Natafuta dada wa kazi

BILGERT

JF-Expert Member
Feb 27, 2015
6,535
10,974
Anahitajika dada wa kazi,awe na vigezo vifuatavyo.
A)Umri kuanzia miaka 18-25
B)Awe na uzoefu wa kazi za ndani, pamoja na kupika.asiwe mtu wa kuanza kufundishwa kazi.
C) Awe anatokea Singida, Manyara ama Mwanza.
D) Awe na mdhamini anaye tambulika in case of anything.
E) Awe muaminifu na mwenye tabia njema.

AINA YA MAJUKUMU
A) kupika, kufua na usafi kiujumla.
B) Wahusika bado hawana mtoto kwa sasa,muda mwingi wanashinda kazini.

MSHAHARA
A) Atalipwa Tsh 60,000 inaweza kuongezeka kulingana na uwajibikaji wake mzuri na wataishi naye kama ndugu.
B) Atagharamiwa matibabu.

Mwenye ndugu ambaye ana vigezo anaweza kunicheki PM.

Makubaliano yakisha fikiwa,huyo binti ataanza kazi mwishon mwa mwezi wa 12 mwaka huu.

Karibun sana.
 
2000 kutwa nzima? Acheni unyanyasaji ni kinyume na haki za kibinaadamu
Alaf wakienda uarabuni watu wanakuja kusema wana nyanyaswa kwa hali hii ndio maana dada zetu wanaona bora wajilipue waende huko uarabuni kwenye manyanyaso maana kwa ghalama za maisha iv sasa na mshahara wa iyo kazi hapa tz ni mbingu na ardhi
 
Mnaobeza hiyo pesa na huenda mkawakatili ndgu zenu kwenda kwenye hiyo kazi ilhali huko waliko hamwasaidii kwa chochote hata hiyo 60,000 kwa mwezi hapati zaidi ya kusubiri apate mimba familia iilee coz uwezo wa kumuendeleza hamna.

Kama wataishi kama ndgu, kula, kuvaa na kulala ni juu ya mwajiri hiyo si ni nafasi ya wazazi/walezi/ndgu kujipanga huku ile pesa inawekwa kama akiba ili walau akimaliza mwaka kazini ajue atafanya nini.

Kuna familia wakikusanya pesa zao familia nzima hawafikii huo mshahara kwa mwezi mzima. Labda hamjaishi vijijini huko ambako mlo kwao ni kwa manati.
 
2000 kutwa nzima? Acheni unyanyasaji ni kinyume na haki za kibinaadamu
1.Sabuni 20,000
2.Maji. 30,000
3.Chakula, chai na dinner 300,000
4.matibabu 200,000
5.Entertainment 50,000
6.Vinjwaji 20,000
7.Malazi Kwa siku 150,000
Hiyo 60 elfu na mavazi?


760,000/-
 
Yani wadada wa kazi walivyo wagumu kuwapata alaf unakuja na masharti kibao as if wapo mahali tu hawana pa kwenda. Ungejua soko lao lilivyo gumu saiz hata usingekuwa na masharti kibao. Yani umeandika as if kuna watu wako mtaani wanatafuta kazi za kuwa wadada wa kazi.

Skilizia show
 
Yani wadada wa kazi walivyo wagumu kuwapata alaf unakuja na masharti kibao as if wapo mahali tu hawana pa kwenda. Ungejua soko lao lilivyo gumu saiz hata usingekuwa na masharti kibao. Yani umeandika as if kuna watu wako mtaani wanatafuta kazi za kuwa wadada wa kazi.

Skilizia show
atajua hajuii :D :D :D :D
 
Back
Top Bottom