Nataka kujaza body nitumie powder ipo inanifaa

Bei gan hii
Bei hiyo ni bila usafiri na ushuru..na ni bei za jumla
Screenshot_20210515-195138.jpg
Screenshot_20210515-195054.jpg
 
Habari za jion wakuu nataka kuongeza uzito kidogo na mwili maana ni mwembamba sana tena upande wa mikono nina kilo 65 msaada wenu supploment ipi nzuri kwa kuongeza body maana kama msosi napiga sana lakini wapi

Msaada wenu hapo wakuu
Me sikushauri utumie ayo mavitu yote,sijui poda, Creatine, au whey protein, me wakati nafanya mazoezi nilikuwa natumia ayo, ila yalikuja kuniletea madhala kwenye figo, nilipata Kidney stone (mawe kwenye figo,

Kuna kitu kilizidi , kikatengeneza vijimawe kwenye figo, wataalamu wanajua,

Nilikuwa na body ya ukweli, na nguvu Kama zote, skwati uzito nilikuwa na sukuma hadi kg 160 , triceps nilikuwa napiga weight ya kg 40 na biceps alkadhalika, kwenye dumbbell uko ni hatari,

nakushauri kula sana mboga mboga, na matunda ,maziwa, maji kwa wingi, na chai ya tangawizi, na matango tafuna na maganda yake, na matunda ya apples, halafu jitaid mara moja moja uwe unapata usingizi wakutosha mchana,
 
Una 65kg unalalamika. Mimi nina 58 maybe sasa 59 na nimetulia kabisa. Gym nililipia nikaenda wiki moja, nikalipia tena nikaenda wiki moja. Kula ni mlo mmoja daily kwa miaka minne sasa, nikila mchana usiku siisi njaa hivo inabidi nile usiku zaidi. Kuongeza uzito kwa kula na mazoezi nimeshindwa ngoja nisome hizi supplements.
Mzee unajitesa bure yani hela utafte kwa shida alafu kula ujibane mwishowe uwe na vidonda vya tumbo et kisa unatengeneza body mwajuma akusifie?

Ni kitu ambacho hakiwezekani lazima jasho langu nililipie kwa kupiga msosi wa maana, ata mwili uwe kama wa ngo'mbe ata sijali mana imeandikwa mbiguni tutapewa mwili mpya
 
Habari za jion wakuu nataka kuongeza uzito kidogo na mwili maana ni mwembamba sana tena upande wa mikono nina kilo 65 msaada wenu supploment ipi nzuri kwa kuongeza body maana kama msosi napiga sana lakini wapi

Msaada wenu hapo wakuu
Wenzako wanahaha kupunguza uzito wewe unataka kuongeza? Duuh!
 
Mbona easy ssna

Nilikuwa na 65 hivi saivi ninagonga 82 hivi


Nakunywa Sana supu na chapati yaani mfululizo

Ugali dagaa,wali nyama na samaki na mbogamboga .

Mazoezi yangu push ups na kukimbia .

Nimenenepa Sana Hadi najishtukia

Sent from my TECNO P703 using JamiiForums mobile app
 
Habari za jion wakuu nataka kuongeza uzito kidogo na mwili maana ni mwembamba sana tena upande wa mikono nina kilo 65 msaada wenu supploment ipi nzuri kwa kuongeza body maana kama msosi napiga sana lakini wapi

Msaada wenu hapo wakuu
"Unene haujawahi kumpendeza mtu yeyote" alisikika kijana mmoja.
 
Mzee unajitesa bure yani hela utafte kwa shida alafu kula ujibane mwishowe uwe na vidonda vya tumbo et kisa unatengeneza body mwajuma akusifie?

Ni kitu ambacho hakiwezekani lazima jasho langu nililipie kwa kupiga msosi wa maana, ata mwili uwe kama wa ngo'mbe ata sijali mana imeandikwa mbiguni tutapewa mwili mpya
Sili kisa natengeneza body, kwanza nina uzito mdogo sana BMI yangu nadhani inapungua moja kuwa wastani hivo mara nyingi huwa nachezea kuwa underweight. Ni kwamba sina uwezo wa kula milo mitatu au miwili kwa siku. Ilinishinda hata nikilazimisha
 
Duh, wengine wanatamani kuongezeka na wengine tunatamani kupungua.
 
Back
Top Bottom