Kishaju
Senior Member
- Feb 23, 2008
- 106
- 62
Ndugu zangu naomba mnisaidie kama mnawajua vijana wachapa kazi wanaoweza kufanya kazi ya palizi kwenye shamba langu la nanasi ambalo lipo Bagamoyo, Fukayosi. Nahitaji kufanya palizi kabla ya mvua kuanza mwezi wa tatu.
Eka ambazo nimepanda hadi sasa ni 12 na tatizo kubwa linalonikabili kwa sasa ni nguvu kazi. Vijana wengi ambao wananifanyia kazi wana tatizo la ulevi (sio beer za TBL ni mataptap), uzembe, wizi na udanganyifu . Wakipata pesa mpaka waimalize yote ndo warudi kazini na ukiwapa "advance" kabla ya kazi ndo inakula kwangu.
Bila shaka wale mnaojishghulisha na kilimo mnaweza kuwa mmeshakutana na vijana wanaojituma na kufanya kazi kwa usahihi.
Pili natafuta mtu mwenye uzoefu na usimamizi wa mashamba (hasa ya nanasi) ambaye nitamuajiri kama Bibi au Bwana Shamba (Farm Manager). Kazi yake kubwa itakuwa ni kusimamia palizi kuhakikisha kwamba kazi ya kulitunza shamba inafanyika vizuri na kuwapangia kazi za kufanya vibarua. Hii inaweza kuwa ajira ya kudumu kwani mpango wangu ni kuwa ni ufikisha eka 30 za nanasi ifikapo 2014 pia na kufuga mifugo mbalimbali hapo shamba (mbuzi, ng'ombe, kuku, bata nk). Kwa hivi sasa niko kwenye ujenzi wa nyumba ya Farm Manager na pia kisima cha maji kitakachokuwa na uwezo wa kutunza lita 100,000.
Kama unawajua vijana wa kazi basi naomba uni-PM kwa mawasiliano zaidi tafadhali.
Nitashukuru sana kwa msaada wenu.
Eka ambazo nimepanda hadi sasa ni 12 na tatizo kubwa linalonikabili kwa sasa ni nguvu kazi. Vijana wengi ambao wananifanyia kazi wana tatizo la ulevi (sio beer za TBL ni mataptap), uzembe, wizi na udanganyifu . Wakipata pesa mpaka waimalize yote ndo warudi kazini na ukiwapa "advance" kabla ya kazi ndo inakula kwangu.
Bila shaka wale mnaojishghulisha na kilimo mnaweza kuwa mmeshakutana na vijana wanaojituma na kufanya kazi kwa usahihi.
Pili natafuta mtu mwenye uzoefu na usimamizi wa mashamba (hasa ya nanasi) ambaye nitamuajiri kama Bibi au Bwana Shamba (Farm Manager). Kazi yake kubwa itakuwa ni kusimamia palizi kuhakikisha kwamba kazi ya kulitunza shamba inafanyika vizuri na kuwapangia kazi za kufanya vibarua. Hii inaweza kuwa ajira ya kudumu kwani mpango wangu ni kuwa ni ufikisha eka 30 za nanasi ifikapo 2014 pia na kufuga mifugo mbalimbali hapo shamba (mbuzi, ng'ombe, kuku, bata nk). Kwa hivi sasa niko kwenye ujenzi wa nyumba ya Farm Manager na pia kisima cha maji kitakachokuwa na uwezo wa kutunza lita 100,000.
Kama unawajua vijana wa kazi basi naomba uni-PM kwa mawasiliano zaidi tafadhali.
Nitashukuru sana kwa msaada wenu.