Natafuta Zilipendwa

Rev. Kishoka

JF-Expert Member
Mar 7, 2006
4,526
1,529
Jamani mwenye Zilipendwa origino kati ya miaka 1975-1995 naomba awasiliane nami kwa PM.

Hususan natafuta Nuta.Juwata/Ottu, Mlimani Park, Vijana Jazz, Marquis, Mzee Makassy, OSS, Kyauri Voice, King Kiki, Biashara Jazz, Kimulimuli, Mwenge Jazz, Dar Jazz, Bima Jazz, Tshimanga Assosa na Mambo Bado, Nk.
 
.... Zilipendwa origino -kati ya miaka 1975-1995 naomba awasiliane nami kwa PM...

Ah!, Rev Kishoka nyimbo za 1975 ni zilipendwa, si nyimb za juzi tu hizo??? kwi!kwi!kwi!. Miye nilidhani utauliza za 1950 au 1960 ambazo hata miye nazitafuta!!!

On serous note,
Kwa yeyote ambaye anazo hata miye nitashukuru kama atanitumia PM au choveki@yahoo.co.uk
 
Jamani mwenye Zilipendwa origino kati ya miaka 1975-1995 naomba awasiliane nami kwa PM.

Hususan natafuta Nuta.Juwata/Ottu, Mlimani Park, Vijana Jazz, Marquis, Mzee Makassy, OSS, Kyauri Voice, King Kiki, Biashara Jazz, Kimulimuli, Mwenge Jazz, Dar Jazz, Bima Jazz, Tshimanga Assosa na Mambo Bado, Nk.


mchUngaji wa kondooo wa BWANA....
heee umefikwa na nini mwenzetu,unataka niymbo???mie nilifikiria wachungaji hawasikilizaji nyimbo.heshima yako,mie ninazo za taarab kama za NADI IKHWAN SWAFAA na CULTURE MUSICAL CLUB jee zitakufaa??
 
REV WEWE UKO TANZANIA DAR ES SALAAM AU ?

KAMA UKO DAR ES SALAAM NITAFUTE NAWEZA KUKUSAIDIA KWA ASILIMIA KUBWA SANA

PIA UNAWEZA KUTEMBELEA www.shy.phpbb24.com ANGALIA SEHEMU YA ZILIPENDWA UTAONA MASHAHIRI YA NYIMBO HIZO
 
mchUngaji wa kondooo wa BWANA....
heee umefikwa na nini mwenzetu,unataka niymbo???mie nilifikiria wachungaji hawasikilizaji nyimbo.heshima yako,mie ninazo za taarab kama za NADI IKHWAN SWAFAA na CULTURE MUSICAL CLUB jee zitakufaa??

Mchungaji mwema huzijua nyasi zote zilizoko malishoni, zifaazo na zisizofaa, zenye taka na zilizo safi, zilizo na sumu na zilizo salama, ili aweze kuwaelekeza kondoo katika malisho mema.
Mchungaji,
Nadhani www.bongo5.com wanazo zilipendwa, watembelee, click penye neno music, telemka chini utaona.
 
Huyu atakuwa anataka Zake mwenyewe kwa ajili yake Softcopy sio zile za mtandao mimi nimeelewa hivyo sijui wenzangu
 
Kuna wakati shy ulituwekea nyimbo kibao....ile email bado ipo?......je umei-update?
 
mchUngaji wa kondooo wa BWANA....
heee umefikwa na nini mwenzetu,unataka niymbo???mie nilifikiria wachungaji hawasikilizaji nyimbo.heshima yako,mie ninazo za taarab kama za NADI IKHWAN SWAFAA na CULTURE MUSICAL CLUB jee zitakufaa??

Mfalme Daudi alipiga zumari na kucheza muziki, alokwambia kusikiliza mziki ni dhambi nani?

Je unazo za Bi. Shakila na yule Mzee alikuwa ana madongo makali? je wakumbuka bunduki risasi hewa? pochi?

Kama unazo naomba nichomee, halafu tuwasiliane jinsi ya kutumiana!
 
Mfalme Daudi alipiga zumari na kucheza muziki, alokwambia kusikiliza mziki ni dhambi nani?

Je unazo za Bi. Shakila na yule Mzee alikuwa ana madongo makali? je wakumbuka bunduki risasi hewa? pochi?

Kama unazo naomba nichomee, halafu tuwasiliane jinsi ya kutumiana!


mchungaji.....
wakati ninapoongelea zilipendwa za tarab za znz,akina shakila na wengine walikuwa bado wanacheza TANCUT ALMASI,MAQUIZ,VIJANA JAZZ n.k,kwa maana hiyo mie hao nimeanza kuwajua majuzi tu.lakini kuna nina vigongo vya TAARAB ASILIA kama za MOHD ILYASI,FAUZIA,RUKIYA RAMADHAN, n.k hizo ndio nyimbo zetu yakhe sio za siku hizi akina khadija kopa na wezake TAARAB DANSA.
kwa hiyo mchungaji kama wataka hizo naweza kukuchomea na kukufikishia kunakohusika.
endelea kuwachunga KONDOO WA BWANA.muombee sana ANDREW CHENGE mola amsamehe madhambi yake.amin.
 
mchungaji.....
wakati ninapoongelea zilipendwa za tarab za znz,akina shakila na wengine walikuwa bado wanacheza TANCUT ALMASI,MAQUIZ,VIJANA JAZZ n.k,kwa maana hiyo mie hao nimeanza kuwajua majuzi tu.lakini kuna nina vigongo vya TAARAB ASILIA kama za MOHD ILYASI,FAUZIA,RUKIYA RAMADHAN, n.k hizo ndio nyimbo zetu yakhe sio za siku hizi akina khadija kopa na wezake TAARAB DANSA.
kwa hiyo mchungaji kama wataka hizo naweza kukuchomea na kukufikishia kunakohusika.
endelea kuwachunga KONDOO WA BWANA.muombee sana ANDREW CHENGE mola amsamehe madhambi yake.amin.

Mhandisi,

Nimekuuliza kuhusu Bi. Shakila si kuhusu Khadija Kopa bwana. Ama humfahamu Bi. Shakila weye...!

Je Issa Matona unaye? na yule bibie malkia wa Afrika Kulthum wa Misri wamfahamu?
 
Mhandisi,

Nimekuuliza kuhusu Bi. Shakila si kuhusu Khadija Kopa bwana. Ama humfahamu Bi. Shakila weye...!

Je Issa Matona unaye? na yule bibie malkia wa Afrika Kulthum wa Misri wamfahamu?

mchungaji
yes za omoo kolthoom ninazo lkn sio nyingi kama 4 hivi,kuna moja hiyo unaijua inaitwa ZALAMNA EL-HUUB,ahhh weee acha tu.kwani mchungaji kiarabu kinapanda hapo?
za shakila na bw matona sina mkuu.
 

Similar Discussions

1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom