Natafuta mtu wa Kuniloga.

Wakuu,

Nina miaka 4 sasa nafanya utafiti kuhusu kuwepo kwa uchawi sijapata kujiridhisha kihalisia kuwepo kwa ushirikina.
Uchawi ni nini katika utafiti wako/wenu? Ushirikina na uchawi ni kitu kimoja? Mazingaombwe ni nini? Hii ni muhimu sana kwa maana si rahisi kuweza kutafuta kitu ambacho hukifahamu.
 
Wakuu,

Nina miaka 4 sasa nafanya utafiti kuhusu kuwepo kwa uchawi sijapata kujiridhisha kihalisia kuwepo kwa ushirikina.Nimetembelea maeneo yote yanayosemekana ni maarufu kwa ushirikina kama Tanga, Sumbawanga, Pemba na Bagamoyo. Huko pemba nimefika maeneo ya wete kuna kamsitu wanasema ndio hatari kwa wachawi kukaa na kufanya matambiko kuna makaburi ya zamani sana walisema tukifukua tutakufa kwa vile tutachokoza 'wazee' tumefanya excavation vizuri tukakuta artifacts na masufuria ma hirizi na mavitambaa mekundu na meusi na manyoa, ni mwaka sasa na mpaka sasa hata mafuta hakuna aliye pata kwenye team yetu. Tulilala hapo hapo makaburini kwa kutumia tent hata mbu hakutun'ata.

Sasa swali ni kwamba mtu anasema ooh nimelogwa na kukimbilia kwa hawa watumishi fake wa Mungu na kusema wamepona, wamenpona nini? Mimi nimeomba wazee waniloge wakasema wameniloga sitozaa kabisa kwa sasa na miaka 28 na watoto 6 na wana afya nzuri na nimepima DNA ni wa kwangu.

Kama kuna mtu amelogwa au anaweza kuniloga atoe fact hapa.
Mzizi mkavu Asprin Bujibuji Nyani Ngabu faiza Fox Yericko Nyerere

Wamekudharau wala hawatakudhuru,ukitaka sema unataka kununua uchawi tena tangaza dau kubwa uone watakavyokuletea kila mmoja akijisifu wake ndiyo mkali tena watakujaribia kama siyo kwako kwa mwenzio unajua hii ni secret society fulani hivi sawa na freemason au haloween hawapendi kujionesha pasipo maslahi. hata biblia inatambua kuwa uchawi upo ila unadhbitiwa kwa jina la Yesu,wenzetu wengine kwao ni sehemu ya dini.unaweza kuletewa hata kwa njia ya meseji au hata kwa mawasiliano ya simu ila endelea na utafiti wako iko siku utauona
 
Kama huna cha kujibu bora
ukae kimya. Wanasema bora kukaa kimya nakuonekana unajua kuliko kufungua
mdomo na kuthiirishia umma ulivyo mtupu. Kila nacho post ndio jibu hilo
hilo unatoa. Inaonekana wewe mjane na unaendeshwa kwa hisia zaidi ya
reasoning. Kuna tiba nitakuponya kisaikolojia kwa vile kila jamii ina
watu kama nyie na mko ili sisi tujione ni kiasi gani tumebarikiwa na
Mungu.
Kwa post hii,kweli umerogwa!
 
Mbona tayari usharogwa na aliyekuloga humjui,

Matokeo ya kulogwa huko ni haya unayoyaongea hapa na juzi ulisema tukukutanoshe na mwenye jamhuri kwakuwa unafanana nae tu, kibaya zaidi mchawi aliyekuloga kakupiga jabulani ya kutosha yani una miaka 28 na tayari una watoto 6, ukifika miaka 40 sijui utakuwa na sakosi ya aina gani.

Huo ndio uchawi, hakuna kingine
 
Hilo la watoto naomba mliache kwa sasa. Siko kuelezea maisha yangu binafsi naulizia uchawi. Kuna member wanaonijua uhalisia wangu na hao watoto kwa mfano Bujibuji na @aspirin. Nikielezea nilivyopata hawa watoto itakuwa thread maisha yangu ni muujiza tosha kaka.
unaamini uwepo wa miujiza ,lakini huamini uwepo wa uchawi....majanga

Kama huna cha kujibu bora ukae kimya. Wanasema bora kukaa kimya nakuonekana unajua kuliko kufungua mdomo na kuthiirishia umma ulivyo mtupu. Kila nacho post ndio jibu hilo hilo unatoa. Inaonekana wewe mjane na unaendeshwa kwa hisia zaidi ya reasoning. Kuna tiba nitakuponya kisaikolojia kwa vile kila jamii ina watu kama nyie na mko ili sisi tujione ni kiasi gani tumebarikiwa na Mungu.
unaamini mungu yuou na anabariki lakini huamini kama kuna uchawi ambaye huyo anayekubariki anatambua na kuukiri upo...majanga

Wakuu,

Nina miaka 4 sasa nafanya utafiti kuhusu kuwepo kwa uchawi sijapata kujiridhisha kihalisia kuwepo kwa ushirikina.
Kama kuna mtu amelogwa au anaweza kuniloga atoe fact hapa.
kazi ipo....
 
