Natafuta binti wa kazi kwa ajili ya Mama Ntilie. Mshahara Tsh. 3,000/- kwa siku

Mwita Mtu Mrefu

JF-Expert Member
Sep 6, 2020
740
1,106
Hello Jf

Binti wa kazi anatafutwa.

Sifa
1. Ajue kupika chapati
2. Awe na Lugha nzuri kwa wateja na mchangamfu
3. Ajue hesabu
4. Awe anajua kuhudumia vizuri

Kazi ni ya mama ntilie, kuuza supu na chapati

Mshahara ni 3000 kwa siku, nyongeza utajadiliana na boss wako.

Chakula utapata hapo hapo asubuhi.

Kazi inaanza saa 1 asubuhi mwisho saa saba

Piga simu 0744033555

Tupunguze comment za kejeli, ukiona mshahara mdogo endelea na mishe zako.
 
Hello Jf

Binti wa kazi anatafutwa.

Sifa
1. Ajue kupika chapati
2. Awe na Lugha nzuri kwa wateja na mchangamfu
3. Ajue hesabu
4. Awe anajua kuhudumia vizuri

Kazi ni ya mama ntilie, kuuza supu na chapati

Mshahara ni 3000 kwa siku, nyongeza utajadiliana na boss wako.

Chakula utapata hapo hapo asubuhi.

Kazi inaanza saa 1 asubuhi mwisho saa saba

Piga simu 0744033555

Tupunguze comment za kejeli, ukiona mshahara mdogo endelea na mishe zako.
...mkuu Kwan lazima awe binti ... Kama kuna kijana wa Kiume mpishi mzuri wa chapati , Ana lugha nzuri kwa wateja,mjuzi wa hesabu, anajua kuhudumia vizuri wateja na ni mchangamfu .. hakufai ? Kwakua sio binti.?
 
...mkuu Kwan lazima awe binti ... Kama kuna kijana wa Kiume mpishi mzuri wa chapati , Ana lugha nzuri kwa wateja,mjuzi wa hesabu, anajua kuhudumia vizuri wateja na ni mchangamfu .. hakufai ? Kwakua sio binti.?
Mama ntilie na watu wa bar huwa wanahitaji mabinti kwa sababu nyingi tu.

Nadhani wanaume wanaelewa hili kwa kirefu..

Karibu supu kongoro mixer karafuu
 
Mkuu japo umejitetea na operation cost lakini ukweli kwa maisha ya Dar pesa yako bado ni ndogo! Maana unasema mfanyakazi wako anaanza kazi saa 1 asubuhi na kumaliza saa 7.

Hii manake anafanya kazi kuanzia asubuhi mpaka mchana! Offa zako umesma nje ya mshahara atapata chakula cha asubuhi, hii mana yake mchana na usiku gharama za chakula ni zake mwenyewe! Je kwa malipo hayo ya elf tatu anaishije kumbe?

Si itakuwa inaishia tu kwenye mlo wa mcha na usiku? Vipi kuhusu nauli yake ya kumleta na kumrudisha kazini everyday? Vipi kuhusu pesa ya sabuni ya kufungulia nguo zake maana unadhifu nao ni muhimu kwa mama ntilie, hata kama anavaa zile uniform na kofia lazima kuzifua kila wakati! Je kwa hiyo 3k ataweza kweli? Na kama kila siku unamlipa hiyo buk 3 means mwisho wa mwezi hana chake, Je akiugua upo tayari kumgharamia matibabu?

Mshahara wako unakaba kwa kila namna, mi binafs nashauri kama haiwezekani kuongeza japo ikafika buk5, basi fanya kumpa hifadhi ukae nae ili apate milo yote 3 kwako, alafu mkubaliane mshara hata ukipunguza mpaka 50k kwa mwezi ni nafuu kuliko hali hiyo ni ngumu, nina uhakika hata ukimpata hatodumu ataacha tu maana kama anaishi amepanga nyumba, kwa mshahara huo hawezilipa kodi ya nyumba!

Na kama anaishi kwao ni lazima watambana atoe pesa ya mahitaji nyumbani maana mabint wa nature hiyo hata makwao huwa hawajiwezi kiuchumi hivyo unawezakuta yeye ndo akawa tegemeo wa familia na mshahara wa buku 3 kwa siku!
 
Back
Top Bottom