Danpol
JF-Expert Member
- Aug 15, 2013
- 5,682
- 8,809
Ulifanikiwa kuanza mradi ?Hii thread ilifika mwisho?
Ulifanikiwa kuanza mradi ?Hii thread ilifika mwisho?
Yes, nimeanza phase one, nina nguruwe 4, nitawapandisha disemba mwishoniUlifanikiwa kuanza mradi ?
Magomeni Tanga na Zanzibar kuna mashoga wengi sana, na wale mashoga ni waislamu. unataka kusema na hao walianza kula kitimoto tangu wadogo? astagfirulah
hata mimi hapo nimezungumzia wengi sio wote.
Unatakiwa usome kwanza na kutafakari kabla hujajibu.
mimi sikutaka kuzunguka dunia nzima kutolea mifano ndo mana nimechukua sampo ya makazi ambayo yana waislamu wengi na mashoga wengi, dhumuni ni kukuonyesha kwamba hio dini hawali nguruwe ila mashoga ni wengi sana, hata uarabuni hawali nguruwe ila wanachokonoana sana matakoni.
unawazungumziaje waislamu hawa wanaochokonoana matakoni angali nyama ya nguruwe hawali?
na hao wote uliowataja wanakula kitimoto?
kwahio cha msingi unaweza ukala kitimoto na usiwe shoga na unaweza usile kitimoto na ukawa shoga?
hapo nimekuelewa chief tupo pamoja.
We jamaa mimi nilikutumia PM ina miezi zaidi ya minne hata hukujibu inaonekana hauko serious.Kufuatia maoni ya wadau waliosoma uzi huu imenipasa nitoe japo a concept note.
Kiufupi lengo kuu la mradi ni Kuanzisha ufugaji wa Nguruwe kibiashara - Commercial Piggery Project (as opposed to traditional/subsistence Piggery Project). Features za commercial Piggery project include
1. Profitable Business
2. Energy-saving technology
3. Ecologically clean production
4. Humane attitude to pigs
Nimechagua kufuga Nguruwe badala ya wanyama wengine Kwa sababu zifuatazo
1. Nguruwe ana relatively low feed conversion ratio (FCR) ambayo ni nzuri mana inaelezea ufanisi Mkubwa alionao wa kuzalisha nyama toka Kwenye chakula ana chokula. Yaani anatumia chakula kidogo kuzalisha Kilo moja ya nyama.
2. Nguruwe wanakua haraka (Wana high growth rate). Nguruwe aliyetunzwa vzr anaweza kuwa na kilo Kati ya 100 -110 ndani ya miezi 6.
3. Wanabeba mimba Kwa muda mfupi Sana i.e. three months, three weeks and three days= in total 114 days. Na wanaweza kuzaa Kwa wastani watoto 10-14 Kwa mzao. Hii inategemea ubora wa mbegu, chakula na afya yao. Nguruwe pia anaweza kuzaa mara 2 Kwa mwaka.
4. Nyama yake ni White meat, hivyo ni nzuri Kwa afya na wateja wengi wanaipenda.
5. Kwa Tanzania wafugaji wa kibiashara ni wachache na kimsingi wameshindwa kumeet market demand. Hivyo Kuna soko kubwa Sana nchini ambalo Kwa sasa linalazimika kuagiza nyama hiyo nje ya nchi mana hatujaweza bado zalisha Bidhaa wanzozihitaji.
6. Wazalishaji karibu wote wamejikita katika kuuza raw pork meat/live animals (nguruwe mzima mzima). Hivyo kuna uhaba Mkubwa Sana Sana wa Bidhaa za Nguruwe zilizoongezewa thamani kama specialized and packed pork cuts, Bacon, Smoked pork meat, pork sausages etc.
Kwa kutambua haya. Ndio nikawiwa kutafuta wenzangu wanaopenda kuungana nami ili tuchangamkie fursa hii.
Gharama za ufugaji wa Nguruwe.
Kwa ujimla gharama zina tofautiana Sana kulingana na namna unavyoendesha ufugaji wako. Gharama kubwa ktk ufugaji wa Nguruwe, ukiachia Ujenzi wa Banda la kisasa, zipo kwenye chakula. Japo kuna wataalamu wanaotoa gharama za makadirio, ukweli ni kwamba si rahisi kuwa realistic Kwenye makadirio hayo.
Chakula:
1) Nguruwe ana nyonya Kwa muda wa week 4 (siku 28). Baada ya hapo anapaswa kutengwa na mama yake na kuwekwa Kwenye Banda la kukulia ili kumpa mama yake muda wa kuzalisha joto ili apandwe tena. Nguruwe no Omnivore (hula nyama na majani, nafaka/mbegu) hivyo inapaswa umlishe chakula chenye mchanganyo na virutubisho vyote na ikifaa iwe katika form ya Pellets.
Baada ya kunyonya hula chakula cha uzito mbalimbali kulingana na uzito wao mfano.
2) Nguruwe mwenye 10-17kg anapaswa kula 0.8 kg Kwa siku
3) Nguruwe mwenye 18-29Kg anapaswa Kula 1kg Kwa siku
4) Nguruwe mwenye 30-40kg anapaswa Kula 1.5kg Kwa siku.
5) Nguruwe mwenye 40-60 kg anapaswa Kula 2kg Kwa siku.
6) Nguruwe mwenye 61-80kg anapaswa Kula 2.5kg Kwa siku.
7) Nguruwe mwenye 81-100kg anapaswa Kula 3kg Kwa siku.
8) Nguwure zaidi ya 100kg na mwenye mimba anapaswa Kula 6 kg.
Inashauriwa Nguruwe auzwe chini ya 120kg maana baada ya bado anakuwa na high feed conversion ratio. Anatumia chakula kingi kutengeneza kilo moja ya nyama hivyo ni hasara Kwa mfugaji.
Naweza kudadavua zaidi Kwa interested and serious partners baadaye.
Bei ya Mbegu (Breeding Stock)
Bei ya Nguruwe wa mbegu pia inategemea unahitaji mbegu aina gani, wa ukubwa gani na unamtoa wapi. Kuna aliyetaka niuzia wa mwezi mmoja Kwa 100,000 na wa miezi sita kwa 600,000 Dar Es Salaam. Hivyo bei zina range hapo.
Soko la Nguruwe.
Soko ni kubwa Sana kuanzia soko la wateja wa kawaida hadi mahotelini. Wakati kilo 1 ya raw meat inauzwa Kwa TZS 8000 Kwa bei ya rejareja, Kwenye mahoteli ambako wananunua Bidhaa zilizoongezewa dhamani, kilo moja ya Bidhaa hiyo huuzwa hadi TZS 30,000.
Kwenye ufugaji ninaotaka kuufanya Mimi target yangu ni Soko la mahotelini.
Nini kipo tayari Hadi sasa
Ninaye mtaalam wa kuongezea thamani yaani kufanya smoking, kufanya hizo pork cuts, kutengeneza bacon n.k.
Nina shamba zaidi ya heka 3 lipo mita 600 kando ya mto Ruvu, Mlandizi na umeme haupo mbali. Hivyo suala la Maji na umeme Kwenye shamba Hilo ni rahisi.
Nina kijana wa kazi mmoja na Mimi mwenyewe ntakuwa naishi hapo hapo Shambani muda mwingi.
Nina wataalamu wa magonjwa ya Nguruwe wawili ambao wameshaonesha interest ya kushirikiana nami katika hii project.
Vinavyokosekana Hadi sasa.
Mtaji Kwa maana ya Fedha za kujenga Banda la kisasa la kuaccomodate breeding stock ya Nguruwe angalau 50 na Banda la kutunzia watoto, kujenga processing unit/house, kuweka uzio eneo la banda, kununua chakula na breeding stock 50 pigs, kutengenezea cold room/chiller, smoker, kununua machine za cutting, vacuum na vifungashio, kujisajiri TFDA na TBS.
Kama Kuna maswali zaidi nitaendelea Kujibu.
Hutujui wabongo eh!Vipi huu mradi umefikia wapi
Naona kahamia kwenye mchanga... Bongo nyosoHutujui wabongo eh!
😀😀! Kuna mtu naye ananihojigi balaa kuhusu mishe zangu. Bas akuambie kesho nategemea kutembelea walau mgodi mmoja wapiii...Sana San kila siku unaombwa picha za dhahabu😆😆! Utadhani mtafiti ..hatupo serious kbs kbs yaan
Very sorry jamaa yangu. Nlitumiwa texts nyingi Kwa bahati mbaya yako sikuiona na kuweza kuijibu timely. Niwie Radhi.We jamaa mimi nilikutumia PM ina miezi zaidi ya minne hata hukujibu inaonekana hauko serious.
Mradi hatukuweza kutake-off ingawa niliweza kukutana na wadau wachache kujadiliana. Niliweza kuandaa andiko la mradi ila hatukuweza kuendelea zaidi ya hapo.Vipi huu mradi umefikia wapi
Hahaha wakaa kwa shemeji hao.! Kuna mtu naye ananihojigi balaa kuhusu mishe zangu. Bas akuambie kesho nategemea kutembelea walau mgodi mmoja wapiii...Sana San kila siku unaombwa picha za dhahabu! Utadhani mtafiti ..hatupo serious kbs kbs yaan
Pole sanaMradi hatukuweza kutake-off ingawa niliweza kukutana na wadau wachache kujadiliana. Niliweza kuandaa andiko la mradi ila hatukuweza kuendelea zaidi ya hapo.
Ahsante! But natafuta mtaji from my own sources Ili siku moja ndoto yangu itimie. Tuzidi kuombeana na kuwasiliana.Pole sana
Pamoja Sana mkuuAhsante! But natafuta mtaji from my own sources Ili siku moja ndoto yangu itimie. Tuzidi kuombeana na kuwasiliana.
😆😆🤸🤸😀! Blah blah Sana watz...dahHahaha wakaa kwa shemeji hao.
Ukute anakuuliza hayo maswali amenyoosha zake miguu kwenye sofa huku mkono mmoja umeshika rimoti ya DStv na pembeni juice ya embe anakuchora tu.
Mitandaoni Raha Sana.