Natafuta kazi mikoa ya Nyanda za Juu Kusini. Nimesomea Diploma ya Ualimu

Empirically

JF-Expert Member
Oct 27, 2019
238
86
Wakuu habari za saizi! Mimi ni kijana wa kiume, mhitimu wa diploma ya ualimu lakini bado sijafanikiwa kupata kazi. Hivyo naomba kazi yoyote ya halali ya kuniwezesha kuendesha maisha yangu.

Iwe niliyosomea au yoyote nitakayoweza kuifanya. Mimi naishi Dodoma. Kama kazi ikipatikana mikoa ya nyanda za juu kusini itakuwa vizuri zaidi, maana pia napenda kilimo.Na pia ndoto yangu kuishi mikoa ya huko wakuu.

Hivyo naomba msaada wakuu niende mbali na nyumbani nije huko kutafuta.

Natanguliza shukrani ndugu.
 
Kazi yeyeto? Duh ila si mbaya kama upo Mbeya nenda BigStar fm wanapokea wafanya kazi
Nipo Dodoma mkuu yah namaanisha Kaz yoyote ya halali nitayoweza kuifanya iwe niliyosomea au yoyote nitakayoweza kujishughulisha. Ila hiyo Kama ya utangazaji hapana Sina ujuzi nayo
Kazi yeyeto? Duh ila si mbaya kama upo Mbeya nenda BigStar fm wanapokea wafanya kazi
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom