Natafuta mtu wa Kuniloga.

NGULI

JF-Expert Member
Mar 31, 2008
4,803
637
Wakuu,

Nina miaka 4 sasa nafanya utafiti kuhusu kuwepo kwa uchawi sijapata kujiridhisha kihalisia kuwepo kwa ushirikina.Nimetembelea maeneo yote yanayosemekana ni maarufu kwa ushirikina kama Tanga, Sumbawanga, Pemba na Bagamoyo. Huko pemba nimefika maeneo ya wete kuna kamsitu wanasema ndio hatari kwa wachawi kukaa na kufanya matambiko kuna makaburi ya zamani sana walisema tukifukua tutakufa kwa vile tutachokoza 'wazee' tumefanya excavation vizuri tukakuta artifacts na masufuria ma hirizi na mavitambaa mekundu na meusi na manyoa, ni mwaka sasa na mpaka sasa hata mafuta hakuna aliye pata kwenye team yetu. Tulilala hapo hapo makaburini kwa kutumia tent hata mbu hakutun'ata.

Sasa swali ni kwamba mtu anasema ooh nimelogwa na kukimbilia kwa hawa watumishi fake wa Mungu na kusema wamepona, wamenpona nini? Mimi nimeomba wazee waniloge wakasema wameniloga sitozaa kabisa kwa sasa na miaka 28 na watoto 6 na wana afya nzuri na nimepima DNA ni wa kwangu.

Kama kuna mtu amelogwa au anaweza kuniloga atoe fact hapa.
Mzizi mkavu Asprin Bujibuji Nyani Ngabu faiza Fox Yericko Nyerere

Kuamini au kutoamini kulogwa ndiyo msingi wa kuweza kulogwa au kutoweza kulogwa.

Ni nguvu ya kuamini au kutoamni inayowezesha hali yeyote, tukio au mazingira unayopitia maishani
.
Matokea yatategemea kama unaamini kuwa unaweza kulogwa au hapana.

Uchawi ni matokeo ya nguvu ya imani. Huwa unawashangaza watu kwa kutojua nguvu ya imani.

Imani hufanya kazi kama msumeno. Kama unaamini kuwa kuwa unaweza kulogwa na ukalogeka ni sawa utalogeka vizuri sana lakini kama una amini uwezi kulogeka ni sawa pia uwezi kulogeka.

Unapoamini kuwa hauwezi kulogeka alaf ukaingia shaka kuwa unaweza kulogeka utalogeka vizuri tena mchana kweupe. Matokeoyakulogwa au kutologwa lazima yaumbwe na imani, hakuna kinyume na hapo.

Wazo lakulogwa linakuwepo/linakuja,halafu inategemea nini kiko kwenye imani zako. Mfano; unaposema sala zako hazijibiwi inaweza kuwa ni suala la kukinzana kwa kile unachoamini kwenye mawazo ya kina na unachotaka kiwe kwenye mawzo yako ya kawaida au imani haikuwa imara. Ukiwa na wazo lakulogwa na kulogeka, wazo hilo huzaa hisia, ambazo husema nini kitatokea. Hisia zilizotengenezwa nyuma zaweza kuharibu nia au lengo la leo.


Baada ya kutoa hizo dondoo naona sasa nielezee kidogo kuhusu hicho kinaitwa uchawi. Hakuna ajuaye uchawi ulianza lini. Lakini, katika kujiuliza maswali binadamu aligundua nguvu zenye kumzunguka.
Lakini, miaka mingi kabla ya Yesu kuja watu walianza kutambua nguvu nyingi kamauchawi,zenye kuweza kudhuru.

Baadaye uchawi ulianza kutumiwa kamakisingizio, ambapomatajiri walituhumiwana kuhukumiwa, kwamba, ni wachawi. Kijicho na uadui mwingine vilitekekelezwa kupitia uchawi. Walioouwawa zaidi hasa ulaya na Marekani walikuwa wanawake (asilimia 90). Kisa, Kanisa liliamini Ibilisi anaweza kuwashawishi kirahisi zaidi wanawake kupitia uchawi.

Hivi sasa wanaokubali kuwepo kwa uchawi wanaugawa katika makundi mawili-Mweupe na Mweusi.

Nadharia kuhusu uchawi Mweupe na Mweusi

-Ni kwamba uchawi mweupe au mweusi, wote ni uchawi bali ule mweusi ndiyo wenye lengo la kudhuru. Hata dini zinapozungumzia uchawi zinazungumzia huu mweusi.

-Wengine wanaamini kwamba, uchawi unakuwa uchawi wenye madhara ( mweusi) kama tu kuna vitu kama nywele, damu, au nguo za anayeunuiziwa zinazotumika katika kufanya hivyo.

-Wengine wanasema hakuna uhusiano kati ya uchawi mweusi na mweupe kwani kila mmoja unatumia njia na mbinu zake kufanya kazi. Wengine wanasema uchawi mweupe na mweusi ni sawa, ingawa matokeo ndiyo yanayotofautiana. Kama ni manuizi ni yaleyale, bali nani analengwa na kwa lengo gani, ndicho kitaleta matokeo, ambayo yatakua tofauti.

Sheria/amri kuu za uchawi.

Mchawi yeyote anayejua kwamba, analoga anajua kuhusu sheria hizi, hata kama hajui kuwa ni sheria au hata kama hatazijua kwa njia ya moja kwa moja.

1.Sheria ya uzao wa utatu Hii ina maana tutavuna tulichopanda. Tunachopanda kitaota na kutupa mazao mara tatu zaidi. Kama ni mazao ya maumivu, umasikini, utaturudia mara tatu. Watu wa Wicca wanatishwa sana na kanuni hii.

2.The wiccan rede Mchawi anahusiwa kufanya chochote kupitia nguvu za uchawi, mradi tu hajiumizi mwenyewe wala kumuumiza mwingine. Kwa wale wa wicca, hili wanalifuata sana pia.

3.ULOGAJI:kuna matumizi ya nguvu nyingi. Mawazo ndiyo chanzo kikuu. Ile nia ya kudhuru. Laana:Hapa kuna aina kadhaa kama vile gypsy
frown.gif
kunuiza:mfano; utakua mtu wa kutangatanga kwenye uso wa dunia milele, hutalala mara mbili kwenye kitanda kimoja, hutakunywa maji mara mbili toka kisima kimoja na hutavuta mto huohuo zaidi ya mara mbili kwa mwaka).

-Siyo kila neno au maneno yanaweza kuwa na nguvu ya kuathiri. Kama ingekuwa hivyo, wengi tungeshakufa ua kuumia kupindukia. Utaalamu wa maneno ni muhimu pia, kwani unaweza kuwa unampa mtu baraka badala ya kumloga.

-Maneno yasiyo maalumu sana huleta tu mikosi na yale maalumu huweza kudhuru afya au kipato.

Ishara
; Mtu anachukua hata toi, analivisha nywele za anayetaka kumdhuru au kipande cha nguo yake ama damu yake. Halafu mchawi hutumia pini kumchoma huu mdoli akiwa ameweka uzingativu kiakili kwa anayemloga. Hii hutumika sana kwenye uchawi wa voodoo wa Carbbean.

Kunuia: kunakuwa na seti maalumu ya aya, kanuni, kitendo au aya na kitendo. Mchawi hunuizia kwa aya au aya na kitendo akimnuia mtu. -Anaweza hata kwenda kwa mtu akafanya kitu mlangoni mwa nyumba yake. Mfano, mfano punje za mchele na sarafu akazitupa mlangoni mwa mtu kwa kunuizaa kwamba asipate kipato…alafu….!!!! -Kwa mfano, Oborojino wa Australia wanaamini kwamba, ukimnyooshea mtu mfupa wa kangaroo na kunuiza jambo baya, anaweza kudhurika. -Kaburi la Farao Tutankhamen wa Misri lina historia hii. Ni aya ya zamani ambayo ilisemwa na Mfalme huyo na kubandikwa nje ya kaburi hilo. -Mrusi Rasputin alitamka maneno Fulani wakati akikata roho dhidi ya Utawala wa Kifalme wa Urusi enzi zake, kufuatia kupigwa kwake risasi na kuasiwa na mtoto wa Mfalme. …..!!!! …
 
Tafuta mwanamke wa uswahilini, muonyeshe kama una gari nyumba na mali. Anzisha mahusiano

kisha utakuja kusema mwenyewe kama kurogwa kuko

Tena hao ndio hawalogi kabisa sema wanajua kumtuliza mwanaume kumpa..... kisawasawa refer to my last thread... kuwa watoto wa imani ya.... ni noma. Sasa mwanaume anakuwa zuzu akiambiwa mguu pande na mguu sawa anaenda. So hakuna uchawi
 
Okay, fanya jaribio la mwisho kabisa. Nenda Sumbawanga, ulizia wale wazee wenye sifa ya kuwa ni walozi wa ukweli halafu wafanyie moja kati ya haya:-

i. Tembea na mwanae halafu umpe mimba kisha ukimbie, au
ii. Kawatukane, uone kama watakupeleka polisi, wasipokupeleka polisi, subiri majibu
iii. Au ukawaombe tu wakuroge.
 
wakuu,

nina miaka 4 sasa nafanya utafiti kuhusu kuwepo kwa uchawi sijapata kujiridhisha kihalisia kuwepo kwa ushirikina.nimetembelea maeneo yote yanayosemekana ni maarufu kwa ushirikina kama tanga, sumbawanga, pemba na bagamoyo. Huko pemba nimefika maeneo ya wete kuna kamsitu wanasema ndio hatari kwa wachawi kukaa na kufanya matambiko kuna makaburi ya zamani sana walisema tukifukua tutakufa kwa vile tutachokoza 'wazee' tumefanya excavation vizuri tukakuta artifacts na masufuria ma hirizi na mavitambaa mekundu na meusi na manyoa, ni mwaka sasa na mpaka sasa hata mafuta hakuna aliye pata kwenye team yetu. Tulilala hapo hapo makaburini kwa kutumia tent hata mbu hakutun'ata.

Sasa swali ni kwamba mtu anasema ooh nimelogwa na kukimbilia kwa hawa watumishi fake wa mungu na kusema wamepona, wamenpona nini? Mimi nimeomba wazee waniloge wakasema wameniloga sitozaa kabisa kwa sasa na miaka 28 na watoto 6 na wana afya nzuri na nimepima dna ni wa kwangu.

Kama kuna mtu amelogwa au anaweza kuniloga atoe fact hapa.
mzizi mkavu asprin bujibuji nyani ngabu faiza fox yericko nyerere

kwenye blue hapo ndio umenifanya nianze kutilia mashaka uhalisia wa post yako.najua inawezekana lakini haileti mantiki kwa ''mtafiti'' kama wewe..
 
NGULI, umenikumbusha mbali sasa, umenikumbusha ule mwembe mkubwa ambao ulikuwa unageuka kuwa mamba.
Pia unanikumbusha yale maji taka yaliyokuwa yakikutwa kwenye kabati bovu jirani na ule mwembe.
Safari yenu ya Pemba imenikumbusha giLESi wangu wa moyo, ngoja nimtafute.
Wakuu,

Nina miaka 4 sasa nafanya utafiti kuhusu kuwepo kwa uchawi sijapata kujiridhisha kihalisia kuwepo kwa ushirikina.Nimetembelea maeneo yote yanayosemekana ni maarufu kwa ushirikina kama Tanga, Sumbawanga, Pemba na Bagamoyo. Huko pemba nimefika maeneo ya wete kuna kamsitu wanasema ndio hatari kwa wachawi kukaa na kufanya matambiko kuna makaburi ya zamani sana walisema tukifukua tutakufa kwa vile tutachokoza 'wazee' tumefanya excavation vizuri tukakuta artifacts na masufuria ma hirizi na mavitambaa mekundu na meusi na manyoa, ni mwaka sasa na mpaka sasa hata mafuta hakuna aliye pata kwenye team yetu. Tulilala hapo hapo makaburini kwa kutumia tent hata mbu hakutun'ata.

Sasa swali ni kwamba mtu anasema ooh nimelogwa na kukimbilia kwa hawa watumishi fake wa Mungu na kusema wamepona, wamenpona nini? Mimi nimeomba wazee waniloge wakasema wameniloga sitozaa kabisa kwa sasa na miaka 28 na watoto 6 na wana afya nzuri na nimepima DNA ni wa kwangu.

