Nataka kuachana na UDOM haitaniathiri kwenye mikopo nikitoka advance?

King snr

JF-Expert Member
May 25, 2015
1,165
1,461
Mimi ni mmoja wa tuliofukuzwa UDOM sitaki tena kurudi chuo kile kwani wameshanivuruga kisaikolojia nataka kwenda advance.

Naombeni ushauri nilikuwa napata mkopo pale UDOM hivi nikiondoka mkopo si unaweza ukawa unaendelea kufika chuoni halafu Mimi nisiupate na vipi nikitoka advance kuna uwezekano wa kupata mkopo tena?

Naombeni msaada wakuu
 
Wewe nenda katoe taarifa kwa afisa mikopo chuoni kwako kuwa hautarud chuoni hata ukirudishwa ili awaandikie barua bodi ya mikopo ya kukuondoa

Uspotoa taarifa utaonekana bado unanufaika na mkopo ili Hali haupo chuoni, kitu ambacho kitakuathiri ukija
Kuomba mkopo baada ya kumaliza advance
 
Unaweza kuendelea kufika afu wewe usiupate kivipi?! You mean baada ya kumaliza six na kwenda chuo unaweza usipate tena mkopo; au?!

In addition, kwanini uvurugukiwe? Hayo mambo mbona ya kawaida sana? Don't forget, haupo sekondari anymore! Minyukano kati ya serikali/chuo na wanafunzi ni mambo ya kawaida? Enzi hizo watu walikuwa wakiona paper hizoooo zinakuja na network haisomi signal... unashangaa tu from nowhere watu wanaanzisha unresolved agenda ya miaka 2 iliyopita ili mradi tu!

NOTE: Kwa muda sasa, nimekuwa nikitafuta bila mafanikio course outline ya hiyo Special Diploma program! Naweza kuipata toka kwako; au unaweza kuiweka hapa?!
 
Unaweza kuendelea kufika afu wewe usiupate kivipi?! You mean baada ya kumaliza six na kwenda chuo unaweza usipate tena mkopo; au?!

In addition, kwanini uvurugukiwe? Hayo mambo mbona ya kawaida sana? Don't forget, haupo sekondari anymore! Minyukano kati ya serikali/chuo na wanafunzi ni mambo ya kawaida? Enzi hizo watu walikuwa wakiona paper hizoooo zinakuja na network haisomi signal... unashangaa tu from nowhere watu wanaanzisha unresolved agenda ya miaka 2 iliyopita ili mradi tu!

NOTE: Kwa muda sasa, nimekuwa nikitafuta bila mafanikio course outline ya hiyo Special Diploma program! Naweza kuipata toka kwako; au unaweza kuiweka hapa?!
Nilimaanisha mkopo utakuwa unafika chuoni af Mimi sinufaiki nao sababu nitakuwa advance,, unahitaji course outline general ya special diploma?
 
Wewe nenda katoe taarifa kwa afisa mikopo chuoni kwako kuwa hautarud chuoni hata ukirudishwa ili awaandikie barua bodi ya mikopo ya kukuondoa

Uspotoa taarifa utaonekana bado unanufaika na mkopo ili Hali haupo chuoni, kitu ambacho kitakuathiri ukija
Kuomba mkopo baada ya kumaliza advance
Asante kwa ushauri mkuu
 
Wewe nenda katoe taarifa kwa afisa mikopo chuoni kwako kuwa hautarud chuoni hata ukirudishwa ili awaandikie barua bodi ya mikopo ya kukuondoa

Uspotoa taarifa utaonekana bado unanufaika na mkopo ili Hali haupo chuoni, kitu ambacho kitakuathiri ukija
Kuomba mkopo baada ya kumaliza advance
aende tu advance mana udom hapamuhusu tena na asahau kuwa aliwahi soma udom.kaisikilize tena speech ya baba J
 
Mkopo sitapewa lakini utakuwa unafika chuoni kama kawaida utalipia tution fees ila pesa tu ya meals and accommodation ndo nitaikosa sasa hiyo itakuwa hasara kwangu mkuu
Umeshaambiwa hapo kaka we Andika termination letter ipeleke Udom wao wataipeleka bodi na kukutoa kwenye system simple as that wala usiogope mkopo Uta pata tena
 
Mkuu mkopo utakuwa unaingia kama kawaida mpaka uandike termination letter alafu loan officer wa chuo aipeleke bodi.

Kama utapenda kupata mkopo baada ya kumaliza form six inabidi uwe umeulipia mkopo wote uliotumia ukiwa special diploma vinginevyo hutaweza kuuomba.

Nakushauri,usikate tamaa mapema hvyo! Ulishatumia rasilimali nyingi ikiwepo fedha na muda,tulia uwasikilizie serikali. Kuna kila dalili mtarudishwa. Mambo ya kwenda kupigika tena miaka miwili ni ishu.

Ila kama umedhamiria kabisa kutorudi,nakutakia kila la kheri mbeleni. Advance siyo mchezo kwa combination za P yaani za sayansi haswa zenye Physics..
 
Mkopo sitapewa lakini utakuwa unafika chuoni kama kawaida utalipia tution fees ila pesa tu ya meals and accommodation ndo nitaikosa sasa hiyo itakuwa hasara kwangu mkuu
acha kujidanganya wee dogo.pesa zote hadi ada huwa tunasaini kisha zinaletwa.wewe nenda zako huko advance ukasome na usiende PCM mana itakula kichwa kwa jinsi navyokuona.
 
Mkuuu, kitendo cha kuitwa kilaza ndio kimekuchanganya kiasi hicho? Usife moyo, mapambano ndio kwanza yameanza...
 
mkuu suala la mkopo au ada kupelekwa udom sahau. imeshatoka oda kutoka kwa magufuli kuzuia mikopo yote ya special dip. nenda advance hujachelewa kapige six ukijakutoboa utaomba tena mkopo, ila taratibu za loan board znabak palepale kuwa ulichokitumia udom unatakiwa ukirefund kwa 25% pale loan board ili uje kuendelea kuwa mnufaika ukifanikiwa kupata udahil wa elimu ya juu. nakushauri achana na udom kwa sasa coz tayar mmeshachinjiwa baharini.
 
Tafadhali hebu tupia ulichopata O level kisha tujue ukweli wa Baba Jesca...
 
Mkuu mkopo utakuwa unaingia kama kawaida mpaka uandike termination letter alafu loan officer wa chuo aipeleke bodi.

Kama utapenda kupata mkopo baada ya kumaliza form six inabidi uwe umeulipia mkopo wote uliotumia ukiwa special diploma vinginevyo hutaweza kuuomba.

Nakushauri,usikate tamaa mapema hvyo! Ulishatumia rasilimali nyingi ikiwepo fedha na muda,tulia uwasikilizie serikali. Kuna kila dalili mtarudishwa. Mambo ya kwenda kupigika tena miaka miwili ni ishu.

Ila kama umedhamiria kabisa kutorudi,nakutakia kila la kheri mbeleni. Advance siyo mchezo kwa combination za P yaani za sayansi haswa zenye Physics..
Hapana siyo mkopo wote inapaswa alipe 25% ya tuition fees watu wengine mko kwa kumislead watu basi tu sijui mnajisikiaje kupanikisha mtu alipe yote onesha imeandikwa wapi na sheria ipi kama hujui au una mashaka na kitu kabla ya kuandika uliza kwanza
 
Nilimaanisha mkopo utakuwa unafika chuoni af Mimi sinufaiki nao sababu nitakuwa advance,, unahitaji course outline general ya special diploma?
Kwa staili hiyo lazima mkopo utaendelea kwenda at least kwa semester ya kwanza! Endapo utafikia uamuzi wa kwenda A-Level, basi fuata ushauri wa Victor wa happy hapo juu!

HOWEVER, usimjulishe huyo Afisa Mikopo kwa mdomo bali kwa barua and make sure one copy ya barua inaenda HESLB na nyingine kwenye Head of Department.

Anyway, sifahamu flow mzima ya kitaasisi imekaaje lakini hata ukifanya kama hapo juu, itakuwa okay.

Kuhusu Course Outline, nimekosea... I mean COURSE STRUCTURE ( though sina hakika ikiwa ndivyo mnavyoita wenyewe). Hapa nazungumzia ile ambayo inaorodhesha First Semester mnasoma units zipi, second semester n.k! Nilikuwa naulizia ya Diploma Special Program either Physics & Mathematics or Chemistry & Mathematics ndizo ambazo naweza kuzichambua vizuri.

Lakini ikiwa ni kubwa sana to the point itakupa shida ku-screenshot na ku-post basi unaweza kupotezea... nitatafuta alternative nyingine.
 
Mimi nina swali langu la ukilaza; Hivi watakofukuzwa kabisa bila kupangiwa vyuo vingine, wakifight back wakawa na kazi nzuri watalipa huo mkopo hewa?
 
Back
Top Bottom