Natafuta mtu wa Kuniloga.

Kama huna cha kujibu bora ukae kimya. Wanasema bora kukaa kimya nakuonekana unajua kuliko kufungua mdomo na kuthiirishia umma ulivyo mtupu. Kila nacho post ndio jibu hilo hilo unatoa. Inaonekana wewe mjane na unaendeshwa kwa hisia zaidi ya reasoning. Kuna tiba nitakuponya kisaikolojia kwa vile kila jamii ina watu kama nyie na mko ili sisi tujione ni kiasi gani tumebarikiwa na Mungu.

Uliniita mwenyewe nichangie, sasa nachangia unataka kunifunga mdomo. Lipi nililoandika ambalo hukulipenda?
 
Tena hao ndio hawalogi kabisa sema wanajua kumtuliza mwanaume kumpa..... kisawasawa refer to my last thread... kuwa watoto wa imani ya.... ni noma. Sasa mwanaume anakuwa zuzu akiambiwa mguu pande na mguu sawa anaenda. So hakuna uchawi
Ngoja nikamwambie bibi yangu akushushe busha la kilogram 8.
 
mtafute dokta manyaunyau...nenda kivukoni kuna dala dala zake zinapiga ruti ya goms-kivukoni, chukua namba zake za simu, mtwangie....nenda kapate ushauri wake kisha tuletee feedback!
 
Lete majina yako yote matatu hapa jamvin nikuonyeshe kazii ndani ya msaa 24! ( first, middle & surname)
 
Kutokuamini kwako hakuna uchawi hakuwezi kufanya kusiwepo uchawi. Endelea kuamini hakuna uchawi (kwakua hauja fanyiwa vitendo vya kichawi) kama ninavyo amini mimi hakuna Ukimwi (kwakua bado sijaathirika)
 
  • Thanks
Reactions: Paw
Wakuu,

Nina miaka 4 sasa nafanya utafiti kuhusu kuwepo kwa uchawi sijapata kujiridhisha kihalisia kuwepo kwa ushirikina.Nimetembelea maeneo yote yanayosemekana ni maarufu kwa ushirikina kama Tanga, Sumbawanga, Pemba na Bagamoyo. Huko pemba nimefika maeneo ya wete kuna kamsitu wanasema ndio hatari kwa wachawi kukaa na kufanya matambiko kuna makaburi ya zamani sana walisema tukifukua tutakufa kwa vile tutachokoza 'wazee' tumefanya excavation vizuri tukakuta artifacts na masufuria ma hirizi na mavitambaa mekundu na meusi na manyoa, ni mwaka sasa na mpaka sasa hata mafuta hakuna aliye pata kwenye team yetu. Tulilala hapo hapo makaburini kwa kutumia tent hata mbu hakutun'ata.

Sasa swali ni kwamba mtu anasema ooh nimelogwa na kukimbilia kwa hawa watumishi fake wa Mungu na kusema wamepona, wamenpona nini? Mimi nimeomba wazee waniloge wakasema wameniloga sitozaa kabisa kwa sasa na miaka 28 na watoto 6 na wana afya nzuri na nimepima DNA ni wa kwangu.

Kama kuna mtu amelogwa au anaweza kuniloga atoe fact hapa.
Mzizi mkavu Asprin Bujibuji Nyani Ngabu faiza Fox Yericko Nyerere

Mkuu hata usipate taabu ukiwaomba tu wanakuonesha we usiombe ulogwe ukadhurika omba uoneshwe kama uchawi upo.Mfano wa ukweli kuna Padri moja ktkt ya mahubiri alisema hakuna uchawi hukohuko Sumbawanga,alipomaliza tu ibada kwenye ile nyumba anayoishi akasikia sauti hodi hodi nauza mayai padre kutoka nje kinachoongea ni Chura na kabeba kapu la mayai.Toka siku hiyo alishika adabu na akakiri uchawi upo! Daima kuna mawili Mungu na Shetani lakini Mungu ndiye mkuu.Rasilimali zote za uchawi zinatoka kwa shetani.Mazuri yote Kwa Mungu.Amini usiamini haya manbo yapo usikute hapo ulipo ushalogwa ndo maana huelewi as uchawi upo mahali pote since shetani yupo mahali pote!
 
