Natafuta Serious Partner wa Kuanzisha Mradi Mkubwa Wa Nguruwe Tanzania

.Hao nguruwe unawapeleka sokoni wakiwa na umri gani?!
Wanakuwa na uzito gani wanapoenda sokoni!!?
Sisi hatupeleki sokoni. Kuna wateja wanakuja toka Dsm, unampeleka bandani anachugua anaona wanamfaa. Tukiafikiana bei analipa anachukua mzigo wake.
Soko kubwa ni Dsm.
 
Ni sawa.Nilikuwa nna maanisha unawauza wakiwa na umri gani na uzito gani!!
Ila nimekuelewa;kwenu haijalishi umri wala uzito wa mnyama;yawezekana pia haijarishi ni gharama kiasi gani umetumia kuwalea hao nguruwe🤭.Hao jamaa wakija bandani wakachagua na mkaelewana basi wanachukua😊🤔!Nadhani namna hiyo ni kawaida katika ufugaji vijijini;ufugaji wa kujikimu. Kawaida huko vijijini mtu kuuza nguruwe wakiwa na umri wa mwaka mmoja au zaidi bali wakiwa bado wana uzito mdogo.Kwa mtu anaetaka kufuga nguruwe kibiashara labda anahitaji kufanya zaidi ya hivyo🤝🤝🤝
 
Ni sawa.Nilikuwa nna maanisha unawauza wakiwa na umri gani na uzito gani!!
Ila nimekuelewa;kwenu haijalishi umri wala uzito wa mnyama;yawezekana pia haijarishi ni gharama kiasi gani umetumia kuwalea hao nguruwe.Hao jamaa wakija bandani wakachagua na mkaelewana basi wanachukua!Nadhani namna hiyo ni kawaida katika ufugaji vijijini;ufugaji wa kujikimu. Kawaida huko vijijini mtu kuuza nguruwe wakiwa na umri wa mwaka mmoja au zaidi bali wakiwa bado wana uzito mdogo.Kwa mtu anaetaka kufuga nguruwe kibiashara labda anahitaji kufanya zaidi ya hivyo
Hapana. Tunachofanya, ni kuwa nguruwe wanakuwa na wastani wa kg 80-100. Namoa pei nayotaka, mara nyingi ni 300k mpaka 350k. Akiingia bandani anachagua wanaomridhisha. Kwa kuwa wale nguruwe walinunuliwa wakiwa wanalingana basi lazima apate wengi. Akichukua 30 tu sikosi 10m.
 
Habari wadau.

Mimi ni Mtanzania niliyebahatika kupata elimu katika nchi mbalimbali za Bara la Ulaya. Baada ya kumaliza elimu yangu nimerejea nchini kujenga taifa.

Kufuatia changamoto ya ajira nimeonelea nichukua route ya kujiajiri. Baada ya kufanya utafiti wa kina, nimejiridhisha kuwa mradi wa Ufugaji wa Nguruwe kibiashara (Commercial Piggery Project) unaweza lipa katika muda mfupi.

Lengo langu sio tu kufuga Nguruwe, bali kufuga na kuongezea thamani bidhaa nitakazizozalisha ili kuuza bidhaa hizo Kwenye upper-end market.

Nafahamu wapo watanzania wenye mitaji ila hawana muda wa kufanya mradi wa aina hii. Mimi nina ardhi kubwa kando ya mto Ruvu, access ya kupata soko zuri na elimu ya kutosha ambayo ninatarajia kuitumia katika mradi huo.

Hivyo nakaribisha wenye mitaji ya hali (Relevant education) na Mali (Fedha) ktk kufanikisha mradi huu.

Mambo yote yataenda kisomi/kisheria.

Karibuni sana
Hongera sana kijana kwa maono yako
 
Ahsante Tutor B. Ntawasiliana nawe. Nimeona namba yako.
Nimefurahi sana kukutana na uzi huu na nina siku nyingi sijaingia JF.
Kwa upande wangu naweza kukujoin kwa kuwekeza kwenye teknolojia ya kuzalisha chakula cha mifugo hao kwa kupunguza gharama ya malisho zaidi ya 50%
Niwe wazi ni kwamba kwa sasa najishughulisha zaidi na ufundishaji wa teknolojia ya Hydroponics Fodder pamoja na kilimo cha Azolla. Kwa pamoja yote hayo ni kwa ajili ya kupunguza gharama za malisho ili kuongeza faida kwa mfugaji.
Kama utakuwa umenielewa (wewe mtoa mada) tunaweza kuwasiliana zaidi.
 
Kufuatia maoni ya wadau waliosoma uzi huu imenipasa nitoe japo a concept note.

Kiufupi lengo kuu la mradi ni Kuanzisha ufugaji wa Nguruwe kibiashara - Commercial Piggery Project (as opposed to traditional/subsistence Piggery Project). Features za commercial Piggery project include

1. Profitable Business
2. Energy-saving technology
3. Ecologically clean production
4. Humane attitude to pigs

Nimechagua kufuga Nguruwe badala ya wanyama wengine Kwa sababu zifuatazo

1. Nguruwe ana relatively low feed conversion ratio (FCR) ambayo ni nzuri mana inaelezea ufanisi Mkubwa alionao wa kuzalisha nyama toka Kwenye chakula ana chokula. Yaani anatumia chakula kidogo kuzalisha Kilo moja ya nyama.

2. Nguruwe wanakua haraka (Wana high growth rate). Nguruwe aliyetunzwa vzr anaweza kuwa na kilo Kati ya 100 -110 ndani ya miezi 6.

3. Wanabeba mimba Kwa muda mfupi Sana i.e. three months, three weeks and three days= in total 114 days. Na wanaweza kuzaa Kwa wastani watoto 10-14 Kwa mzao. Hii inategemea ubora wa mbegu, chakula na afya yao. Nguruwe pia anaweza kuzaa mara 2 Kwa mwaka.

4. Nyama yake ni White meat, hivyo ni nzuri Kwa afya na wateja wengi wanaipenda.

5. Kwa Tanzania wafugaji wa kibiashara ni wachache na kimsingi wameshindwa kumeet market demand. Hivyo Kuna soko kubwa Sana nchini ambalo Kwa sasa linalazimika kuagiza nyama hiyo nje ya nchi mana hatujaweza bado zalisha Bidhaa wanzozihitaji.

6. Wazalishaji karibu wote wamejikita katika kuuza raw pork meat/live animals (nguruwe mzima mzima). Hivyo kuna uhaba Mkubwa Sana Sana wa Bidhaa za Nguruwe zilizoongezewa thamani kama specialized and packed pork cuts, Bacon, Smoked pork meat, pork sausages etc.

Kwa kutambua haya. Ndio nikawiwa kutafuta wenzangu wanaopenda kuungana nami ili tuchangamkie fursa hii.

Gharama za ufugaji wa Nguruwe.

Kwa ujimla gharama zina tofautiana Sana kulingana na namna unavyoendesha ufugaji wako. Gharama kubwa ktk ufugaji wa Nguruwe, ukiachia Ujenzi wa Banda la kisasa, zipo kwenye chakula. Japo kuna wataalamu wanaotoa gharama za makadirio, ukweli ni kwamba si rahisi kuwa realistic Kwenye makadirio hayo.

Chakula:

1) Nguruwe ana nyonya Kwa muda wa week 4 (siku 28). Baada ya hapo anapaswa kutengwa na mama yake na kuwekwa Kwenye Banda la kukulia ili kumpa mama yake muda wa kuzalisha joto ili apandwe tena. Nguruwe no Omnivore (hula nyama na majani, nafaka/mbegu) hivyo inapaswa umlishe chakula chenye mchanganyo na virutubisho vyote na ikifaa iwe katika form ya Pellets.

Baada ya kunyonya hula chakula cha uzito mbalimbali kulingana na uzito wao mfano.

2) Nguruwe mwenye 10-17kg anapaswa kula 0.8 kg Kwa siku

3) Nguruwe mwenye 18-29Kg anapaswa Kula 1kg Kwa siku

4) Nguruwe mwenye 30-40kg anapaswa Kula 1.5kg Kwa siku.

5) Nguruwe mwenye 40-60 kg anapaswa Kula 2kg Kwa siku.

6) Nguruwe mwenye 61-80kg anapaswa Kula 2.5kg Kwa siku.

7) Nguruwe mwenye 81-100kg anapaswa Kula 3kg Kwa siku.

8) Nguwure zaidi ya 100kg na mwenye mimba anapaswa Kula 6 kg.

Inashauriwa Nguruwe auzwe chini ya 120kg maana baada ya bado anakuwa na high feed conversion ratio. Anatumia chakula kingi kutengeneza kilo moja ya nyama hivyo ni hasara Kwa mfugaji.

Naweza kudadavua zaidi Kwa interested and serious partners baadaye.

Bei ya Mbegu (Breeding Stock)

Bei ya Nguruwe wa mbegu pia inategemea unahitaji mbegu aina gani, wa ukubwa gani na unamtoa wapi. Kuna aliyetaka niuzia wa mwezi mmoja Kwa 100,000 na wa miezi sita kwa 600,000 Dar Es Salaam. Hivyo bei zina range hapo.


Soko la Nguruwe.

Soko ni kubwa Sana kuanzia soko la wateja wa kawaida hadi mahotelini. Wakati kilo 1 ya raw meat inauzwa Kwa TZS 8000 Kwa bei ya rejareja, Kwenye mahoteli ambako wananunua Bidhaa zilizoongezewa dhamani, kilo moja ya Bidhaa hiyo huuzwa hadi TZS 30,000.

Kwenye ufugaji ninaotaka kuufanya Mimi target yangu ni Soko la mahotelini.

Nini kipo tayari Hadi sasa

Ninaye mtaalam wa kuongezea thamani yaani kufanya smoking, kufanya hizo pork cuts, kutengeneza bacon n.k.

Nina shamba zaidi ya heka 3 lipo mita 600 kando ya mto Ruvu, Mlandizi na umeme haupo mbali. Hivyo suala la Maji na umeme Kwenye shamba Hilo ni rahisi.

Nina kijana wa kazi mmoja na Mimi mwenyewe ntakuwa naishi hapo hapo Shambani muda mwingi.

Nina wataalamu wa magonjwa ya Nguruwe wawili ambao wameshaonesha interest ya kushirikiana nami katika hii project.

Vinavyokosekana Hadi sasa.

Mtaji Kwa maana ya Fedha za kujenga Banda la kisasa la kuaccomodate breeding stock ya Nguruwe angalau 50 na Banda la kutunzia watoto, kujenga processing unit/house, kuweka uzio eneo la banda, kununua chakula na breeding stock 50 pigs, kutengenezea cold room/chiller, smoker, kununua machine za cutting, vacuum na vifungashio, kujisajiri TFDA na TBS.

Kama Kuna maswali zaidi nitaendelea Kujibu.
Umeelezea vizuri..!

Mimi nimfugaji , na tuna chama cha wafugaji wa nguruwe wa kisasa kinaitwa TAPIFA, HQ ni morogoro. Ukiweza fika hapo, unaweza tafuta watu mkainvest now. But kutoa ardhi bila kuwa na fedha ni kazi bure. Nguruwe 50 sio msikhara. Inabidi uwe na sio chini ya 10M. Na unaanza kuona matunda yake baada ya miaka 2-3 kama ukifuga vizuri,
 
🤣🤣🤣
Words are opinions;action is the only truth🤣🤣

Hapana. Tunachofanya, ni kuwa nguruwe wanakuwa na wastani wa kg 80-100. Namoa pei nayotaka, mara nyingi ni 300k mpaka 350k. Akiingia bandani anachagua wanaomridhisha. Kwa kuwa wale nguruwe walinunuliwa wakiwa wanalingana basi lazima apate wengi. Akichukua 30 tu sikosi 10m.
🤣🤣
 
Naomba nitoe maoni yangu japo naweza kuwa na uandishi mbaya, ila ujitahidi kunielewa. Hii miradi ya ufugaji wa nguruwe mimi nilishawahi kufanya. Kwa kifupi zipo changamoto tena kubwa.

1. Ufugaji wowote ambao utanunua nguruwe then ukawapandisha na kuzalisha wototo, ufugaji huu ni hatari na utakupelekea kwenye hasara. Maana mara nyingi vifaranga wanakufa na wanaugua mara kwa mara. Pia ukuaji wao una shida, hivyo kuwa na vifaranga ambao sio wazuri. Waliodumaa

Nini ufanye? Nunua vifaranga wa nguruwe wa miezi mitatu (wapo wengi tu huku mitaani) ambao ni wazuri na wakubwa kiasi. wewe unaenda kuwalisha na ukishaona wamefikia ukubwa ambao wewe unaona wanafaa kwa biashara. Fanya biashara.

2. Soko la nguruwe lipo japo sio zuri kama unavyofikiri. Mara nyingi tunauza nguruwe wa wastani wa kilo 80-100 kwa kati ya shilingi 300000-350000/=. Na kuna kipindi Tunakosa wateja. Kiasi kwamba nguruwe aliyestahili kuuzwa unaendelea kumlisha kwa wiki kadhaa. Hii ni kutengeneza hasara. Hivyo soko huwa linapanda na kushuka kulingana na uhitaji. Kumbuka nguruwe wanafugwa karibu kila pembe ya hii nchi.

3. Kwa ufugaji wako wa kisomi (mimi sijasoma) naona unakwenda kushindwa kabla ya kuanza. Kivipi? Mara nyingi sisi tusiosoma na hatuna tabia ya kuweka kumbukumbu ya gharama tulizotumia kuanzia kununua vifaranga, vyakula, madawa, na kulipa mfanyakazi, tungekuwa tunaorodhesha vyote hivyo walllah tusingeweza kuuza kwa hizo bei za 300-350k. Tungeona hasara. Maana kifaranga mzuri tunanunua kwa shs 70-80k ndio uanze kumtunza.

Na si kweli kwamba kifaranga wa miezi mitatu ukimnunua unamlisha au kumtunza kwa miezi 6 kama ulivyosema. Utamtunza kwa zaidi ya mwaka. Vyakula na madawa + mfanyakazi + muda hata ukimuuza kwa 400k halipi.
Sasa kwa usomi wako jiandae kuorodhesha kila gharama afu uje uuze kwa bei unazosema uone kama utapata mteja. Nakuhakikishia hapa hasara ipo wazi.

Ushauri wangu kwako. Tafuta mtaji, jenga banda la kutosha nguruwe 50-80 wakubwa. Nenda mikoani nunua nguruwe wazuri kwa bei ya ukandamizaji. Safirisha mpaka hapo ruvu. Washushe. Chinja na Anza kuwaongezea thamani kama ulivyosema. Lakini hili wazo la kuwafunga, uwakuze mpaka wakue utapitia changamoto nyingi na nyingine ngumu.

Kazi njema
Mkuu uko mkoa gani?Ngurue wanatafutwa sana maana nakumbuka kipindi niko moshi,kulikua kuna wadau wanatoka Dar kutafuta ngurue,na walituambia kuna kipindi wanaenda mpaka mbulu kutafuta ngurue,mama yangu alikua mfugaji mzuri sana,na Ngurue wa 70kg alikua anamuuza 350k,hii ni kwa wastani wa 5000kwa kg.
Na pia alikua anasuply kiwanda cha soseji Arusha,na hawa wa soseji arusha walikua hawana longolongo,ukiwa na breed nzuri,na ngurue wa kiume uwe umemuasi toka akiwa na miezi mitatu,amasivyo nyama inakua na harufu ambayo madume wanakua nayo,na kwenye soseji hawataki iyo harufu.Ngurue wakifika kiwandani tuu,hela mama anawekewa CRDB Chap!
So demand ya Ngurue in kubwa sana has a Arusha,Moshi,Dar na Mwanza
 
Nguruwe ni nyama tamu sana kwa kweli, kuhsu madhara, kitu chochote ukikitumia kupita kiasi kina madhara, hata nyama ya ng'ombe ina madhara... tusivuke mipaka, inapoishia haki yako, ni mwanzo wa haki ya mtu mwingine
 
Ngurue mzuri ni wa miezi tisa toka wamezaliwa ukimtunza vizuri anakua na kilo kati ya 65-75,na nivizuri ukawaasi wakiwa na miezi mitatu
Na wanahitaji maji asikudanganye mtu hasa kipindi cha joto ile mida ya mchana unawamwagia maji
Kijijini kwetu tuko karibu na mto na mzee kamfungia pump mama kwa ajili ya kuvuta maji kwa ajiili ya ngurue na maboga,maana mama hua anapanda maboga kwa ajili ya ngurue, maboga na migomba na majani shambani,vinampunguzia sana gharama ya chakula
.Hao nguruwe unawapeleka sokoni wakiwa na umri gani?!
Wanakuwa na uzito gani wanapoenda sokoni!!?
 
Hao wa kushirikiana nao unahitaji mtu mmoja ama ata kama ni 20. Namaanisha huyu katoa kiasi hichi yule kile mpaka kupata kiasi kinacho itajika.
Kwa mtazamo wangu majadiliano ya kiasi cha mtaji kinapaswa kujadiliwa na interested parties. Kama nilivyoeleza mtaji una vary kutegemeana na mnachotaka kufanya. Hivyo tukishaafikiana, wale watakaopenda tutakutana na kujadiliana suala Hilo Kwa kina. Hapa nimewasilisha mada tu. Hizo details itapendeza zikijadiliwa na wanahisa/interested partners.
 
Wanaweza wakawa zaidi ya mmoja. So far kuna watu tayari wameshaonesha interest ya kufanya kazi zaidi ya watu wawili. So tunakaribisha wadau wengine.
Hao wa kushirikiana nao unahitaji mtu mmoja ama ata kama ni 20. Namaanisha huyu katoa kiasi hichi yule kile mpaka kupata kiasi kinacho itajika.
 
Mkuu uko mkoa gani?Ngurue wanatafutwa sana maana nakumbuka kipindi niko moshi,kulikua kuna wadau wanatoka Dar kutafuta ngurue,na walituambia kuna kipindi wanaenda mpaka mbulu kutafuta ngurue,mama yangu alikua mfugaji mzuri sana,na Ngurue wa 70kg alikua anamuuza 350k,hii ni kwa wastani wa 5000kwa kg.
Na pia alikua anasuply kiwanda cha soseji Arusha,na hawa wa soseji arusha walikua hawana longolongo,ukiwa na breed nzuri,na ngurue wa kiume uwe umemuasi toka akiwa na miezi mitatu,amasivyo nyama inakua na harufu ambayo madume wanakua nayo,na kwenye soseji hawataki iyo harufu.Ngurue wakifika kiwandani tuu,hela mama anawekewa CRDB Chap!
So demand ya Ngurue in kubwa sana has a Arusha,Moshi,Dar na Mwanza
Nipo morogoro. Wilaya ya kilombero mjini ifakara.
 
Habari wadau.

Mimi ni Mtanzania niliyebahatika kupata elimu katika nchi mbalimbali za Bara la Ulaya. Baada ya kumaliza elimu yangu nimerejea nchini kujenga taifa.

Kufuatia changamoto ya ajira nimeonelea nichukua route ya kujiajiri. Baada ya kufanya utafiti wa kina, nimejiridhisha kuwa mradi wa Ufugaji wa Nguruwe kibiashara (Commercial Piggery Project) unaweza lipa katika muda mfupi.

Lengo langu sio tu kufuga Nguruwe, bali kufuga na kuongezea thamani bidhaa nitakazizozalisha ili kuuza bidhaa hizo Kwenye upper-end market.

Nafahamu wapo watanzania wenye mitaji ila hawana muda wa kufanya mradi wa aina hii. Mimi nina ardhi kubwa kando ya mto Ruvu, access ya kupata soko zuri na elimu ya kutosha ambayo ninatarajia kuitumia katika mradi huo.

Hivyo nakaribisha wenye mitaji ya hali (Relevant education) na Mali (Fedha) ktk kufanikisha mradi huu.

Mambo yote yataenda kisomi/kisheria.

Karibuni sana


Mkuu,hongera sana kwa kuwa na mawazo mazuri sana ya ubunifu wa mradi unaoweza kutoa ajira si kwako pekee bali kwa ushirika.

Kwa fikra yangu; ni kwamba mradi huo siyo mzuri kwa jamii kwani nguruwe hutumiwa zaidi kwa ajili ya kitoweo, watu wengi hawajui kwamba pamoja na madhara mengine yanayosabishwa na nyama ya nguruwe kama cancer pia ulaji wake huambukiza "USHOGA", angalia Mashoga wengi historia yao utakuta walianza kula nyama ya nguruwe kwa wingi toka wakiwa wadogo/watoto kama (staple food).

Kifupi ulaji "sana" wa nyama ya nguruwe inachangia "sana"watu kuwa mashoga.

Ushauri wangu (with due respect), Tafuta mradi mwingine.

🙏🏻🙏🏻
 
Mkuu,hongera sana kwa kuwa na mawazo mazuri sana ya ubunifu wa mradi unaoweza kutoa ajira si kwako pekee bali kwa ushirika.

Kwa fikra yangu; ni kwamba mradi huo siyo mzuri kwa jamii kwani nguruwe hutumiwa zaidi kwa ajili ya kitoweo, watu wengi hawajui kwamba pamoja na madhara mengine yanayosabishwa na nyama ya nguruwe kama cancer pia ulaji wake huambukiza "USHOGA", angalia Mashoga wengi historia yao utakuta walianza kula nyama ya nguruwe kwa wingi toka wakiwa wadogo/watoto kama (staple food).

Kifupi ulaji "sana" wa nyama ya nguruwe inachangia "sana"watu kuwa mashoga.

Ushauri wangu (with due respect), Tafuta mradi mwingine.

Pork meat is one of the best meat ever!!
Usidanganye watu.
Kuna joint moja iko nyamanoro,kabla hujafika njia ya kupandisha kawekamo kuna kiti moto moja matata Sana'a!This wkend lazima nimshtue boss tukatandike kilo na ndizi nne.
 
Back
Top Bottom