Natafuta kiwanja Dar kwa sh milioni moja ya Kitanzania.

Mikopo Chefuchefu

JF-Expert Member
May 15, 2017
3,373
6,756
Waungwana, natafuta kiwanja chenye thamani kati ya milioni moja hadi moja na nusu kwenye maneo ya pembezoni mwa jiji la Dar. Kiwanja kisiwe umbali wa zaidi ya km 15 to city center.
Karibuni kwa wenye navyo muweke hapa details.
Nategemea kiwe na ukubwa angalau wa miguu 20X20 na kuendelea!
Tapeli asisogelee kabisa uzi huu, kazi yangu inaniwezesha kumchukulia hatua mimi mwenyewe bila hata kumfikisha kwenye vyombo husika...
 
Kipo mwasonga kwa mbele kama unaenda kiwanda cha cement cha kigamboni jamaa anacho 30*20.
 
Hyo bei labda uende handeni.pwani ni ngumu.tatizo una masharti.km 15 si bado upo dar hapo!?
 
Naona dalili za kuuziwa kiwanja sehemu haramu(bondeni eneo la mto msimbazi)
na shida kubwa ni hilo sharti la umbali na ukubwa wa kiwanja.
 
Ukikipata nam nakuongezea mara mbili au tatu dakika hyo hyo baada ya kununua... Hyo hata chanika kilometa 41 hupati hata ukaloge
 
Njoo in box tungee Mimi ninacho,kipo jangwani,upande WA kusini kinapakana na makao makuu mabasi ya mwendokasi, kaskazini klabu ya yanga.barabara IPO .umeme na maji huulizi
 
Back
Top Bottom