Natafuta Serious Partner wa Kuanzisha Mradi Mkubwa Wa Nguruwe Tanzania

Habari wadau.

Mimi ni Mtanzania niliyebahatika kupata elimu katika nchi mbalimbali za Bara la Ulaya. Baada ya kumaliza elimu yangu nimerejea nchini kujenga taifa.

Kufuatia changamoto ya ajira nimeonelea nichukua route ya kujiajiri. Baada ya kufanya utafiti wa kina, nimejiridhisha kuwa mradi wa Ufugaji wa Nguruwe kibiashara (Commercial Piggery Project) unaweza lipa katika muda mfupi.

Lengo langu sio tu kufuga Nguruwe, bali kufuga na kuongezea thamani bidhaa nitakazizozalisha ili kuuza bidhaa hizo Kwenye upper-end market.

Nafahamu wapo watanzania wenye mitaji ila hawana muda wa kufanya mradi wa aina hii. Mimi nina ardhi kubwa kando ya mto Ruvu, access ya kupata soko zuri na elimu ya kutosha ambayo ninatarajia kuitumia katika mradi huo.

Hivyo nakaribisha wenye mitaji ya hali (Relevant education) na Mali (Fedha) ktk kufanikisha mradi huu.

Mambo yote yataenda kisomi/kisheria.

Karibuni sana
Daaah...! Nina wazo hilo muda mrefu mkuu,na ardhi nilishanunua. Lakini ardhi yako iko mahala pazuri kuliko mimi,nafikiri tukikubariana. Ni wazo zuri,halina mjadala linavusha
 
Haa haa haa karibu Sana Kiongozi. Hakuna linaloshindikana. Nimefurahi kusikia Una wazo kama hili. Ni-PM Kwa majadiliano zaidi.
Daaah...! Nina wazo hilo muda mrefu mkuu,na ardhi nilishanunua. Lakini ardhi yako iko mahala pazuri kuliko mimi,nafikiri tukikubariana. Ni wazo zuri,halina mjadala linavusha
 
kwa makadirio tu itahitajika 100,000,000+ kwa, hali ya mifuko ya wengi + uaminifu na watanzania tulivyo wataalam kwenye risk cakculation utaambulia kuungwa mkono kwa kauli tu badala ya vitendo.

nashauri upange mradi wako ktk hatua/phases hata 4. kama unaanza na banda la banzi+nguruwe 10 utakaowauza hai itapendeza.

baada ya kuona faida panua banda, ongeza mbegu mara mbili au tatu

hatua ya 3 jenga miundombinu kwa kutumia faida na kuanza kusaka wadhamini+wadau wa kuunga juhudi tyr ukiwa na kianzio.

mwisho panua soko lako ulilolenga (hotels), vyombo na mabanda ya kisasa sanjari na usajili ktk mamlaka husika ukiwa umeshaonja matunda.

nchi yangu ya Tanzania imejaaliwa watu wenye vipawa vyote, wajuaji, wakatisha tamaa, werevu wa kusigana, matapeli wa kila hali, washirikina na non risk takers (sijui niisemeje kwa kiswahili) . usitegemee atokee mtanzania akuamini kwa maneno matupu tu hayo na hesabu zako za kisomi (iweke sawa hesabu za makaratasi) badala yako watakuwela kundi moja na wale inspiration speakers; wanahamasisha kilimo cha biashara mf. bustani kuwa unatumua milioni 1 ulivuna unapiga milioni 10. amini bure ekari 3 bila hatua uliyokwishapiga kuelekea wazo lako, hazitoshi kumshawishi mtu amwage pesa.

mimi ni miongoni mwa watanzania wagumu kumuamini msomi wa nchi hii kwa taaluma ya uchumi. maramia nimwamini mwanasiasa na ahadi zake maana huwa nimejindaa kisaikolojia kwa kitakachofuata, huwa wanaanguka lakini baada ya kujaribu na hakika hututia matumaini kuwa awamu ijayo watafanikisha. laiti maafisa ugani na bw/bi. kilimo wangekuwa lau na mashamba darasa ya lau rbo heka kutuwekea elimu zao kutoka makaratasi kuwa vitendo ingefaa kunibadili.


naungana na mchangiaji hapo juu.

sisi ambao hatukusoma/hatukubahatika kuajiriwa hakuna fursa ambazo hatujajaribu. kilimi, ufugaji, biashara, viwanda vidogo (vyerehani, mashine za, mbao na nafaka) we speak frankly from experience. ni msomi tu anatuchukulia poa kwa vile anatuzidi hesabu


hitimisho :
unda kundi la jamaa zako pengine school mates,members wa grp za whatsap, work mates mchangishane hata 500,000 au m1 kwa watu kama 10/20 mjenge credibility, hapo tutawapokea kirahisi hata kwa kutuuzia hisa (chonde tu zisije kuwa km za voda).


KILA LA KHERI!

Nimekupenda bure
 
Naomba nitoe maoni yangu japo naweza kuwa na uandishi mbaya, ila ujitahidi kunielewa. Hii miradi ya ufugaji wa nguruwe mimi nilishawahi kufanya. Kwa kifupi zipo changamoto tena kubwa.

1. Ufugaji wowote ambao utanunua nguruwe then ukawapandisha na kuzalisha wototo, ufugaji huu ni hatari na utakupelekea kwenye hasara. Maana mara nyingi vifaranga wanakufa na wanaugua mara kwa mara. Pia ukuaji wao una shida, hivyo kuwa na vifaranga ambao sio wazuri. Waliodumaa

Nini ufanye? Nunua vifaranga wa nguruwe wa miezi mitatu (wapo wengi tu huku mitaani) ambao ni wazuri na wakubwa kiasi. wewe unaenda kuwalisha na ukishaona wamefikia ukubwa ambao wewe unaona wanafaa kwa biashara. Fanya biashara.

2. Soko la nguruwe lipo japo sio zuri kama unavyofikiri. Mara nyingi tunauza nguruwe wa wastani wa kilo 80-100 kwa kati ya shilingi 300000-350000/=. Na kuna kipindi Tunakosa wateja. Kiasi kwamba nguruwe aliyestahili kuuzwa unaendelea kumlisha kwa wiki kadhaa. Hii ni kutengeneza hasara. Hivyo soko huwa linapanda na kushuka kulingana na uhitaji. Kumbuka nguruwe wanafugwa karibu kila pembe ya hii nchi.

3. Kwa ufugaji wako wa kisomi (mimi sijasoma) naona unakwenda kushindwa kabla ya kuanza. Kivipi? Mara nyingi sisi tusiosoma na hatuna tabia ya kuweka kumbukumbu ya gharama tulizotumia kuanzia kununua vifaranga, vyakula, madawa, na kulipa mfanyakazi, tungekuwa tunaorodhesha vyote hivyo walllah tusingeweza kuuza kwa hizo bei za 300-350k. Tungeona hasara. Maana kifaranga mzuri tunanunua kwa shs 70-80k ndio uanze kumtunza.

Na si kweli kwamba kifaranga wa miezi mitatu ukimnunua unamlisha au kumtunza kwa miezi 6 kama ulivyosema. Utamtunza kwa zaidi ya mwaka. Vyakula na madawa + mfanyakazi + muda hata ukimuuza kwa 400k halipi.
Sasa kwa usomi wako jiandae kuorodhesha kila gharama afu uje uuze kwa bei unazosema uone kama utapata mteja. Nakuhakikishia hapa hasara ipo wazi.

Ushauri wangu kwako. Tafuta mtaji, jenga banda la kutosha nguruwe 50-80 wakubwa. Nenda mikoani nunua nguruwe wazuri kwa bei ya ukandamizaji. Safirisha mpaka hapo ruvu. Washushe. Chinja na Anza kuwaongezea thamani kama ulivyosema. Lakini hili wazo la kuwafunga, uwakuze mpaka wakue utapitia changamoto nyingi na nyingine ngumu.

Kazi njema

Watu mna madini Kama yote.

Nimependa maoni yako.
 
Watu mna madini Kama yote.

Nimependa maoni yako.
Nyongeza kidogo.

Mimi nipo mkoani ifakara, Morogoro. Ufugaji wa nguruwe kwa hapa ni rahisi kuliko sehemu yoyote nchini. Unapata pumba za Mpunga kwa bei ya kutupa. Maana hapa ndio wazalishaji wakubwa wa mpunga. Kg 70 ya pumba napata kwa shs 2500 hapo nishamlipa na mjazaji. Kwa nilivyo alwatan naweza kupata bure.

Mashudu ya alizeti yapo kwa wingi, Pumba za mahindi zipo kibao kwa kifupi ufugaji wa hapa ni rahisi. Ila changamoto zipo. Mimi sifanyi ufugaji wa kuzalisha, nafuga kuendeleza. Nanunua kwa kuchagua nguruwe wazuri ambao hawajadumaa.

Natengeneza chakula cha mwezi mzima kinanigharimu kama tsh 200k na kinatosha kulisha nguruwe 80-100 kwa mwezi. Ila pumba za mpunga zinazidi kwenye huo mchanganyiko.

Nachanganya pumba za mahindi, Mashudu ya alizeti, pumba za mpunga, chumvi, pig mix wakati mwingine na dagaa. Matengeneza gunia 30 zinatosha kulisha mwezi mzima. Nawalisha Ahsubuhi na jioni. Wanapewa majani kila baada ya siku tatu.

Ufugaji wangu ni kama kibubu. Nikiuza ndio nimevunja.
 
Ahsante 072, nashkuru Kwa kunipa taarifa na uzoefu wako. Utakuwa wa msaada katika kupata vyakula toka huko kwenu.
Nyongeza kidogo.

Mimi nipo mkoani ifakara, Morogoro. Ufugaji wa nguruwe kwa hapa ni rahisi kuliko sehemu yoyote nchini. Unapata pumba za Mpunga kwa bei ya kutupa. Maana hapa ndio wazalishaji wakubwa wa mpunga. Kg 70 ya pumba napata kwa shs 2500 hapo nishamlipa na mjazaji. Kwa nilivyo alwatan naweza kupata bure.

Mashudu ya alizeti yapo kwa wingi, Pumba za mahindi zipo kibao kwa kifupi ufugaji wa hapa ni rahisi. Ila changamoto zipo. Mimi sifanyi ufugaji wa kuzalisha, nafuga kuendeleza. Nanunua kwa kuchagua nguruwe wazuri ambao hawajadumaa.

Natengeneza chakula cha mwezi mzima kinanigharimu kama tsh 200k na kinatosha kulisha nguruwe 80-100 kwa mwezi. Ila pumba za mpunga zinazidi kwenye huo mchanganyiko.

Nachanganya pumba za mahindi, Mashudu ya alizeti, pumba za mpunga, chumvi, pig mix wakati mwingine na dagaa. Matengeneza gunia 30 zinatosha kulisha mwezi mzima. Nawalisha Ahsubuhi na jioni. Wanapewa majani kila baada ya siku tatu.

Ufugaji wangu ni kama kibubu. Nikiuza ndio nimevunja.
 
kwa makadirio tu itahitajika 100,000,000+ kwa, hali ya mifuko ya wengi + uaminifu na watanzania tulivyo wataalam kwenye risk cakculation utaambulia kuungwa mkono kwa kauli tu badala ya vitendo.

nashauri upange mradi wako ktk hatua/phases hata 4. kama unaanza na banda la banzi+nguruwe 10 utakaowauza hai itapendeza.

baada ya kuona faida panua banda, ongeza mbegu mara mbili au tatu

hatua ya 3 jenga miundombinu kwa kutumia faida na kuanza kusaka wadhamini+wadau wa kuunga juhudi tyr ukiwa na kianzio.

mwisho panua soko lako ulilolenga (hotels), vyombo na mabanda ya kisasa sanjari na usajili ktk mamlaka husika ukiwa umeshaonja matunda.

nchi yangu ya Tanzania imejaaliwa watu wenye vipawa vyote, wajuaji, wakatisha tamaa, werevu wa kusigana, matapeli wa kila hali, washirikina na non risk takers (sijui niisemeje kwa kiswahili) . usitegemee atokee mtanzania akuamini kwa maneno matupu tu hayo na hesabu zako za kisomi (iweke sawa hesabu za makaratasi) badala yako watakuwela kundi moja na wale inspiration speakers; wanahamasisha kilimo cha biashara mf. bustani kuwa unatumua milioni 1 ulivuna unapiga milioni 10. amini bure ekari 3 bila hatua uliyokwishapiga kuelekea wazo lako, hazitoshi kumshawishi mtu amwage pesa.

mimi ni miongoni mwa watanzania wagumu kumuamini msomi wa nchi hii kwa taaluma ya uchumi. maramia nimwamini mwanasiasa na ahadi zake maana huwa nimejindaa kisaikolojia kwa kitakachofuata, huwa wanaanguka lakini baada ya kujaribu na hakika hututia matumaini kuwa awamu ijayo watafanikisha. laiti maafisa ugani na bw/bi. kilimo wangekuwa lau na mashamba darasa ya lau rbo heka kutuwekea elimu zao kutoka makaratasi kuwa vitendo ingefaa kunibadili.


naungana na mchangiaji hapo juu.

sisi ambao hatukusoma/hatukubahatika kuajiriwa hakuna fursa ambazo hatujajaribu. kilimi, ufugaji, biashara, viwanda vidogo (vyerehani, mashine za, mbao na nafaka) we speak frankly from experience. ni msomi tu anatuchukulia poa kwa vile anatuzidi hesabu


hitimisho :
unda kundi la jamaa zako pengine school mates,members wa grp za whatsap, work mates mchangishane hata 500,000 au m1 kwa watu kama 10/20 mjenge credibility, hapo tutawapokea kirahisi hata kwa kutuuzia hisa (chonde tu zisije kuwa km za voda).


KILA LA KHERI!
100 Millions ukafungue mradi wa ufugaji wa nguruwe! This is a joke. Mkuu nguruwe wala hawaitaji nguvu kubwa kiasi hicho. Mbona ni rahisi sana, labda kwa sababu huko jamaa alipo ni mbali.

Pili mradi kama huo hauitaji kuwa na partners, unauendesha mwenyewe tu. Ngoja nikupe mfano mzuri kabisa.

1. Kwa kuanza kwa kuwa tayari ana utayari, anajenga banda la mbao/banzi. Liwe na urefu wa futi 10-12 kwenda juu. Akate vyumba vya kutosha kukaa nguruwe wa5 kila chumba. Hii maanake atajenga banda la bati 40. Unapauwa kwa upande mmoja. Yaani linamwaga maji upande m1.
Wastani hili lita gharimu kama 3 millions. Hapa utatumia nguzo na mbao au banzi.

Nguruwe ananunua 50 kwa wastani wa tshs 70-80k. Kazi imeisha. Anaanza kulisha anasubiri soko. Sasa ukiangalia hapo harama haiwezi kuzidi 15ml.
 
Nyongeza kidogo.

Mimi nipo mkoani ifakara, Morogoro. Ufugaji wa nguruwe kwa hapa ni rahisi kuliko sehemu yoyote nchini. Unapata pumba za Mpunga kwa bei ya kutupa. Maana hapa ndio wazalishaji wakubwa wa mpunga. Kg 70 ya pumba napata kwa shs 2500 hapo nishamlipa na mjazaji. Kwa nilivyo alwatan naweza kupata bure.

Mashudu ya alizeti yapo kwa wingi, Pumba za mahindi zipo kibao kwa kifupi ufugaji wa hapa ni rahisi. Ila changamoto zipo. Mimi sifanyi ufugaji wa kuzalisha, nafuga kuendeleza. Nanunua kwa kuchagua nguruwe wazuri ambao hawajadumaa.

Natengeneza chakula cha mwezi mzima kinanigharimu kama tsh 200k na kinatosha kulisha nguruwe 80-100 kwa mwezi. Ila pumba za mpunga zinazidi kwenye huo mchanganyiko.

Nachanganya pumba za mahindi, Mashudu ya alizeti, pumba za mpunga, chumvi, pig mix wakati mwingine na dagaa. Matengeneza gunia 30 zinatosha kulisha mwezi mzima. Nawalisha Ahsubuhi na jioni. Wanapewa majani kila baada ya siku tatu.

Ufugaji wangu ni kama kibubu. Nikiuza ndio nimevunja.
70kg kwa 2500/=???
Vp mashamba yakununua wanauzaje huko kwa ekari?
Upatikanaji wa maji ya ardhini ukoje?
 
70kg kwa 2500/=???
Vp mashamba yakununua wanauzaje huko kwa ekari?
Upatikanaji wa maji ya ardhini ukoje?
Mashamba kama ni nje kabisa ya mji ni 800000-100000 kwa heka. Mashambani kabisa unaweza kupata mashamba heka 10 kwa mpaka 3000000.

Maji ya ardhini yapo mengi. Kila nyumba hapa ina kisima cha kupampu. Wanyeji wanaita mdundiko. Kila mtu anajichimbia tu. Tena kwa gharama nafuu. 350000 unapata kisima chako.
 
Mkuu nakupa tahadhari, RUDIA RESEARCH YAKO MKUU. Alafu Nguruwe hawafugwi kando ya vyanzo vya maji hasa hawa wa large scale farms sasa hapo umejipanga vipi?

Anyway all the best
 
Nimefurahi sana kukutana na uzi huu na nina siku nyingi sijaingia JF.
Kwa upande wangu naweza kukujoin kwa kuwekeza kwenye teknolojia ya kuzalisha chakula cha mifugo hao kwa kupunguza gharama ya malisho zaidi ya 50%
Niwe wazi ni kwamba kwa sasa najishughulisha zaidi na ufundishaji wa teknolojia ya Hydroponics Fodder pamoja na kilimo cha Azolla. Kwa pamoja yote hayo ni kwa ajili ya kupunguza gharama za malisho ili kuongeza faida kwa mfugaji.
Kama utakuwa umenielewa (wewe mtoa mada) tunaweza kuwasiliana zaidi.
 
Mashamba kama ni nje kabisa ya mji ni 800000-100000 kwa heka. Mashambani kabisa unaweza kupata mashamba heka 10 kwa mpaka 3000000.

Maji ya ardhini yapo mengi. Kila nyumba hapa ina kisima cha kupampu. Wanyeji wanaita mdundiko. Kila mtu anajichimbia tu. Tena kwa gharama nafuu. 350000 unapata kisima chako.
Kama sijakupata hivi au ni typing error.umeandika laki8 mpaka laki 1.huku kwa ekari 10 kwa m3 ambayo ni sawa laki3 kwa kila ekari.
 
Nyongeza kidogo.

Mimi nipo mkoani ifakara, Morogoro. Ufugaji wa nguruwe kwa hapa ni rahisi kuliko sehemu yoyote nchini. Unapata pumba za Mpunga kwa bei ya kutupa. Maana hapa ndio wazalishaji wakubwa wa mpunga. Kg 70 ya pumba napata kwa shs 2500 hapo nishamlipa na mjazaji. Kwa nilivyo alwatan naweza kupata bure.

Mashudu ya alizeti yapo kwa wingi, Pumba za mahindi zipo kibao kwa kifupi ufugaji wa hapa ni rahisi. Ila changamoto zipo. Mimi sifanyi ufugaji wa kuzalisha, nafuga kuendeleza. Nanunua kwa kuchagua nguruwe wazuri ambao hawajadumaa.

Natengeneza chakula cha mwezi mzima kinanigharimu kama tsh 200k na kinatosha kulisha nguruwe 80-100 kwa mwezi. Ila pumba za mpunga zinazidi kwenye huo mchanganyiko.

Nachanganya pumba za mahindi, Mashudu ya alizeti, pumba za mpunga, chumvi, pig mix wakati mwingine na dagaa. Matengeneza gunia 30 zinatosha kulisha mwezi mzima. Nawalisha Ahsubuhi na jioni. Wanapewa majani kila baada ya siku tatu.

Ufugaji wangu ni kama kibubu. Nikiuza ndio nimevunja.

Hivi Ifakara ishakuwa Mkoa...??

Ila hongera kwa ufugaji usio na gharama Kama wa mijini hasa dar...kuku tu wanakutoa hela Hadi unaomba pooo..

By ze way vipi mafuriko huko??
 
Hivi Ifakara ishakuwa Mkoa...??

Ila hongera kwa ufugaji usio na gharama Kama wa mijini hasa dar...kuku tu wanakutoa hela Hadi unaomba pooo..

By ze way vipi mafuriko huko??
bado haijawa mkoa. Soma post yangu vizuri. Nimesema nipo ifakara morogoro. Kuhusu mafuriko Juzi kati ilikuwa balaaa.
 
Mashamba kama ni nje kabisa ya mji ni 800000-100000 kwa heka. Mashambani kabisa unaweza kupata mashamba heka 10 kwa mpaka 3000000.

Maji ya ardhini yapo mengi. Kila nyumba hapa ina kisima cha kupampu. Wanyeji wanaita mdundiko. Kila mtu anajichimbia tu. Tena kwa gharama nafuu. 350000 unapata kisima chako.

Bei za wapi hizo mlongo namimi nikanunue aisee.
 
Nyongeza kidogo.

Mimi nipo mkoani ifakara, Morogoro. Ufugaji wa nguruwe kwa hapa ni rahisi kuliko sehemu yoyote nchini. Unapata pumba za Mpunga kwa bei ya kutupa. Maana hapa ndio wazalishaji wakubwa wa mpunga. Kg 70 ya pumba napata kwa shs 2500 hapo nishamlipa na mjazaji. Kwa nilivyo alwatan naweza kupata bure.

Mashudu ya alizeti yapo kwa wingi, Pumba za mahindi zipo kibao kwa kifupi ufugaji wa hapa ni rahisi. Ila changamoto zipo. Mimi sifanyi ufugaji wa kuzalisha, nafuga kuendeleza. Nanunua kwa kuchagua nguruwe wazuri ambao hawajadumaa.

Natengeneza chakula cha mwezi mzima kinanigharimu kama tsh 200k na kinatosha kulisha nguruwe 80-100 kwa mwezi. Ila pumba za mpunga zinazidi kwenye huo mchanganyiko.

Nachanganya pumba za mahindi, Mashudu ya alizeti, pumba za mpunga, chumvi, pig mix wakati mwingine na dagaa. Matengeneza gunia 30 zinatosha kulisha mwezi mzima. Nawalisha Ahsubuhi na jioni. Wanapewa majani kila baada ya siku tatu.

Ufugaji wangu ni kama kibubu. Nikiuza ndio nimevunja.

🤔😀.Hao nguruwe unawapeleka sokoni wakiwa na umri gani?!
Wanakuwa na uzito gani wanapoenda sokoni!!?
 
Back
Top Bottom