri wa afya.
🙏🙏🙏Rafiki sweet memories that's all is walking inside of me.I hope life will treats you kind and i wish you joy,happiness and love. I will always love you.
 
Rafiki, unajua kuna vitu vinaenda na umri. Nimepunguza uteja wa Jf, kwa sasa nalea wajukuu rafiki. Ukimuona Kaveli mtolee salamu. Mwambie mimi ni bukheri wa afya.

The Patience123 of mine.

Long time sana my lovely sisy babe.

Za masiku? How is everything?

Nafurahi kusikia umzima wa afya. Endelea kufurahi na kutabasamu coz Kaveli is always there for you.

-Kaveli-
 
It is a matter of time kuhama inawezekana kabisa kuliko kumwachisha kazi. Biashara ikiyumba atakuja kukulaumu kwa kuwa ulimwachisha kazi na angeendelea kujipatia kipato cha kulea familia. Mke wangu alipangiwa Mtwara mie nipo Bukoba kwa wahaya. nimekaa naye mbali kwa miaka miine na nusu tunaonana likizo. Alipanga kuacha kazi ili tuishi pamoja but I said no ipo siku Mungu atatufanikisha. Nimefanya route kila likizo Bukoba to Mtwara but now Mungu katenda tupo pamoja mimi nimehama Bukoba na yeye kahama Mtwara tupo tunaishi eneo la ndoto yetu, na maisha yanaendelea.

Biashara inaweza kufa ila sio ajira ya umma vinginevyo ufe wewe
 
Back
Top Bottom