Mkuu ulisharogwa siku nyingi, kwa umri wako na timu ya watoto ulionao!


Sent from my BlackBerry 8900 using JamiiForums
Mkuu cha umri na idadi ya watoto hapo sishangai nina jamaa yangu alipokuwa na umri wa miaka 26 tayari alikuwa na watoto saba............hakuna housegirl wa kwao alietoka salama achilia mbali videm vya mtaani....so kwa idadi ya wtoto wa mshkaji na umri wake wala sishangai.kikubwa tayari ameshalogwa na ye hajijui kuwa keshapigwa
 
Uchawi ni siri, ili tukurithishe/shirikishe lazima utoe sadaka ya watoto 2 kwa kuwatwanga kwenye kinu na kunywa rojo yao, uko tayari?
 
hilo la watoto naomba mliache kwa sasa. Siko kuelezea maisha yangu binafsi naulizia uchawi. Kuna member wanaonijua uhalisia wangu na hao watoto kwa mfano bujibuji na @aspirin. Nikielezea nilivyopata hawa watoto itakuwa thread maisha yangu ni muujiza tosha kaka.

ni kipengele cha uchawi.....ushapata jibu !!!
 
Umenikwaza kwa neno boja tu ulilotumia la kejeli kwamba "Watumishi feki wa Mungu" Kuwa makini na kauli zako
 
jaribu kufanya provocation kama vile kuchukua mke wa mtu handeni kwa msisi. kapeleleze jamaa walio mabingwa wa uchawi wa kunasa wezi wa wake za watu halafu utest kwa wake zao

mi nakumbuka Tanga nimekaa kuna mzee alikua anaogopwa mtaani kisa ana wanyama(majini). alikuwa anafuga mbuzi amewapa majina kama watu. hao mbuzi wanaishi kiholela na wakila mimea yako we mwambie tu kuliko sijui kuwapa sumu au kuwafanyizia wezi wakiiba tu anatoa tangazo msikitini kwenye vipaza sauti kama warning. baadaye anatoa la mwisho kabla ya kwenda kwenye action. vijana wa vijiweni walikua wanakufa live kabisa unakuta mtaani msiba wa vijana watatu wanne ghafla siku moja. uchawi upo ila inategema na imani yako. siri moja wapo ya kunaswa na uchawi ni kuwa na nguvu za giza za kujihami kwenye mwili wako. ukifanya hivyo tu ujue jamaa akikurushia combora kunakuwa na attractions ambazo wewe mwenyewe ndo umeziruhusu.

wachawi wanaangalia provacation na some cults link to the victim
 
nenda muheza kisha chukua mke wa mtu,uone jinsi utakavyokojoa dagaa tena dagaa mwenyewe akiwa ametanguliza mkia.
 
Lete majina yako yote matatu hapa jamvin nikuonyeshe kazii ndani ya msaa 24! ( first, middle & surname)

Frank Joram Mwanga babu yangu anaitwa Mvungomali eneo nalotokea ni Rombo mkuu Moshi
 
Umenikwaza kwa neno boja tu ulilotumia la kejeli kwamba "Watumishi feki wa Mungu" Kuwa makini na kauli zako

Wapowaliokuwa fake hilo tutalianzishia thread na nitakuja na evidence, sio wote waniitao bwana bwana wataingia ufalme wa Mungu, pia siku za mwisho zikifika utasikia niko huku niko kule msiwasikilize......
 
NGULI Watu Wanavuta Bangi ila Hii Yako Nadhani ni MCHANGANYIKO wa Kitu cha Kwetu TARIME ( MARA ) na Kwao LONGIDO ( ARUSHA ).
 
Last edited by a moderator:
Nenda sehemu moja karibu na bulyanhulu kuna kijiji cha Ilogi ukajisifu hivyo utaona cha mtemakuni maana utaamkia vichakani asubuhi pu....m..b... zinaonekana
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom