Nataka kujifunza Kisambaa

Aisee!!
Kuna siku tulifukuza mwizi akaingia nyumba ya wasambaa..
Basi tukawa tunapiga kelele kwa nje Mtoe!!Mtoe!! Na wao huko ndani tunasikia aisee!! Mtoe!!Mtoe aisee!!
Hadi tunakuja kushtuka wasambaa washaua mwizi kimya kimya huko ndani..
Kumbe MTOE kwa kisambaa PIGA..
duu!! Lugha hizi..!!
 
Habari ndugu zangu. Nina hamu sana ya kufahamu lugha ya majirani zangu wasambaa. Ni kipaumbele kwangu kwa kweli likija suala la kujua lugha mbalimbali tofauti. Kuna mtu anaweza kunipa mbinu inayoweza kunifanya nijifunze lugha hii kwa urahisi, mfano vitabu...

Mkuu mi_mdau , nani aliyekufundisha Kiswahili? -- Hakuna. Ulijifunza mwenyewe.

Njia bora kuliko zote ya kujifunza lugha, na kimsingi, elimu yoyote: ni kujifundisha mwenyewe. Ukipata menta (stelingi wa kukusaidia) inaharakisha zaidi muda wa wewe kujifunza. Mfano: Soma / Sikilizia Biblia ya Kishambalai; linganisha na ya Kiswahili.

Angalia video za laoshu505000 kwa hamasa na mbinu za kujifunza lugha kwa haraka.

Angalia na hii hapa chini video ya maisha ya Yesu -- Kwa Kisambaa!

 
IMG-20201012-WA0170.jpg
 
Back
Top Bottom