Natafuta wanunuzi wa kuni kwa jumla

ROKY

Senior Member
May 4, 2011
182
70
Hi wana JF wote,
Natafuta watu wa kununua kuni za jumla.
Nina shamba jipya nalisafisha, hivyo kuna miti mingi sana kwa ajili ya kuni.
Eneo lilipo shamba hilo ni mkoa wa Pwani, umbali wa kilometa 100 toka DSM.
Bei ya kuni ni maelewano tu na wanunuzi.
Wana JF naomba mnipe contacts za wanunuzi watakaonunua kuni hizo kwa jumla.

Thanks in advance.
 
Jaribu pia kuwasiliana na uongozi wa canteens za vyuo mf. Ardhi au UD. Hawa pia ni watumiaji wazuri wa kuni, suredly you'll get a delicious market.
 
hivi huu uharibufu wa mazingira bila aibu????/

Huu sio uharibifu wa mazingira. Kinachofanyika hapa ni matumizi ya miti inayoondolewa kwenye shamba ili kupisha kilimo.
Kama nilivyosema kwenye post yangu, "ninasafisha shamba jipya", na katika usafishaji wa shamba jipya, ambalo kwa sasa ni pori, lazima kuna miti itakatwa ili kupata eneo la kilimo. Sasa miti kama hiyo ndio naitafutia soko ili itumike kama kuni badala ya kuichoma moto na kuipoteza bure.
Hapa hakuna uharibifu wa mazingira.

Wana JF naomba mwenye contacts za wanunuzi wa miti kwa ajili ya kuni anipe.
 
Back
Top Bottom