Wamekudharau wala hawatakudhuru,ukitaka sema unataka kununua uchawi tena tangaza dau kubwa uone watakavyokuletea kila mmoja akijisifu wake ndiyo mkali tena watakujaribia kama siyo kwako kwa mwenzio unajua hii ni secret society fulani hivi sawa na freemason au haloween hawapendi kujionesha pasipo maslahi. hata biblia inatambua kuwa uchawi upo ila unadhbitiwa kwa jina la Yesu,wenzetu wengine kwao ni sehemu ya dini.unaweza kuletewa hata kwa njia ya meseji au hata kwa mawasiliano ya simu ila endelea na utafiti wako iko siku utauona

Naamini NGULI atakuja kukujibu ila naomba kuchangia tu kuwa huyo padri niliyemzungumzia hapo juu, alikwenda kwa waganga wengi(majina aliyataja) wengine unawafahamu. Hata yule mchawi alitaka kuomba kibari cha kuruka na ungo alionananaye, na kote alikokwenda, alikwenda eidha kama mteja wa uchawi au kama mgojwa lakini aliishia kusema yote ni sanaa na mazingaombwe.
 
Mbona tayari usharogwa na aliyekuloga humjui,

Matokeo ya kulogwa huko ni haya unayoyaongea hapa na juzi ulisema tukukutanoshe na mwenye jamhuri kwakuwa unafanana nae tu, kibaya zaidi mchawi aliyekuloga kakupiga jabulani ya kutosha yani una miaka 28 na tayari una watoto 6, ukifika miaka 40 sijui utakuwa na sakosi ya aina gani.

Huo ndio uchawi, hakuna kingine

Sikutemea hii judgement kutoka kwako. i thought your thinking capacity is beyond this.....
 
unaamini uwepo wa miujiza ,lakini huamini uwepo wa uchawi....majanga


unaamini mungu yuou na anabariki lakini huamini kama kuna uchawi ambaye huyo anayekubariki anatambua na kuukiri upo...majanga


kazi ipo....

Hapo kuna mchanganyiko. Naungana na wewe, ume-spot kitu cha msingi.
Ngoja tumsubiri NGULI mwenyewe.
 
Mi naona ungeanza kujitafiti kwamba kwa nini katika umri mdogo huo una watoto 6? Nadhani hapo ndo umelogwa kwa vile umeshindwa kujitambua.
 
Naomba unipe jina lako na la mama yako liwe kamili.
Halafu niambie unataka nikuroge uweje
1.Ufe kabisa?
2. Uwe kichaa?
3.Uwe fukara maisha yote?
4.Uwe shoga?
 
Sitosahau siku moja nikiwa mkoa flani ambao sitoweza kutaja jina nikiwa nimerudi toka kwenye mihangaiko yangu usiku nikalala usiku nilila na bukta ndani nikiwa na boxer nilistuka usiku wa saa tisa na kujikuta nipo uchi chini ya uvungu nilinyanyuka nakuangalia mlango umefungwa vilevile alafu bado unaniambia uchawi haupo hapana mkuu mimi nakataa.
 
Wakuu,

kwa sasa na miaka 28 na watoto 6 na wana afya nzuri na nimepima DNA ni wa kwangu.

hongera bro...
11292013_B_HIV_Frontlin_6-300.jpg
 
Nitajitolea kufanya kazi yako; nitahitaji vitu vifuatavyo ili kufanikisha zoezi langu.

1. Nitahitaji kupata Tambiko (Zindiko) lako la ukoo, kama hulijui basi nitatumia utaratibu wa kukupisha huku kiganja chako
cha mkono wa kulia kikiwa kimekandamiza pembe la kiapo.

2. Nitahitaji kuchukua moja ya vifuatavyo: Unyayo, Unyewe wa utosini, kucha au kope

Hivi vitu ndiyo vinatakiwa kufanikisha zoezi la kukugeuza uwe ndondocha!!

Vitu vingine ambavyo wewe havikuhusu - nitahitaji kupata:

1. Sanda iliyotumika kumzikia mtoto mchanga.
2. Kipande cha mbao kilichongolewa kutoka kwenye kitanda kinachotumika kubebea maiti
3. Bundi mweusi - Hasa kama mizimu yako ni mikorofi kukuachia
4. Maji ya baharini kama utaamua kuishi baharini au maji ya mtoni kama pia utapenda kuishi huko - hapa ni chaguo lako

Note: Huu uchawi ni wa Bara (Ndagu)- Pwani wao wanatumia Majini.

Upo tayari.....
 

Similar Discussions

10 Reactions
Reply
Back
Top Bottom