Natafuta Serious Partner wa Kuanzisha Mradi Mkubwa Wa Nguruwe Tanzania

Kiasi gani kinahitajika
Habari wadau.

Mimi ni Mtanzania niliyebahatika kupata elimu katika nchi mbalimbali za Bara la Ulaya. Baada ya kumaliza elimu yangu nimerejea nchini kujenga taifa.

Kufuatia changamoto ya ajira nimeonelea nichukua route ya kujiajiri. Baada ya kufanya utafiti wa kina, nimejiridhisha kuwa mradi wa Ufugaji wa Nguruwe kibiashara (Commercial Piggery Project) unaweza lipa katika muda mfupi.

Lengo langu sio tu kufuga Nguruwe, bali kufuga na kuongezea thamani bidhaa nitakazizozalisha ili kuuza bidhaa hizo Kwenye upper-end market.

Nafahamu wapo watanzania wenye mitaji ila hawana muda wa kufanya mradi wa aina hii. Mimi nina ardhi kubwa kando ya mto Ruvu, access ya kupata soko zuri na elimu ya kutosha ambayo ninatarajia kuitumia katika mradi huo.

Hivyo nakaribisha wenye mitaji ya hali (Relevant education) na Mali (Fedha) ktk kufanikisha mradi huu.

Mambo yote yataenda kisomi/kisheria.

Karibuni sana
 
Hongera sana mimi ni kijana ,mwenye future kubwa sana lakin sijaona kijana mwenye maono kama wew inshort umebalikiwa sana ,pia nina maoni kidogo japo unaruhusiwa kunikosoa
1: anza kwanza uzalishaji wa nguruwe then utajisajili badae ukisha fikisha target ya nguruwe uliyo panga,nafikir mwaka moja tuu.utakuwa umefikisha nguruwe si chini ya mia nane nikitoa hasara,
2: usiwaze kuhusu sokoo maana lipo la uhakika badala yake unaweza unaweza kuuza kwa bei ya jumla nguruwe mzima itaripaa sana ,
3 ungekuwa iringa ungefaidi zaid maana ,kutengeneza mabanda ungetumia mabanzi ,na kumimina tu chini maana huku mabanzi ni bure kabisa .
4 ukianza mradi wako tengeneza bustan za mbogaa itasaidia kuwalisha wanyama kam supriment ,vitamin na madim source,
5 jiepushe na kununua nguruwe piglet wa kizazi kimoja kuepushaa inbreeding huwa inasumbua kidogo,
Naamin utafanikiwa pia tupo nyuma yako kwa ajili ya mawazo na maoni mbalimbali pia soko tutakisaidiaa .

Sent from my X-TIGI_V11 using JamiiForums mobile app
Nmevutiwa ghafla mkuu nipo Iringa ningefurahi unipatie elimu kidogo
 
Hello UrbanGentleman ahsante Kwa kupenda kufahamu zaidi. Tumeanza mchakato wa kutengeneza business plan, document ambayo itatupa uwezo wa kutambua gharama halisi za mradi huu. So later this week nitakupa makadirio ya gharama za Kuanzisha huu mradi.
Kiasi gani kinahitajika
 
Nijurishe as soon as possible
Hello UrbanGentleman ahsante Kwa kupenda kufahamu zaidi. Tumeanza mchakato wa kutengeneza business plan, document ambayo itatupa uwezo wa kutambua gharama halisi za mradi huu. So later this week nitakupa makadirio ya gharama za Kuanzisha huu mradi.
 
Ahsante Kwa kufwatilia. Tumeanza ku-develop a business plan Kwa ajili ya Mradi ili tujue tunaelekea wap na Kwa namna gani. Soon tutakutana tena na wadau kuijadili na kuiapprove ili ituongeze. Karibu sana
 
Naomba nitoe maoni yangu japo naweza kuwa na uandishi mbaya, ila ujitahidi kunielewa. Hii miradi ya ufugaji wa nguruwe mimi nilishawahi kufanya. Kwa kifupi zipo changamoto tena kubwa.

