Nataka kufanya biashara ya "Uber" lakini sijui pa kuanzia

sonofobia

JF-Expert Member
Jun 21, 2015
369
2,513
Wakuu nina gari yangu imepaki nataka iniingizie pesa kwa kuifanya uber.

Naomba kwa mwenye ufahamu anifahamishe process yote mpaka gari inaingia barabarani.

Yani kama kuna vibali ni vipi? Kama najisajili naenda wapi kujisajili? Kama ni leseni naenda kuikata wapi?

Pia nilitaka kufahamu kama nitampa dereva kwa siku hesabu uwa ni sh ngapi?

Ni hayo tu ninahitaji kuyafahamu ili nione naanzia wapi.
 
Nenda ofisini kwao kwanza the tafuta dereva muulize unayotaka kujua mengine utaongezea mwenye, kumpata dereva fanya ata ku request atakae kuja ndo uyo uyo muulize.
 
Kwanza badili kadi ya gari kutoka private kwenda commercial, pili lipia bima third part iwe commercial, kingine kalipie Sumatra Sasa Ni latra Bei elf 30 Hadi elf 50 ila Ila unapeleka kopi ya kadi ya commercial. Pia dereva awe na leseni iwe halali na Ina daraja la kuendesha teksi yaani C1, ç2.

Baada ya kuwa na hivyo una download app yao (bolt au Uber) Kisha jisajili na una appload picha ya kadi ya gari, bima, Sumatra, leseni na cheti Cha maadili mema kutoka wizara ya mambo ya ndani Kisha ndani ya siku 2 au 3 unapewa access na kuanza kuingiza kipato.
 
Kwanza badili kadi ya gari kutoka private kwenda commercial, pili lipia bima third part iwe commercial, kingine kalipie Sumatra Sasa Ni latra Bei elf 30 Hadi elf 50 ila Ila unapeleka kopi ya kadi ya commercial. Pia dereva awe na leseni iwe halali na Ina daraja la kuendesha teksi yaani C1, ç2. Baada ya kuwa na hivyo una download app yao (bolt au Uber) Kisha jisajili na una appload picha ya kadi ya gari, bima, Sumatra, leseni na cheti Cha maadili mema kutoka wizara ya mambo ya ndani Kisha ndani ya siku 2 au 3 unapewa access na kuanza kuingiza kipato.
Iv unaweza kuendesha uber uku plate namb yako ikiwa ya njano na si ile nyeupe y biashara.
 
Asante mkuu kwa maelezo yako yenye msaada!

Ila naomba unisaidie kufahamu, bima third part ya commercial ndio inakuwaje? Mimi gari yangu ina bima tayari ambayo ni third part.

Pia dereva akiwa na C plain bado hawezi kuruhusiwa endesha teksi?
Mkuu Sonofobia, bima zimegawanyika sehemu mbili ambazo ni bima kubwa au comprehensive au bima ndogo au third part. Na Kila moja imegawanyika Tena sehem mbili ambazo ni bima kubwa ya binafsi au ya biashara na bima ndogo/third party ya binafsi au ya biashara.

Sasa Kama unabima ndogo ya binafsi inabidi uibadili kuwa third part commercial, Sasa inategemea na kampuni uliyokata hiyo bima, Kuna baadhi ya kampuni unaweza ukaongezea hela kidogo kwenye bima yako ya binafsi wanaita kutop up halaf wanakubadilishia bima yako kuwa ya biashara na Kuna kampuni zingine wanakataa kabisa hivyo itabidi ukate nyingine mpya ya biashara.

Na bila bima ya biashara hawakuruhusu kujiunga nao Uber/bolt.
 
Duh aisee hii naona ishakuwa ngumu! Gharama hizi sitoziweza.

Ila nashukuru sana kwa kunifumbua macho.
Usikate tamaa, wasiliana na kampuni ya bima Kama watakuruhusu u top up na kubadili kadi ya gari kuwa commercial. Hata Kama sio Sasa hata baada ya miez 3 au 6 waweza Anza.
 
Naomba kuuliza , je magari yaliotengezwa zamani mfano yenye namba A yaliyo kwenye hali nzuri yanaweza kusajiliwa bolt?

Pili cheti cha maadili kinachukua muda gani kukipata huko polisi?
 
Wakuu nina gari yangu imepaki nataka iniingizie pesa kwa kuifanya uber.

Naomba kwa mwenye ufahamu anifahamishe process yote mpaka gari inaingia barabarani.

Yani kama kuna vibali ni vipi? Kama najisajili naenda wapi kujisajili? Kama ni leseni naenda kuikata wapi?

Pia nilitaka kufahamu kama nitampa dereva kwa siku hesabu uwa ni sh ngapi?

Ni hayo tu ninahitaji kuyafahamu ili nione naanzia wapi.

Uber na bolt mimi naweza kukufwatilia vibali vyote boss. Tunaweza kwa kutumia account maana kwa sasa cna gari nicheck 0715715385 kwa mawasiliano zaidi.
 
Back
Top Bottom