Elections 2010 Nataka kugombea urais wa tz 2010

Exaud J. Makyao

JF-Expert Member
Nov 30, 2008
1,518
22
Wana JF,
Nataka kugombea Urais wa Tanzania bara mwaka 2010.
Nipeni orodha ya mbinu za kushinda. 1, 2 , 3, ............n.k.
 
Kama unataka kugombea Urais,kwanza,lazima uwe na original thinking. Thinking yako lazima iwe unique.
Pia ni lazima uwe na speech writer. Speech writer kazi yake ni kuyapa mabawa mawazo yako,kuyapa magurudumu mawazo yako. Kama ukitaka kusema jambo fulani,na unadhani Winston Churchill alisema jambo kama hilo,ni kazi ya speech writer kwenda kufanya utafiti.
Lazima uwe mcha Mungu,uwe spiritual,kwa sababu ukiwa na spiritual knowledge,hii itakuwa ni ushahidi kwamba Mungu anataka kukupa political power.
Lazima pia uwe na fedha nyingi. Kama unafahamiana na Gavana wa Benki Kuu,hiyo itasaidia.
Lazima uwe mkweli,lazima uongee ukweli,lazima ufahamu tofauti kati ya ukweli na uongo.
Lazima uwe serious,uwe na imani kwamba utashinda. Usifanye mambo kupoteza muda wako na muda wa watu wengine,na kupoteza muda wa Taifa.
Nadhani haya nilyosema yatakusaidia. Ihope to you in the State House in Nov. 2010.
 
Ha ha ha Muheshimiwa Exaud Makyao, kula zoezi la kujog kwenye ubenge kwanza, to get the feel of it!
 
President Exaud Makyao of Tanzania, your policies aside,whatever they may be, the name just doesn't sound presidential... sue me. No offense meant but it's hard for me to take anyone called exaud seriously. I'm assuming that's your real name
 
Mengine pembeni...lazima uwe mwanaCCM halisi.

Kazi kweli kweli. We need change!!!!!!!!! Sisi.M Sisi.M tumechoka binafsi antaka rais yeyote hata akiwa niwampito yule toka chama kingine sio Sisi.M from there tutarekebisha na kuboresha mambo hata Sisi.M wakirudi tena baadae watakuwa makini zaidi. Hii hali ya sasa inawapa kiburi mpaka wanasubutu kusma wapinzani wasahau kuingia ikuru utadhani wao ndio wapiga kura.
 
Kazi kweli kweli. We need change!!!!!!!!! Sisi.M Sisi.M tumechoka binafsi antaka rais yeyote hata akiwa niwampito yule toka chama kingine sio Sisi.M from there tutarekebisha na kuboresha mambo hata Sisi.M wakirudi tena baadae watakuwa makini zaidi. Hii hali ya sasa inawapa kiburi mpaka wanasubutu kusma wapinzani wasahau kuingia ikuru utadhani wao ndio wapiga kura.

Give me some options.
Chama gani mbadala kina mwelekeo wa kuingia ikulu 2010?
Exaud kashajitoa kwa kutotaja chama chake so we assume ni mgombea binafsi...out of the question!
 
Lazima uwe fisadi na umezungukwa na marafiki wa kifisadi fisadi vile.
 
Wana JF,
Nataka kugombea Urais wa Tanzania bara mwaka 2010.
Nipeni orodha ya mbinu za kushinda. 1, 2 , 3, ............n.k.

Exaud,

Kwa nini unataka kwenda ikulu? Nini kinakuvutia (motivation)?

Kwa nini Tanzania Bara na si Tanzania?(au ulimi/vidole vimeteleza:)?). Kama ni Tanzania Bara nadhani katiba tuliyonayo kwa sasa haitoi hiyo nafasi.

Kama ni Tanzania kwa ujumla, basi ni wazo zuri lakini naona umechelewa kuanza. Kugombea Urais,kwa maoni yangu, unahitaji maandalizi ya si chini ya miaka mitano! 2010 ni 'kesho' tu!. Kutokana na muda, ili umshinde JK, utahitaji nzuvu za ziada. Pamoja na mabo mengine;

-Ni lazima ufahamike vizuri kwa watanzania (hili linahitaji muda na rasilimali)
-Ni lazima uifahamu vizuri Tanzania na watanzania (SWOT analysis inaweza kukusaidia!).

Umesha-recruit campaign manager?
 
Hizi ndizo njia sahihi:
1. Hakikisha unakuwa na waganga(sangoma) kila mkoa. Mbinu rahisi ni kushiriki kikamilifu katika zoezi jipya la usajili wa waganga kwa kufanya ushikaji na waliopewa dhamana hiyo ili uweze kupenyeza wa kwako.
2. Anza kuangalia muonekano wako, vaa vizuri, chekacheka hata bila sababu.
3. Jiweke karibu na mwalimu, pitapita msasani kumsalimia mama , tafuta hata picha za babu yako alizopiga na mwalimu pamba sebule yako. Ukiweza kutengeneza suti hata mbili kama za mwalimu na uzivae kila kwenye public appearance.
4. kama una mke (jina lako lina suggest wewe ni mwanaume) mwambie aanze kuvaa mabazee ni vilemba vikubwaaa.
5. kamwe usithibutu kutangaza mapenzi yako kwa timu yeyote iwe simba au yanga(ficha rohoni)
6. Jijengee utaratibu wa kuhudhuria majumba ya ibada.

haya yote yamejaribiwa na yamefanya kazi kwa asilimia 100%.
 
Hizi ndizo njia sahihi:
1. Hakikisha unakuwa na waganga(sangoma) kila mkoa. Mbinu rahisi ni kushiriki kikamilifu katika zoezi jipya la usajili wa waganga kwa kufanya ushikaji na waliopewa dhamana hiyo ili uweze kupenyeza wa kwako.
2. Anza kuangalia muonekano wako, vaa vizuri, chekacheka hata bila sababu.
3. Jiweke karibu na mwalimu, pitapita msasani kumsalimia mama , tafuta hata picha za babu yako alizopiga na mwalimu pamba sebule yako. Ukiweza kutengeneza suti hata mbili kama za mwalimu na uzivae kila kwenye public appearance.
4. kama una mke (jina lako lina suggest wewe ni mwanaume) mwambie aanze kuvaa mabazee na vilemba vikubwaaa.
5. kamwe usithubutu kutangaza mapenzi yako kwa timu yeyote iwe simba au yanga(ficha rohoni)
6. Jijengee utaratibu wa kuhudhuria majumba ya ibada.

haya yote yamejaribiwa na yamefanya kazi kwa asilimia 100%.
 
Wazo zuri, lakini urais ni wa Tanzania na siyo Tanzania Bara, na hujaeleza unataka kugombea kupitia chama gani. Hata hivyo uanze kujifunza kuwadanganya wananchi kwa sababu kazi ya siasa imetawaliwa na uongo kuliko ukweli, kama utakuwa mkweli zaidi basi ujuwe hautofika mbali, watakubwaga mapema na kukutoa nje ya mchakato wao.
 
Ushauri wangu ni wa aina mbili za maraisi, sijui wewe unataka kuwa yupi.
1. Rais wanayemtaka:
*Uwe ndani ya mtandao
*Uzungukwe na wapambe
*Uwe na fedha za kutosha, kama huna basi chagua wapambe matajiri, unda kitu kinafanana na kakiti, halafu mshike vizuri gavana wa mapesa yetu.
*Uwezo wako wa kuchekacheka kinafiki lazima uwe juu sana
*Usikubali wapambe wako waadhirike
*Nunua vyombo vya habari vinavyoheshimika vikupambe
*Ita wizi, ufisadi and you name it, ajali ya kisiasani
*Acha wapambe wako wakuelekeze nini cha kufanya, wewe kula nchi
*Amini kwamba maendeleo yanaletwa kwa fedha za misaada na kwa hiyo lazima ukiwa Rais usafiri kuomba sana
*Hakikisha watz wanaendelea kuwa maskini ili gharama ya kuwahonga isipande sana.
* na mabaya mengine mengi

Rais tunayemtaka
*Visionary
*Someone with the right agenda
*Transparent and tells the truth no matter wht
*Cares for the development of all in this country
*Someone who believes in accountability and good governance
*Someone who can think beyond the borders of the party he/she is in
*Anayeamini kuwa kiongozi wa nchi ni wajibu sio tu sifa
*Mtu msafi, hana chembe ya ufisadi, haamini ktk ufisadi
*Mwenye akili timamu, independent thinking as well
hapa yapo mengi wanajamii wataongezea

Unataka kuwa Rais wao au wetu?
 
Ni wazo zuri kutaka kuwaongoza watanzania.Nakushauri uanze na ubunge ili upate uzoefu na kufahamika.Pia tafuta chama kwani hadi sasa mgombea binafsi haijakubalika.
 
President Exaud Makyao of Tanzania, your policies aside,whatever they may be, the name just doesn't sound presidential... sue me. No offense meant but it's hard for me to take anyone called exaud seriously. I'm assuming that's your real name

Ehe,
Mbona vikwazo kibao?
 
Hizi ndizo njia sahihi:
1. Hakikisha unakuwa na waganga(sangoma) kila mkoa. Mbinu rahisi ni kushiriki kikamilifu katika zoezi jipya la usajili wa waganga kwa kufanya ushikaji na waliopewa dhamana hiyo ili uweze kupenyeza wa kwako.
.

Burn,
Kuwa na waganga(sangoma)?
Waliofanikiwa walilitunza hili?
 
Lazima uwe mbea kama yule anayesema TZ nzima hajaona mahali palipojengwa vizuri kama University of Dodoma! Na pia alisema akiingia madarakani ataleta 'mapinduzi ya kilimo'!
 
Back
Top Bottom