Kama kuna mtu amelogwa au anaweza kuniloga atoe fact hapa.
Mzizi mkavu Asprin Bujibuji Nyani Ngabu faiza Fox Yericko Nyerere
 
Last edited by a moderator:
Ninapata mashaka kidogo kwa umri ulionao na idadi ya watoto ulionao! Hata hivyo labda nikuulize swali unaamini uchawi upo?
 
Ninapata mashaka kidogo kwa umri ulionao na idadi ya watoto ulionao! Hata hivyo labda nikuulize swali unaamini uchawi upo?

Hilo la watoto naomba mliache kwa sasa. Siko kuelezea maisha yangu binafsi naulizia uchawi. Kuna member wanaonijua uhalisia wangu na hao watoto kwa mfano Bujibuji na @aspirin. Nikielezea nilivyopata hawa watoto itakuwa thread maisha yangu ni muujiza tosha kaka.
 
Last edited by a moderator:
Tena hao ndio hawalogi kabisa sema wanajua kumtuliza mwanaume kumpa..... kisawasawa refer to my last thread... kuwa watoto wa imani ya.... ni noma. Sasa mwanaume anakuwa zuzu akiambiwa mguu pande na mguu sawa anaenda. So hakuna uchawi

Umenena vyema, hilo halina ubishi.
 
Wakuu,

Nina miaka 4 sasa nafanya utafiti kuhusu kuwepo kwa uchawi sijapata kujiridhisha kihalisia kuwepo kwa ushirikina.Nimetembelea maeneo yote yanayosemekana ni maarufu kwa ushirikina kama Tanga, Sumbawanga, Pemba na Bagamoyo. Huko pemba nimefika maeneo ya wete kuna kamsitu wanasema ndio hatari kwa wachawi kukaa na kufanya matambiko kuna makaburi ya zamani sana walisema tukifukua tutakufa kwa vile tutachokoza 'wazee' tumefanya excavation vizuri tukakuta artifacts na masufuria ma hirizi na mavitambaa mekundu na meusi na manyoa, ni mwaka sasa na mpaka sasa hata mafuta hakuna aliye pata kwenye team yetu. Tulilala hapo hapo makaburini kwa kutumia tent hata mbu hakutun'ata.

Sasa swali ni kwamba mtu anasema ooh nimelogwa na kukimbilia kwa hawa watumishi fake wa Mungu na kusema wamepona, wamenpona nini? Mimi nimeomba wazee waniloge wakasema wameniloga sitozaa kabisa kwa sasa na miaka 28 na watoto 6 na wana afya nzuri na nimepima DNA ni wa kwangu.

Kama kuna mtu amelogwa au anaweza kuniloga atoe fact hapa.
Mzizi mkavu Asprin Bujibuji Nyani Ngabu faiza Fox Yericko Nyerere

Akuroge nani wewe? apoteze wakati wake? mwenyewe hapo ulipo upo hoi bin taabani, ungekuwa mzima ungeota mchana (hallucinate) kuwa Kikwete ni baba'ko mzazi?
 
Akuroge nani wewe? apoteze wakati wake? mwenyewe hapo ulipo upo hoi bin taabani, ungekuwa mzima ungeota mchana (hallucinate) kuwa Kikwete ni baba'ko mzazi?

Kama huna cha kujibu bora ukae kimya. Wanasema bora kukaa kimya nakuonekana unajua kuliko kufungua mdomo na kuthiirishia umma ulivyo mtupu. Kila nacho post ndio jibu hilo hilo unatoa. Inaonekana wewe mjane na unaendeshwa kwa hisia zaidi ya reasoning. Kuna tiba nitakuponya kisaikolojia kwa vile kila jamii ina watu kama nyie na mko ili sisi tujione ni kiasi gani tumebarikiwa na Mungu.
 
Nilikutana na padri mmoja aliyekuwa anafanya utafiti kwa ajili Phd yake.
Anasema alizunguka kwa waganga wote maarufu nchini, mpaka nchi za jirani kujalibu kupata taafa zake ila kati ya mambo ambayo alisema hayapo ni "UCHAWI". Anasema kuna sumu, na mazingaombwe lakini uchawa kama ule wa kudai mtu kuruka na ungo ni uongo na kwamba hakuna anayeweza.
Ni mchango wangu tu.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom