Nataka kuacha kazi, niendeshe Ubber. Ushauri.

Ungefunguka zaidi tungekupa ushauri.
Si kazi zote mbaya, kuna kazi mtu huwa huru kuwekeza pengine, zingine zinatoa kipato kikubwa kwa mwajiriwa kiasi kwamba anaweza kujenga nyumba nzuri, kununua hizi Japanese used car na kusomesha.
Ungefunguka ili watu wakushauri.
Wapo walioacha kazi wakafanikiwa zaidi, pia wapo walioacha kazi ili wajiajiri wakaishie kuchanganyikiwa.
 
Habar za Wikiendi.

Mimi ni kati ya wale tuliochoshwa na Ajira. Nimefikiria sana naona bora nianze ubber. Naomba ushauri kwa wazoefu wa ubber.
Unataka kuruka mkojo ukanyage mavi naona kaka yangu wadamu alikuwa na gari mbili uber kazitoa ww wataka endesha haya kila la kheri
 
Inategemea nn kina kukwaza kazini, tatizo la kazi nyingi za kuajiriwa ni za kitumwa na kipato kidogo , mm nakushauri nenda ofisï za ubber utapata maelezo yote.
 
Kuacha kazi(kazi)UBER(part time job)majanga

Tuulize tuliokuwa huko
Uber unakuja na gari lako au la mtu?
Ushawahi endesha Uber
T
Nb.tuliokuwa UBER tunatafuta kazi njoo ili na we're baadae utafute kazi
 
Ndio maana siku zote matajiri watabaki kuwa wachache mno, uber imetajirisha vijana:
1. Anakopeshwa gari bila sent tano kijana anajikunja ndani ya miaka 2 tu gari lake
kupitia Uber CRDB pekee wamekopesha magari 260 bado bank zingine bado mtu mmoja mmoja.
2. Niambie ni wapi utakopeshwa gari ya 12 mln bila sent ? mtaji ni leseni yako tu
3. Ukiona mabank wanafatilia mradi na wako tayari kutoa pesa zao jua hapo kuna ulaji
4. Uber ni FURSA yako wewe" KIJANA"Mchakalikaji/mchapakazi, Discipline ya hakika,
dereva mjuzi/uzoefu ,huna anasa/ulevi wowote, mwenye ndoto na malengo,

. . . . Inaendelea . . . .
 
Ndio maana siku zote matajiri watabaki kuwa wachache mno, uber imetajirisha vijana:
1. Anakopeshwa gari bila sent tano kijana anajikunja ndani ya miaka 2 tu gari lake
kupitia Uber CRDB pekee wamekopesha magari 260 bado bank zingine bado mtu mmoja mmoja.
2. Niambie ni wapi utakopeshwa gari ya 12 mln bila sent ? mtaji ni leseni yako tu
3. Ukiona mabank wanafatilia mradi na wako tayari kutoa pesa zao jua hapo kuna ulaji
4. Uber ni FURSA yako wewe" KIJANA"Mchakalikaji/mchapakazi, Discipline ya hakika,
dereva mjuzi/uzoefu ,huna anasa/ulevi wowote, mwenye ndoto na malengo,

. . . . Inaendelea . . . .

Tuulize tulioko kwe sector za bank we jamaa...magari 250 unaona kama ndo kama yote sio.
Dereva yoyote hata tax hii mikopo anapata kwakua risk ni ndogo gari ipo insured na wewe lazima kwanza tukucheki mda ambao umekua kwe biashara sio mtu unaanza leo tukupe gari.we utakua ni wale madalali wa uber wanaotafuta madereva..kwanini jamaa asiendelee na kazi akamweka mtu uzuri wa uber haidanganyi kila mteja anayepata nawe waweza ona so mnagawana pasu kwa pasu na atakua na vipato viwili..na sasa serikali inavyowabana hawa madereva sijui ka atapata kipato cha kuridhisha
 
  • Thanks
Reactions: Auz
Habar za Wikiendi.

Mimi ni kati ya wale tuliochoshwa na Ajira. Nimefikiria sana naona bora nianze ubber. Naomba ushauri kwa wazoefu wa ubber.

anza kwanza kuendesha ubber ukiwa hauendi kazini..kwa mfano weekend (kama ratiba inakuruhusu)...ili ujue changamoto zake, alafu baadae ndio ufanye hayo maamuzi
 
Tuulize tulioko kwe sector za bank we jamaa...magari 250 unaona kama ndo kama yote sio.
Dereva yoyote hata tax hii mikopo anapata kwakua risk ni ndogo gari ipo insured na wewe lazima kwanza tukucheki mda ambao umekua kwe biashara sio mtu unaanza leo tukupe gari.we utakua ni wale madalali wa uber wanaotafuta madereva..kwanini jamaa asiendelee na kazi akamweka mtu uzuri wa uber haidanganyi kila mteja anayepata nawe waweza ona so mnagawana pasu kwa pasu na atakua na vipato viwili..na sasa serikali inavyowabana hawa madereva sijui ka atapata kipato cha kuridhisha
WaTZ hawakosi majibu, haya sasa mm dalali ? ? , Hongera sana mkuu, Amina ! !
 
  • Thanks
Reactions: y-n

Similar Discussions

Back
Top Bottom