1. Ufugaji wowote ambao utanunua nguruwe then ukawapandisha na kuzalisha wototo, ufugaji huu ni hatari na utakupelekea kwenye hasara. Maana mara nyingi vifaranga wanakufa na wanaugua mara kwa mara. Pia ukuaji wao una shida, hivyo kuwa na vifaranga ambao sio wazuri. Waliodumaa

Nini ufanye? Nunua vifaranga wa nguruwe wa miezi mitatu (wapo wengi tu huku mitaani) ambao ni wazuri na wakubwa kiasi. wewe unaenda kuwalisha na ukishaona wamefikia ukubwa ambao wewe unaona wanafaa kwa biashara. Fanya biashara.

2. Soko la nguruwe lipo japo sio zuri kama unavyofikiri. Mara nyingi tunauza nguruwe wa wastani wa kilo 80-100 kwa kati ya shilingi 300000-350000/=. Na kuna kipindi Tunakosa wateja. Kiasi kwamba nguruwe aliyestahili kuuzwa unaendelea kumlisha kwa wiki kadhaa. Hii ni kutengeneza hasara. Hivyo soko huwa linapanda na kushuka kulingana na uhitaji. Kumbuka nguruwe wanafugwa karibu kila pembe ya hii nchi.

3. Kwa ufugaji wako wa kisomi (mimi sijasoma) naona unakwenda kushindwa kabla ya kuanza. Kivipi? Mara nyingi sisi tusiosoma na hatuna tabia ya kuweka kumbukumbu ya gharama tulizotumia kuanzia kununua vifaranga, vyakula, madawa, na kulipa mfanyakazi, tungekuwa tunaorodhesha vyote hivyo walllah tusingeweza kuuza kwa hizo bei za 300-350k. Tungeona hasara. Maana kifaranga mzuri tunanunua kwa shs 70-80k ndio uanze kumtunza.

Na si kweli kwamba kifaranga wa miezi mitatu ukimnunua unamlisha au kumtunza kwa miezi 6 kama ulivyosema. Utamtunza kwa zaidi ya mwaka. Vyakula na madawa + mfanyakazi + muda hata ukimuuza kwa 400k halipi.
Sasa kwa usomi wako jiandae kuorodhesha kila gharama afu uje uuze kwa bei unazosema uone kama utapata mteja. Nakuhakikishia hapa hasara ipo wazi.

Ushauri wangu kwako. Tafuta mtaji, jenga banda la kutosha nguruwe 50-80 wakubwa. Nenda mikoani nunua nguruwe wazuri kwa bei ya ukandamizaji. Safirisha mpaka hapo ruvu. Washushe. Chinja na Anza kuwaongezea thamani kama ulivyosema. Lakini hili wazo la kuwafunga, uwakuze mpaka wakue utapitia changamoto nyingi na nyingine ngumu.

Kazi njema
hii ndo inaitwa kukubaliana kutokukubaliana
 
Mkuu,hongera sana kwa kuwa na mawazo mazuri sana ya ubunifu wa mradi unaoweza kutoa ajira si kwako pekee bali kwa ushirika.

Kwa fikra yangu; ni kwamba mradi huo siyo mzuri kwa jamii kwani nguruwe hutumiwa zaidi kwa ajili ya kitoweo, watu wengi hawajui kwamba pamoja na madhara mengine yanayosabishwa na nyama ya nguruwe kama cancer pia ulaji wake huambukiza "USHOGA", angalia Mashoga wengi historia yao utakuta walianza kula nyama ya nguruwe kwa wingi toka wakiwa wadogo/watoto kama (staple food).

Kifupi ulaji "sana" wa nyama ya nguruwe inachangia "sana"watu kuwa mashoga.

Ushauri wangu (with due respect), Tafuta mradi mwingine.

🙏🏻🙏🏻
Asilimia kubwa ya mashoga wako coastal regions ambako wakazi wengi ni Muslims,Nyanda za juu huko tunakula hii kitu tangu utotoni huo upuuzi haupo
 
Asilimia kubwa ya mashoga wako coastal regions ambako wakazi wengi ni Muslims,Nyanda za juu huko tunakula hii kitu tangu utotoni huo upuuzi haupo


Ushoga utakuwepo kwa siri, kwani kwa mila na tamaduni za kiafrika ni aibu kubwa kujitangaza ushoga hadharani.

Halafu siku hizi hujasikia msemo wa "kula jicho" au "kula tigo" au "kula bata" au "kusasambua" nk, hiyo ni misemo inayowakilisha tabia iliyojengeka ya wanaume kuwaingilia wanawake kinyume na maumbile na hii huwa ndiyo hatua ya mwanzo ya watu kuelekea USHOGA, kwani shoga hauanzi papo kwa papo.

Watu wa ulaya na Asia mashariki ya mbali ndio walaji wakubwa wa kitimoto lakini ni Ulaya tu na nchi chache za Afrika Mashoga wanatambuliwa kisheria na hii ni baada ya mashoga kuongezeka huku kwetu (demand ni kubwa na supply lazima iongezeke/ haki zao lazima zilindwe)-- huko mashariki ya mbali huwezi kusikia Upuuzi huo wa watu kujitangaza ushoga kwasababu dini, tamaduni na mila zao haziruhusu jambo hilo kabisa sembuse kujitangaza!!??, shida Waafrika ni "Copy carts" ya watu wengine.

NB: Si kila shoga yupo hjvyo kwasababu ya kula kitimoto kwani wengine wamezaliwa wakiwa na huo ugonjwa wa Ushoga, lakini asilimia kubwa ya mashoga walianza kula SANA kitimoto wakiwa wadogo hadi utu uzima, ninaposema kula Kitimoto nadhani unajua, siyo eti robo kilo kwa mwezi mara moja!!-- ela ya BP!!😁, nazungumzia wale watu ambao kitimoto kwao ni "STAPLE FOOD" kama wazungu na huko mashariki ya mbali.
 
Mkuu umesoma post no 97??.

Halafu unasema; " kwa imani yenu"--- sasa nikuulize kwa imani yetu ipi ??, ujue Qur'an na Biblia zinasema nguruwe ni haramu na hata maandiko ya dini ya kiyahudi yanasema nguruwe ni haramu, kifupi ni kwamba Mungu mwenyewe aliyemuumha huyo nguruwe a aliyetuumba sisi anatukataza kula nyama ya
huyo nguruwe sasa sisi nani zaidi ya Mungu aliyetuumba?!!.

Kwakuwa Mungu katupatia akili ya utambuzi ni juu yetu kutafakari kwanini katukataza kula kitimoto na kitimoto anayo faida gani kwetu??, hayo ndiyo maswali ya kujiuliza.

FAIDA ZA KITIMOTO;

Miongoni mwa wanyama wanaokurubiana na binadamu (close related in metabolism) nguruwe yupo karibu mno na mwanadamu na ndiyo maana kuna nyuzi za kushonea vidonda (stiching) hutumika aina fulani ya utumbo wa nguruwe uliotayarishwa kitaalamu, pia kama nilivyosema kuna baadhi ya dawa za magonjwa ya binadamu hupewa kwanza nguruwe kuangalia kama zinayo madhara na pia kujua kama zinafaa katika tiba kwa magonjwa ambayo ni common kwa nguruwe na binadamu kama mafua nk,

Wanasayansi zama hizi wamekuwa wakitafiti viungo vya nguruwe kama macho, maini, mafigo,moyo, mapafu, kongosho nk, kama viungo mbadala wa viungo vilivyodhurika vya binadamu na imeonekana kuna mafanikio makubwa sana pia mafuta ya nguruwe yanaweza kutumika kama malighafi katika viwanda vya kemikali kama kutengenezea sabuni na lubricants (vilainishi nk), kifupi nguruwe anayo manufaa ila binadamu ni mnyama MROHO kuliko wanyama wote ndiyo maana hasikii onyo la Mungu juu ya uharamu wa nguruwe.

HASARA ZA KULA NYAMA YA NGURUWE:- niliishaekeza hasara zake ila hapa nitazieleza tena kwa faida ya wengine;
Madume ya Nguruwe hayana wivu, kamwe huwezi kuona madume ya nguruwe yakipigana kugombea jike, jike akiwepo ni mali ya wote-- watu wanaokula nguruwe hawashughuliki na wala hakasiriki kabisa akisikia mkewe anagegedwa kwasababu anakuwa karithi tabia za kinguruwe.

Ukiweka pamoja madume ya nguruwe hata kama kuna majike ni aghalabu kuyakuta yakigegedana kinyume cha maumbile (ushoga)--- watu wanaokula nguruwe ni aghalabu kuwaona wakiwa na hizo tabia, yaani wanaambukizwa tabia ya ushoga kutoka kwa nguruwe kwa sababu kiasi fulani "we are close related to nguruwe" katika metabolism kwa sababu sisi sote ni "omnivorous" na ndiyo maana kula nyama ya nguruwe ni KARIBU sana na kula nyama ya mtu jinsi watu wanavyo sema ukila nyama ya mtu huwezi kuacha na ndivyo ilivyo kwa nyama ya nguruwe kwani walaji wameibatiza kwa kuiita eti "mkuu wa meza".

Ulaji wa Nyama ya nguruwe unachochea sana ugonjwa wa kansa,yaani nyama yake imejaa "free radicals" na ukitaka mgonjwa wako wa kansa asipone wewe uwe ukimpa kitimoto.

Nguruwe anaambukiza magonjwa mengi ya minyoo kama nyama yake haikuandaliwa vizuri, kinyesi chake kimejaa wadudu wa kipindupindu na typhoid, mafuta yake yamejaa aina mbalimbali za sumu kwa sababu ndiyo store yake ya kuhifadhi sumu zitokazo na vyakula mbalimbali anavyokula na ndiyo maana huwezi kukuta nguruwe kafa kwa kuumwa na nyoka yeyote hata "black mamba" hawezi kumuua nguruwe, sumu ya 'mafuta" yake ukichanganya na sumu ya nyoka unapata "neutral".

Nyama ya nguruwe inayo madhara ya muda mrefu na mfupi, ya muda mfupi ni kwa wale wanaotokewa na mapele mwilini mara wanapokula na yale ya muda mrefu ni pamoja na kuambukizwa USHOGA na magonja ya cancer nk.

VYAKULA APENDAVYO NGURUWE.

Nguruwe ukimuwekea labda ugali na maharage na pembeni ukamuwekea nyama mbichi iliyooza inayotoa harufu mbaya na mafunza, kwanza atakula hiyo nyama iliyooza, inayotoa harufu mbaya na mafunza na akimaliza ndipo atakula huo ugali na maharage-- hii inaonyesha jinsi nguruwe alivyokuwa mchafu, na hata akishikwa na njaa hula watoto wake kitendo ambacho huweziona kwa wanyama wengine.

Sijafanya utafiti ili kuona kama "cannibalism" kwa baadhi ya watu inaweza kuwa ni kutokana na ulaji wa kitimoto kwa sababu nguruwe ni cannibalist.
😂😂😂 Imperically, ..... Ukila samaki mara kwa mara utaweza kuogelea kama samaki unao wala!!!!..
 
😂😂😂 Imperically, ..... Ukila samaki mara kwa mara utaweza kuogelea kama samaki unao wala!!!!..



Wewe vipi unaelewa au unataka kupoteza muda?!!, kwa mawazo yako finyu imperically hata ukila nyama ya kuku na Wewe utataga mayai !!😁😁 si ndiyo??.

Iko hivi; ukila nyama ya kuku aliyekufa kwa sumu nawewe utakufa, na ndivyo ilivyo kwa kula nyama ya nguruwe mtu unapata "tabia" na menendo ya nguruwe kama vile Ushoga nk, kwa sababu nguruwe anavyo vichocheo mwilini mwake vinavyo mchochea apende USHOGA vichocheo hivyo vinayo madhara hayohayo kwa mlaji wa kitimoto. Hiyo ndiyo substance ya hiyo mada.
 
Wewe vipi unaelewa au unataka kupoteza muda?!!, kwa mawazo yako finyu imperically hata ukila nyama ya kuku na Wewe utataga mayai !!😁😁 si ndiyo??.

Iko hivi; ukila nyama ya kuku aliyekufa kwa sumu nawewe utakufa, na ndivyo ilivyo kwa kula nyama ya nguruwe mtu unapata "tabia" na menendo ya nguruwe kama vile Ushoga nk, kwa sababu nguruwe anavyo vichocheo mwilini mwake vinavyo mchochea apende USHOGA vichocheo hivyo vinayo madhara hayohayo kwa mlaji wa kitimoto. Hiyo ndiyo substance ya hiyo mada.
😂😂😂 Ukila ya mbuzi utaota mapembeeeee😂😂😂😂......na utakula majani kabsaa....😂😂😂😂
 
Kufuatia maoni ya wadau waliosoma uzi huu imenipasa nitoe japo a concept note.

Kiufupi lengo kuu la mradi ni Kuanzisha ufugaji wa Nguruwe kibiashara - Commercial Piggery Project (as opposed to traditional/subsistence Piggery Project). Features za commercial Piggery project include

1. Profitable Business
2. Energy-saving technology
3. Ecologically clean production
4. Humane attitude to pigs

Nimechagua kufuga Nguruwe badala ya wanyama wengine Kwa sababu zifuatazo

1. Nguruwe ana relatively low feed conversion ratio (FCR) ambayo ni nzuri mana inaelezea ufanisi Mkubwa alionao wa kuzalisha nyama toka Kwenye chakula ana chokula. Yaani anatumia chakula kidogo kuzalisha Kilo moja ya nyama.

2. Nguruwe wanakua haraka (Wana high growth rate). Nguruwe aliyetunzwa vzr anaweza kuwa na kilo Kati ya 100 -110 ndani ya miezi 6.

3. Wanabeba mimba Kwa muda mfupi Sana i.e. three months, three weeks and three days= in total 114 days. Na wanaweza kuzaa Kwa wastani watoto 10-14 Kwa mzao. Hii inategemea ubora wa mbegu, chakula na afya yao. Nguruwe pia anaweza kuzaa mara 2 Kwa mwaka.

4. Nyama yake ni White meat, hivyo ni nzuri Kwa afya na wateja wengi wanaipenda.

5. Kwa Tanzania wafugaji wa kibiashara ni wachache na kimsingi wameshindwa kumeet market demand. Hivyo Kuna soko kubwa Sana nchini ambalo Kwa sasa linalazimika kuagiza nyama hiyo nje ya nchi mana hatujaweza bado zalisha Bidhaa wanzozihitaji.

6. Wazalishaji karibu wote wamejikita katika kuuza raw pork meat/live animals (nguruwe mzima mzima). Hivyo kuna uhaba Mkubwa Sana Sana wa Bidhaa za Nguruwe zilizoongezewa thamani kama specialized and packed pork cuts, Bacon, Smoked pork meat, pork sausages etc.

Kwa kutambua haya. Ndio nikawiwa kutafuta wenzangu wanaopenda kuungana nami ili tuchangamkie fursa hii.

Gharama za ufugaji wa Nguruwe.

Kwa ujimla gharama zina tofautiana Sana kulingana na namna unavyoendesha ufugaji wako. Gharama kubwa ktk ufugaji wa Nguruwe, ukiachia Ujenzi wa Banda la kisasa, zipo kwenye chakula. Japo kuna wataalamu wanaotoa gharama za makadirio, ukweli ni kwamba si rahisi kuwa realistic Kwenye makadirio hayo.

Chakula:

1) Nguruwe ana nyonya Kwa muda wa week 4 (siku 28). Baada ya hapo anapaswa kutengwa na mama yake na kuwekwa Kwenye Banda la kukulia ili kumpa mama yake muda wa kuzalisha joto ili apandwe tena. Nguruwe no Omnivore (hula nyama na majani, nafaka/mbegu) hivyo inapaswa umlishe chakula chenye mchanganyo na virutubisho vyote na ikifaa iwe katika form ya Pellets.

Baada ya kunyonya hula chakula cha uzito mbalimbali kulingana na uzito wao mfano.

2) Nguruwe mwenye 10-17kg anapaswa kula 0.8 kg Kwa siku

3) Nguruwe mwenye 18-29Kg anapaswa Kula 1kg Kwa siku

4) Nguruwe mwenye 30-40kg anapaswa Kula 1.5kg Kwa siku.

5) Nguruwe mwenye 40-60 kg anapaswa Kula 2kg Kwa siku.

6) Nguruwe mwenye 61-80kg anapaswa Kula 2.5kg Kwa siku.

7) Nguruwe mwenye 81-100kg anapaswa Kula 3kg Kwa siku.

8) Nguwure zaidi ya 100kg na mwenye mimba anapaswa Kula 6 kg.

Inashauriwa Nguruwe auzwe chini ya 120kg maana baada ya bado anakuwa na high feed conversion ratio. Anatumia chakula kingi kutengeneza kilo moja ya nyama hivyo ni hasara Kwa mfugaji.

Naweza kudadavua zaidi Kwa interested and serious partners baadaye.

Bei ya Mbegu (Breeding Stock)

Bei ya Nguruwe wa mbegu pia inategemea unahitaji mbegu aina gani, wa ukubwa gani na unamtoa wapi. Kuna aliyetaka niuzia wa mwezi mmoja Kwa 100,000 na wa miezi sita kwa 600,000 Dar Es Salaam. Hivyo bei zina range hapo.


Soko la Nguruwe.

Soko ni kubwa Sana kuanzia soko la wateja wa kawaida hadi mahotelini. Wakati kilo 1 ya raw meat inauzwa Kwa TZS 8000 Kwa bei ya rejareja, Kwenye mahoteli ambako wananunua Bidhaa zilizoongezewa dhamani, kilo moja ya Bidhaa hiyo huuzwa hadi TZS 30,000.

Kwenye ufugaji ninaotaka kuufanya Mimi target yangu ni Soko la mahotelini.

Nini kipo tayari Hadi sasa

Ninaye mtaalam wa kuongezea thamani yaani kufanya smoking, kufanya hizo pork cuts, kutengeneza bacon n.k.

Nina shamba zaidi ya heka 3 lipo mita 600 kando ya mto Ruvu, Mlandizi na umeme haupo mbali. Hivyo suala la Maji na umeme Kwenye shamba Hilo ni rahisi.

Nina kijana wa kazi mmoja na Mimi mwenyewe ntakuwa naishi hapo hapo Shambani muda mwingi.

Nina wataalamu wa magonjwa ya Nguruwe wawili ambao wameshaonesha interest ya kushirikiana nami katika hii project.

Vinavyokosekana Hadi sasa.

Mtaji Kwa maana ya Fedha za kujenga Banda la kisasa la kuaccomodate breeding stock ya Nguruwe angalau 50 na Banda la kutunzia watoto, kujenga processing unit/house, kuweka uzio eneo la banda, kununua chakula na breeding stock 50 pigs, kutengenezea cold room/chiller, smoker, kununua machine za cutting, vacuum na vifungashio, kujisajiri TFDA na TBS.

Kama Kuna maswali zaidi nitaendelea Kujibu.


Mzee mbona Kama umeng'oa kwenye andiko langu la kibiashara nililoliacha pale wizara ya kilimo vetenary na ofisi ya kilimo ifakara n siku zimepita ilkua 2014, sema mie sikuifanya hiyo project KWASABABU ya uhaba wa pesa sema ukijifunga mkanda unatoka
 
Habari wadau.

Mimi ni Mtanzania niliyebahatika kupata elimu katika nchi mbalimbali za Bara la Ulaya. Baada ya kumaliza elimu yangu nimerejea nchini kujenga taifa.

Kufuatia changamoto ya ajira nimeonelea nichukua route ya kujiajiri. Baada ya kufanya utafiti wa kina, nimejiridhisha kuwa mradi wa Ufugaji wa Nguruwe kibiashara (Commercial Piggery Project) unaweza lipa katika muda mfupi.

Lengo langu sio tu kufuga Nguruwe, bali kufuga na kuongezea thamani bidhaa nitakazizozalisha ili kuuza bidhaa hizo Kwenye upper-end market.

Nafahamu wapo watanzania wenye mitaji ila hawana muda wa kufanya mradi wa aina hii. Mimi nina ardhi kubwa kando ya mto Ruvu, access ya kupata soko zuri na elimu ya kutosha ambayo ninatarajia kuitumia katika mradi huo.

Hivyo nakaribisha wenye mitaji ya hali (Relevant education) na Mali (Fedha) ktk kufanikisha mradi huu.

Mambo yote yataenda kisomi/kisheria.

Karibuni sana
Ulipata mtu wa kupartner nae mi nafuga tayari njoo tupanuane mawazo
 
Nyongeza kidogo.

Mimi nipo mkoani ifakara, Morogoro. Ufugaji wa nguruwe kwa hapa ni rahisi kuliko sehemu yoyote nchini. Unapata pumba za Mpunga kwa bei ya kutupa. Maana hapa ndio wazalishaji wakubwa wa mpunga. Kg 70 ya pumba napata kwa shs 2500 hapo nishamlipa na mjazaji. Kwa nilivyo alwatan naweza kupata bure.

Mashudu ya alizeti yapo kwa wingi, Pumba za mahindi zipo kibao kwa kifupi ufugaji wa hapa ni rahisi. Ila changamoto zipo. Mimi sifanyi ufugaji wa kuzalisha, nafuga kuendeleza. Nanunua kwa kuchagua nguruwe wazuri ambao hawajadumaa.

Natengeneza chakula cha mwezi mzima kinanigharimu kama tsh 200k na kinatosha kulisha nguruwe 80-100 kwa mwezi. Ila pumba za mpunga zinazidi kwenye huo mchanganyiko.

Nachanganya pumba za mahindi, Mashudu ya alizeti, pumba za mpunga, chumvi, pig mix wakati mwingine na dagaa. Matengeneza gunia 30 zinatosha kulisha mwezi mzima. Nawalisha Ahsubuhi na jioni. Wanapewa majani kila baada ya siku tatu.

Ufugaji wangu ni kama kibubu. Nikiuza ndio nimevunja.
mkuu naomba nikutafute pm
 
Kwa upande wa nadharia(kwenye makaratasi) upo vizuri mkuu na kama hii nadharia kwenye vitendo itakua hivihivi basi ushindi ni 100%,Mara nyingi wataalamu wengi wa bongo huwa kwenye vitendo hawako vizuri.
Mungu akutangulie.
 
Pole Sana Kiongozi. Hapana siwezi kufanya hivyo na sina sababu ya kufanya hiyo. Sisi tumeanza from the scratch na tumeandaa mpango wetu wenyewe juzi tu. Fwatilia mpango wako uingie kazini.
Mzee mbona Kama umeng'oa kwenye andiko langu la kibiashara nililoliacha pale wizara ya kilimo vetenary na ofisi ya kilimo ifakara n siku zimepita ilkua 2014, sema mie sikuifanya hiyo project KWASABABU ya uhaba wa pesa sema ukijifunga mkanda unatoka
 
Back
Top Bottom