Natafuta kazi ya upishi kwenye Hotel au Mgahawa

Mpishi anatafuta kazi,

Ni mpishi mzuri sana wa vyakula mbalimbali vya ndani na nje.

Pia ni mchoma nyama mzuri Sana.

Amebobea Sana Sana kwenye kitengo Cha bites, chapati yake unaweza ukawa hujawahi kula au umeila sehemu chache Sana. Ni mtengeneza sekera mzuri mno!

Anahitaji kazi. Yupo tayari kufanya kazi popote ndani na nje! Kwa sasa anapatikana Dodoma.

Faida1 kwa hotel au mgahawa utakaomwajiri ni kwamba, yeye pia ni driver by professional. Anayo leseni hai ya kuendesha gari yoyote ukiachana na basi la mkoa. Hivyo mda mwingine unaweza ukamtumia katika kusambaza vyakula, kwenda sokoni n.k... ana uhitaji wa kazi

Asanteni.
Aje pm!!tuyajenge niko dar
 
Mwanza mfungulie genge,

Labda umfungulie mgahawa, umkabidhi, akuletee hesabu kwa siku.
 
Wakati nawakilisha ombi hapa, alikuwa dodoma
Lakini kwa sasa yupo dar na ndipo anapoishi? Ndio maana uzi nimeuhariri!!
 
Mkuu nijibu nina jambo nataka kuongea
Mawasiliano uliyonipatia nilimpa, akasema amepatana na bwana mmoja yupo mwanza, juzi akaenda
Kabla hajaenda aliniambia kuwa wamepatana ya kwamba atamlipa kiasi walichokubaliana, atampati mahala pa kulala, na ghalama za matibu yatukuwa kwa mwajiri,
Lakini jana tu nimepata malamiko kuwa, huyo mwajili ameenda kinyume na makubaliano, hakuna pahala pa kulala, ya kwamba ameambiwa ale analala hapo hapo jikoni, au kama hawezi kulala jikoni awe akalale gheto na washikaji!
Hivyo naona atakuwa amekata tamaa ya kazi kutona na huyo boss wake kwenda kinyume na makubaliano. Hivyo naweza nikasema bado anahitaji kazi.
 
Mawasiliano uliyonipatia nilimpa, akasema amepatana na bwana mmoja yupo mwanza, juzi akaenda
Kabla hajaenda aliniambia kuwa wamepatana ya kwamba atamlipa kiasi walichokubaliana, atampati mahala pa kulala, na ghalama za matibu yatukuwa kwa mwajiri,
Lakini jana tu nimepata malamiko kuwa, huyo mwajili ameenda kinyume na makubaliano, hakuna pahala pa kulala, ya kwamba ameambiwa ale analala hapo hapo jikoni, au kama hawezi kulala jikoni awe akalale gheto na washikaji!
Hivyo naona atakuwa amekata tamaa ya kazi kutona na huyo boss wake kwenda kinyume na makubaliano. Hivyo naweza nikasema bado anahitaji kazi.
Analipwa shingapi
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom