Nataka kuagiza gari hii, itanigharimu vipi?

Vidude gani tena nawe Fisadi?

Niliviulizia hapa mkuu...

Nshukurusa sana kwa wazee wa kukokotoa, mnatoa mwanga sana. Inabidi TRA wawalipe, maana lazima wana-budget ya kutoa elimu ila sijui inaendaga wapi.

Matumaini yangu yakujikomboa na hii adha yanarudi, ila naomba wakuu mnikosoe. Na pengine hii inaweza kuwasaidia wengine kama mimi.

Nimeona kuna hivi vigari vidogovidogo (Nissan March, Toyota Duet, etc) vya mwaka 2001, vya cc 1,000, nimeona vinauzwa FOB $600 mpaka $800. Hivi vinapunguza kodi sana kwa kuondoa dumping fee na excise duty. Tukichukulia CIF ni $2000, pengine mtu anaweza kutoka maana nikikokotoa fasta napata 3,345,300/= bila kumhonga mtu.

Je, maana yake nikipata pa kukopa hiyo 500,000 nikaongezea kwa vi M3 vyangu naweza nikapata moja ya hivi vidude?

Kwa mfano:
http://www.tradecarview.com/used_car/japan car/nissan/march/820691/
http://www.tradecarview.com/used_car/japan car/toyota/duet/900408/

Sijali kina nini, mi ilimradi kitembee tu na kiweze ku-overtake daladala basi ... tehe tehe.

Naomba mawazo wakuu.

Nimeshaelewa elewa kidogo jinsi mnavyofanya ukokotozi, ila nauliza ulize usije kukuta kuna catch mahali, nije kushikwa pabaya.
 
Niliviulizia hapa mkuu...



Nimeshaelewa elewa kidogo jinsi mnavyofanya ukokotozi, ila nauliza ulize usije kukuta kuna catch mahali, nije kushikwa pabaya.

Sikuona hapo, sasa hapa kijana mambo yanaweza kukuendea vizuri! Kwa mfano hako ka March ka 2001, CC isiyozidi 1,000 utasave sana....maana hakuna excise duty 5%. hakuna uchakavu 20%...wewe unalipa tu VAT 18% na Import duty 25% (total taxes 43%)!

Kwa FOB US$600, ina maana CIF cost ni kama US$ 1,800 hivi...which means pamoja na kodi utalipa US$ 2,655 kwa rate ya 1,350 ni kama Tshs 3,584,250 tu! Gharama ndogondogo zitafikia kama Ths 500,000 (inaweza pungua au kuongezeka) so total cost kitu unacho barabarani ni Tshs 4,084,250 tu mzee!
 
Sikuona hapo, sasa hapa kijana mambo yanaweza kukuendea vizuri! Kwa mfano hako ka March ka 2001, CC isiyozidi 1,000 utasave sana....maana hakuna excise duty 5%. hakuna uchakavu 20%...wewe unalipa tu VAT 18% na Import duty 25% (total taxes 43%)!

Kwa FOB US$600, ina maana CIF cost ni kama US$ 1,800 hivi...which means pamoja na kodi utalipa US$ 2,655 kwa rate ya 1,350 ni kama Tshs 3,584,250 tu! Gharama ndogondogo zitafikia kama Ths 500,000 (inaweza pungua au kuongezeka) so total cost kitu unacho barabarani ni Tshs 4,084,250 tu mzee!

Asante sana mkuu. Naona sasa huu ndio mwendo. Hapo inakuwa rahisi kuliko hata Bajaji ... tehe tehe

Kuna swali lingine niliulizwa mkubwa naona hukuliona pia.

Je, gharama baada ya kutoka bandarini nazo zikoje? Yaani registration, leseni, etc.
 
Asante sana mkuu. Naona sasa huu ndio mwendo. Hapo inakuwa rahisi kuliko hata Bajaji ... tehe tehe

Kuna swali lingine niliulizwa mkubwa naona hukuliona pia.

Je, gharama baada ya kutoka bandarini nazo zikoje? Yaani registration, leseni, etc.

Hivyo vyote nimekadiria vinaweza fikia Tshs 500,000 (Hela ya agent kama 150,000(bargainable), insurance 3rd party unaweza lipia Ths 50,000 max 100,000, Registration Tshs 120,000, kibao cha namba ya gari Tshs 36,000, Road licence Tshs 50,000 (kwa hicho kigari), gharama za bandarini pale zinaweza kuwa Tshs 100,000 (zaidi au inaweza pungua depending on ushapu wa agent wako)

Hope hapa tupo sawa sasa!

But kama wewe ni mwalimu au mke wako mwalimu au mama or baba ni mwalim au mfanyakazi wa serikalini tena kuna exepmtion ya VAT mzee so cost itashuka zaidi tena!
 
Waungwana nataka kuagiza hii Suzuki ya 1994:
http://www.tradecarview.com/used_car/japan car/suzuki/jimny/814099/

Year / Month: 1994
Odometer: 18,000 km
Displacement: 650 cc

Bei yake ni $980.

Je, kuna mtu anaweza kuniagizia? Na nitamlipa kiasi gani jumla kwa fedha za ki kwetu?

ndugu kuwa muangalifu sana na gari za mitandaoni, hasa hiyo kampuni ya Sakina uliyoiona hiyo pajero ya dollar 33, mie nilikuwa nataka mark 2 yao, nimecontact nao majibu walionipa yamenishitua sababu nimeshawai kuagiza magari japan kwa sana,kidogo najuwa utaratibu unakuwa vipi.
mimi niliwaomba wanipe CIF ya gari mpaka dar majibu yalikuja hivi:

Hi,

We will use Index Cargo Freight Company ( www.Intex-Cargo.110mb.com ) , which is an international shipping company (they deliver the car to you and assure your money).the car will shipp from England . In England this shipping company is very popular and familiar. Index Cargo Freight.company is a shipping company, which offers the possibility to sale cars over the Internet safe . I will pay for all charges (delivery taxes) to your location. As soon as i will begin the delivery of the car ,Index Cargo Freight Company will email you an invoice with shipping info (delivery status, delivery date, time of arrival)and payment instructions . After receipt of all shipping info , You need to transfer the money (50% from price )to Index Cargo Freight Company (your money will be keeped and protected by them until you will receive and inspect the car). After the payment is confirmed the delivery is begun and within 3 days you will receive the car delivered to your house.
Return Policy: After you receive your car, you have 10 working days to test the car and all car papers. If you have any problems with the car, you must contact Index Cargo Freight Company for reimbursement and they bring you your money back (50% )and the car will be shipped back to me on my cost.This agreement is the safest thing I can offer you.
Now, if you are interested to buy the car, I wait for your e-mail with the following information to start the shipping process:

Name :...................... ............................
Surname :....................
Street and house number :................
City :.............................. ........................
Zip :............................. ..........................
Country :......................... .....................

p.s

usifikiri CIF yako ya kweli ndiyo itapita pale TRA, wale jamaa ni wa ajabu sana, huwa wanakuwa na mibei yao waitakayo!
 
hivi kuna mtu amejaribu kununua yanayouzwa mnada bandarini? Ambayo waagizaji wameshindwa kulipia ushuru? anfikiri mengine yanaweza kuwa bei poa!
 
hivi kuna mtu amejaribu kununua yanayouzwa mnada bandarini? Ambayo waagizaji wameshindwa kulipia ushuru? anfikiri mengine yanaweza kuwa bei poa!

hayo wanapeana wenyewe ndugu, mtu wa nje kuonga mpaka kulipata longolongo jingi
 
Aaahaaaaa...mzee wa ''DOCEBIT VOS OMNIA'' ...Huja toa updates...ile tour yako kule kunani iliendaji mzee....vipi ulienjoy or ulipata disappointments?

Tupo mzee, sijui kabaki nani pale Pugu, maana naona hata kanisa kama limechoka hivi! HIvi yule mze wa shamba bado yupo hai?

Tanga nilifaidi sana nilikuwa pale regal; nice place tulikuwa "tunanua tembo kwa ubua"
 
Wazee naomba tena msaada kwenye hili.

Nimesikia kwamba eti ukileta gari ambalo ni jipya sana (yaani baada y 2001 kwa mfano), TRA wana jinsi yao ya kukadiria CIF na wana-ignore CIF iliyoko kwenye invoice yako.

Je, hii ni kweli?

Na kama ni kweli hayo makadirio yao wanayafanya kwa kutumia criterio zipi? Nimeambiwa wanakuwa na table yenye model za magari na miaka na bei zake.

Sina uhakika kwamba huu ni uzushu au kuna ukweli ndani yake.
 
Wazee naomba tena msaada kwenye hili.

Nimesikia kwamba eti ukileta gari ambalo ni jipya sana (yaani baada y 2001 kwa mfano), TRA wana jinsi yao ya kukadiria CIF na wana-ignore CIF iliyoko kwenye invoice yako.

Je, hii ni kweli?

Na kama ni kweli hayo makadirio yao wanayafanya kwa kutumia criterio zipi? Nimeambiwa wanakuwa na table yenye model za magari na miaka na bei zake.

Sina uhakika kwamba huu ni uzushu au kuna ukweli ndani yake.

Hiyo huwa inatokea kama wanaona kuna dalili za mwagizaji kuwa anataka kucheat on genuine documents na CIF cost ya gari! Lkn kama umewapelekea vielelezo (genuine) vyote vya gari husika, hakuna uplifting ya cost mazee!
 
Hiyo huwa inatokea kama wanaona kuna dalili za mwagizaji kuwa anataka kucheat on genuine documents na CIF cost ya gari! Lkn kama umewapelekea vielelezo (genuine) vyote vya gari husika, hakuna uplifting ya cost mazee!

hivi ni vielelezo gani wanavyoitaji hili wasiuplift?
 
Hivyo vyote nimekadiria vinaweza fikia Tshs 500,000 (Hela ya agent kama 150,000(bargainable), insurance 3rd party unaweza lipia Ths 50,000 max 100,000, Registration Tshs 120,000, kibao cha namba ya gari Tshs 36,000, Road licence Tshs 50,000 (kwa hicho kigari), gharama za bandarini pale zinaweza kuwa Tshs 100,000 (zaidi au inaweza pungua depending on ushapu wa agent wako)

Hope hapa tupo sawa sasa!

But kama wewe ni mwalimu au mke wako mwalimu au mama or baba ni mwalim au mfanyakazi wa serikalini tena kuna exepmtion ya VAT mzee so cost itashuka zaidi tena!

NL sahihisho kidogo rafiki,
Watumishi wa umma wanasamehewa Excice duty (kama gari yako inaanzia cc 2000 na zaidi) and Import duty ila VAT unalipa kama kawaida kwa mujibu wa GN. Na. 520 na 522 za mwaka 1995.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom