Nataka kujikita kwenye kilimo, zao lipi naweza anza nalo?

Pishoni

Member
Jan 31, 2013
33
24
Habari zenu wadau..

Napenda kilimo kwa kweli..huwa nikipita sehemu nikaiona ardhi nzuri na kando kando pana kijito cha maji..moyo wangu huwa unapepea.
Ni kwa muda nilikuwa nawaza ni kwa namna gani naweza kujikita katika kilimo hasa katika kigezo cha mtaji. Mtaji ulikuwa changamoto, ila namshukuru Mungu nimepata raia mmoja rafiki yangu amekubali kuniwezesha kiasi fulani.. actually atanipiga tafu hadi hapo nitakaposimama mwenyewe.
Nipo Dar.. ila naona kuna fursa shambani.. nimekuwa na mawazo ya kufanya kilimo(cha umwagiliaji) maeneo nje ya jiji ili baadae soko liwe hapa jijini na ikiwezekana na maeneo mengine. Nina ndoto za kuja kuwa mkulima mkubwa hapo baadae ambaye si tu nitaishia kuuza mazao moja kwa moja toka shambani bali kufanya "processing" ili kuongeza thamani..in short nina maono fulani hivi ya kufanya kilimo cha kisasa na usindikaji wa mazao hapo baadae.

Kwa sasa naomba ushauri wenu.. nianze na zao lipi ambalo soko lake linapatikana kiurahisi ukizingatia pesa nitakayopata ni Milioni 5.

maswali ninayojiuliza ni;
1. zao gani nianze kulima kwa kipindi hiki( miezi hii)?
2. Je, gharama zake ni kiasi gani(Kuanzia hatua ya kwanza hadi kuja kuuza) ?
3. Nikiuza nitapata faida kiasi gani?
4. Ni maeneo gani yanafaa kwa hilo zao?
5. etc etc

Naamini wapo ambao wanafanya kilimo nami si wa kwanza katika hili.. ninahitaji ushauri ambao si tu wa hewani-nikipata mtu ambaye ame-anafanya kilimo nitashukuru zaidi..Nimekuwa nikisikia habari nyingi kuhusu kulima VITUNGUU, MATIKITI MAJI, KAROTI,MATANGO na mazao mengine mengi

Nishaurini jamani, nimechoka kukaa sehemu na kulipwa vijisenti kidogo ambavyo havikidhi mahitaji.. najiona kama naji-underutilize mwenyewe wakati ningeweza kufanya vitu vikubwa zaidi ya hapa..

Karibuni..
Natanguliza shukrani..
 
Ushauri wangu ni kwamba ufugajinwa nguruwe unalipa sana, anza kufuga nguruwe ndani ya miezi sita mradi huu utakuwa unajiendesha wenyewe baada ya hapo utaweza kuingia kwenye kilimo moja kwa moja bila kumtegemea huyo mtu anayekusaidia.

Ukishaingia kwenye kilimo, anza na kilimo cha mboga mboga na kisha uanze kupeleka mboga zako super markets za Dar. Ili upate tenda na uwe mtu wa kuaminika hakikisha unakuwa consistent, uwe na mboga kila mteja ataposema upeleke mboga.
 
Anza Na mbogamboga zinazochumika zaidi ya Mara moja..mfano pilipili aina zote.
 
Nikushauri,

Ili uwe mkulima bora.

hakikisha una muda wa kutosha wa kukaa shambani, uwe tiyari kuhama kwenye nyumba yako nzuri na kukaa huko shama jua mvua, pia upate rafiki mtaalamu atakaye kusaidia kutatua changamoto za shamba za kiutaalamu haswa kwenye mimea ya mbogamboga.

Kwa ujumla, nashauri uanze na kitu kama matikiti au kitungu au nyanya, yote ni mazao ya muda mfupi yakidumu miezi mitatu kuanza kutoa matunda, na mwezi moja kitaluni( 3+1=4), pia uliza zao gani ni zuri mahali gani, sio kila zao linafaa kila mahali.

vibarua ni changamoto, watu wasehemu zingine ni wavivu, hivyo ni vyema ukauliza wapi utapata vijana wachapa kazi, na wana hitaji usimamizi mwanzoni wanakuwa hawajua application za dawa na mbolea.

Uwe na mtaji wa kutosha kumuda madawa,mbolea na mambo ya umwagiliaji na kuwalipa vibarua wako. Jifunze kujua risk za kila zao kabla hujapanda, jifunze magojwa yake na ni vizuri kujua dawa zake ili kurahisha wakati wa uhitaji.

Usisikilize sana kuwa zao fulani linalipa sana, wakati mwingine sio kweli, ukweli ni kuwa uwingi wa mazao sokoni kwa kipindi fulani bei mbaya upungufu wake bei nzuri. kwa maana nyingine demand na supply ndiyo determinant wa ubora wa bei. ninachotaka ujue, jifunze trend za mazo na miezi iliyo bora ndiyo ulime.

mfano mwaka 2014 mwezi wa sita kitunguu cha ruaha mbuyuni bei likuwa elfu 35-50 kwa gunia linalozidi kilo 100 pungufu ya kilo 150, lakini mwaka 2015 mwezi sita gunia hilohilo lilikuwa laki 1.5 hadi 2. ukiwauliza watu hao wawili walio lima misumu hiyo watakujibuje kuhusu kilimo? hivyo fanya kazi ya utafiti kidogo upate maarifa.
 
unawazo zuri sana la kuingia kwenye kilimo, kilimo kitakachokutoa haraka sana ni kilimo cha mboga mboga kama nyanya, vitunguu, karoti, na pilipili hoho, mazao haya yanawateja wengi sana na yananunurika na makundi yote namaansha kuwa walio nacho na wasionacho, mimi nina diploma ya kilimo tuwasiliane kwenye namba 0769192358
 
Nikushauri,

Ili uwe mkulima bora.

hakikisha una muda wa kutosha wa kukaa shambani, uwe tiyari kuhama kwenye nyumba yako nzuri na kukaa huko shama jua mvua, pia upate rafiki mtaalamu atakaye kusaidia kutatua changamoto za shamba za kiutaalamu haswa kwenye mimea ya mbogamboga.

Kwa ujumla, nashauri uanze na kitu kama matikiti au kitungu au nyanya, yote ni mazao ya muda mfupi yakidumu miezi mitatu kuanza kutoa matunda, na mwezi moja kitaluni( 3+1=4), pia uliza zao gani ni zuri mahali gani, sio kila zao linafaa kila mahali.

vibarua ni changamoto, watu wasehemu zingine ni wavivu, hivyo ni vyema ukauliza wapi utapata vijana wachapa kazi, na wana hitaji usimamizi mwanzoni wanakuwa hawajua application za dawa na mbolea.

Uwe na mtaji wa kutosha kumuda madawa,mbolea na mambo ya umwagiliaji na kuwalipa vibarua wako. Jifunze kujua risk za kila zao kabla hujapanda, jifunze magojwa yake na ni vizuri kujua dawa zake ili kurahisha wakati wa uhitaji.

Usisikilize sana kuwa zao fulani linalipa sana, wakati mwingine sio kweli, ukweli ni kuwa uwingi wa mazao sokoni kwa kipindi fulani bei mbaya upungufu wake bei nzuri. kwa maana nyingine demand na supply ndiyo determinant wa ubora wa bei. ninachotaka ujue, jifunze trend za mazo na miezi iliyo bora ndiyo ulime.

mfano mwaka 2014 mwezi wa sita kitunguu cha ruaha mbuyuni bei likuwa elfu 35-50 kwa gunia linalozidi kilo 100 pungufu ya kilo 150, lakini mwaka 2015 mwezi sita gunia hilohilo lilikuwa laki 1.5 hadi 2. ukiwauliza watu hao wawili walio lima misumu hiyo watakujibuje kuhusu kilimo? hivyo fanya kazi ya utafiti kidogo upate maarifa.

Ubarikiwe Mkuu,umetufungua wengi sana.
Tunasikitika kwamba kifufe cha Like kilienda kupiga kura haijarudi,but chukua like ya ki analogue LIKEEEE
 
Kama una material kuja inbox tuingie share mimi nina shamba Bagamoyo very suitable kwa mananasi
 
Binafsi nakushauri uanze na Greenhouse ambayo ni ndogo utakayoanza kulima huku unapunguza ukubwa wa risk za mazao kuharibikia shambani.
Kwa greenhouse unaweza kulima katika majira mbalimbali bila shida yeyote.
Unalima kitaalamu ambapo eneo dogo sana unaweza kuvuna mazao mengi.
Kufanya open field agriculture system huku huna mtaji wa kutosha na huna experience. Naona kama utakuwa dissapointed sana mbele ya safari.
Anza kidogo ukiwa na nia ya kukuza maarifa.
 
For begginers please please please, kilimo cha ujasilia mali ni chakuendea taratibu!! Usione mazao yanastawi mashambani na watu wanasifu fulani kauaga umasikini kwa kilimo ukaondokea papara utajuta! Katika kilimo unashughurika na vitu vikubwa vingi, kulijua soko, kujua mbinu za ustawishaji zao na kujua jinsi ya kutumia vibarua.

Tumia muda wa kutosha kwanza kujifunza soko linataka nn, lini, utauzia wapi? Nenda sokoni unakotarajia kuuza, huko ndiyo utapata taarifa zote za mazao yanayolipa na bei zinavyobadilika kwa mwaka mzima ili ujue miezi ya kupanda, utachagua mazao machache yanayositawi kwenye eneo unalotaka kuzalisha. Hapo hapo sokoni ujifunze aina za zao ulilochagua (varieties) zinazopendwa na wateja, ujue ubora unaohitajia, ujue ufungashaji wake na mfumo wa ununuzi unavyokuwa na ikibidi upate na namba za simu kadhaa za wanunuzi hapo hapo sokoni ili uweze kuwa na mawasiliano nao. hii itakusadia kuendelea kuulizia taarifa mbalimbali ambazo ulisahau kuulizia au zitakazojitokeza.

Baada ya hapo ukirudi kwenye eneo lako la uzalishaji chonde chonde tembelea wakulima waliopo eneo husika wanaolima mazao ulilovutiwa nayo sokoni ili uweze kuamua ulime yapi? hao wakulima watakueleza changamoto na faida ya zao wanalolima. Fanya urafiki nao upate mahari pa kujifunzia. Lima eneo dogo kwanza upate ujuzi wa kilimo cha zao husiika na changamoto za uuzaji sokoni. Upende usipende unahitaji uelimike kwanza katika suala la uuzaji sokoni, timing na mbinu za uzalishaji shambani. Ukijiridhisha kwa hayo hapo sasa waweza kuongeza spidi zaidi kuziwekeza milioni 5 zako.

Kamwe usithubutu kuingia kwa nguvu kubwa kwenye jambo usilolijua undani wake, anza kidogo kidogo ili ujifunze kwa gharama ndogo!! Misimu ya kwanza iwe kama ni darasa kwako. Lazima uelewe kuwa kila utakapobadili zao jipya unaingia kwenye shule nyingine napo anza kidogo maana mazao tofauti yanachangamoto na mbinu tofauti.

Nadhani na mm nimekuongezea pa kuanzia Mkuu !!
 
What is your Passion? Kama huna passion ya haya mambo ni better ukaachana nayo kabisa, Usiingie kwenye kilimo au biashara kwa sababu tu, Jamaa zako wanafanya hivyo, jirani zako au kwa sababu ya shiniko, Expectation ni tofauti na reality,

Kilimo kinahitaji kwanza u fall in love kwenye hicho kilimo, lazima au ufufaji,usifanye kilimo kwa kupiga ramli, usibashili au usifanye kilimom kama upatu kwamba watakacho nishauri watu wengi ndo nitakifanya hicho.

Usilime wala kufuga kwa sababu ya kusikia kwenye redio au kwanye TV, Fanya utafiti wako wewe mwenyewe, angalia unacho penda wewe, angalia soko linataka nini, fanya utafiti wako wewe mwenyewe na si kwa story za mtaani au kusmuliwa.

Miwsho: ukisha maliza kufanya tafiti basi anza na anza kwa sababu umeona kuna tatizo kwenye jamii achana na mawazo ya kwenda kutafuta faida huko kwenye kilimo amke ukienda na hayo mawazo hakika unaweza ukaishia kujinyonga.

Mafanikio itakuwa ni matokea ya kazi yako na si vinginevyo
 
Nikushauri,

Ili uwe mkulima bora.

hakikisha una muda wa kutosha wa kukaa shambani, uwe tiyari kuhama kwenye nyumba yako nzuri na kukaa huko shama jua mvua, pia upate rafiki mtaalamu atakaye kusaidia kutatua changamoto za shamba za kiutaalamu haswa kwenye mimea ya mbogamboga.

Kwa ujumla, nashauri uanze na kitu kama matikiti au kitungu au nyanya, yote ni mazao ya muda mfupi yakidumu miezi mitatu kuanza kutoa matunda, na mwezi moja kitaluni( 3+1=4), pia uliza zao gani ni zuri mahali gani, sio kila zao linafaa kila mahali.

vibarua ni changamoto, watu wasehemu zingine ni wavivu, hivyo ni vyema ukauliza wapi utapata vijana wachapa kazi, na wana hitaji usimamizi mwanzoni wanakuwa hawajua application za dawa na mbolea.

Uwe na mtaji wa kutosha kumuda madawa,mbolea na mambo ya umwagiliaji na kuwalipa vibarua wako. Jifunze kujua risk za kila zao kabla hujapanda, jifunze magojwa yake na ni vizuri kujua dawa zake ili kurahisha wakati wa uhitaji.

Usisikilize sana kuwa zao fulani linalipa sana, wakati mwingine sio kweli, ukweli ni kuwa uwingi wa mazao sokoni kwa kipindi fulani bei mbaya upungufu wake bei nzuri. kwa maana nyingine demand na supply ndiyo determinant wa ubora wa bei. ninachotaka ujue, jifunze trend za mazo na miezi iliyo bora ndiyo ulime.

mfano mwaka 2014 mwezi wa sita kitunguu cha ruaha mbuyuni bei likuwa elfu 35-50 kwa gunia linalozidi kilo 100 pungufu ya kilo 150, lakini mwaka 2015 mwezi sita gunia hilohilo lilikuwa laki 1.5 hadi 2. ukiwauliza watu hao wawili walio lima misumu hiyo watakujibuje kuhusu kilimo? hivyo fanya kazi ya utafiti kidogo upate maarifa.
wise
 
unawazo zuri sana la kuingia kwenye kilimo, kilimo kitakachokutoa haraka sana ni kilimo cha mboga mboga kama nyanya, vitunguu, karoti, na pilipili hoho, mazao haya yanawateja wengi sana na yananunurika na makundi yote namaansha kuwa walio nacho na wasionacho, mimi nina diploma ya kilimo tuwasiliane kwenye namba 0769192358
Vizur mkuu, naomba tuongee ABC za kilimo zao la mpunga

Sent using Jamii Forums mobile app
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom