Natafuta ajira katika fani ya ujenzi

Wakipekee

JF-Expert Member
Aug 21, 2019
5,345
9,202
Habari wanaJF....

Poleni na mihangahiko ya hapa na pale ya ujenzi wa taifa.. Tuendelee kulipambania taifa letu itoshe tu kusema kazi iendelee.

Nije kwenye hoja yangu.. Naamini humu kuna mafundi ujenzi wengi tu na pia kuna wadau ambao walishawahi kufanya hizi pia watu kwenye kampuni za ujenzi au hata wale ambao wanafahamiana na watu wa aina hiyo. Tafadhali naombe usiupite huu Uzi kama unayo nafasi ya kunisaidia mimi ndugu yenu naombeni mnishike mkono tafadhali nahitaji kibarua kama saidia fundi. Nina uzoefu na hiyo kazi pia nafanya kazi kwa bidii sana sehemu yoyote ile hapa nchini niko tayari kuja kufanya kazi.

Natanguliza shukurani zangu.
 
Habari wanaJF....

Poleni na mihangahiko ya hapa na pale ya ujenzi wa taifa.. Tuendelee kulipambania taifa letu itoshe tu kusema kazi iendelee...

Nije kwenye hoja yangu.. Naamini humu kuna mafundi ujenzi wengi tu na pia kuna wadau ambao walishawahi kufanya hizi pia watu kwenye kampuni za ujenzi au hata wale ambao wanafahamiana na watu wa aina hiyo. Tafadhali naombe usiupite huu Uzi kama unayo nafasi ya kunisaidia mimi ndugu yenu naombeni mnishike mkono tafadhali nahitaji kibarua kama saidia fundi. Nina uzoefu na hiyo kazi pia nafanya kazi kwa bidii sana sehemu yoyote ile hapa nchini niko tayari kuja kufanya kazi.

Natanguliza shukurani zangu..

Saidia fundi ni wewe tu kujichanganya mwenyewe. Fika maeneo wanakojenga ongea nao na ukimkuta msimamizi we mfate mwambie tu naomba kazi hapa na mimi
Niamini mimi anakupa hapo hapo na jioni unapata 10000-15000 yako fresh

Usikae tu mtandaoni hizo kazi sio za connection ni za kujiongeza mwenyewe.
 
Saidia fundi ni wewe tu kujichanganya mwenyewe. Fika maeneo wanakojenga ongea nao na ukimkuta msimamizi we mfate mwambie tu naomba kazi hapa na mimi
Niamini mimi anakupa hapo hapo na jioni unapata 10000-15000 yako fresh

Usikae tu mtandaoni hizo kazi sio za connection ni za kujiongeza mwenyewe.
Ndo kazi nazopiga hata sahivi niko job sema natafuta ambayo ina chaka la muda mrefu hata miezi sita mfano kwenye gorofa... Maana hizi napata za siku mbili tatu then unasota hata wiki thus y natafuta MTU mwenye kazi nyingi nisaidie kama inawezekana bro..
 
Ndo kazi nazopiga hata sahivi niko job sema natafuta ambayo ina chaka la muda mrefu hata miezi sita mfano kwenye gorofa... Maana hizi napata za siku mbili tatu then unasota hata wiki thus y natafuta MTU mwenye kazi nyingi nisaidie kama inawezekana bro..

Ah hapo sawa sasa nimeeelewa
Kwa msaaada mimi naweza kukushauri kuna sehemu inaitwa MANDERA, mkoa wa pwani ni mbele kidogo ukivuka mto wami unamaliza yale majengo ya dawasa hapo mbele kuna njia panda ya kwenda Miono/Saadani panaitwa Mandera
Hapo kila asubuhi vijana wanakaa hapo zinakuja kenta kuanzia 2 mpaka 4 zinabeba vijana zinapeleka kufanya kazi kwa mchina wa kujenga, kuna kuchimba sijui, kuna kupiga mawe. Jioni zinawarudisha pale pale na hela zao kibindoni
Jaribu kufatilia pale
 
Ah hapo sawa sasa nimeeelewa
Kwa msaaada mimi naweza kukushauri kuna sehemu inaitwa MANDERA, mkoa wa pwani ni mbele kidogo ukivuka mto wami unamaliza yale majengo ya dawasa hapo mbele kuna njia panda ya kwenda Miono/Saadani panaitwa Mandera
Hapo kila asubuhi vijana wanakaa hapo zinakuja kenta kuanzia 2 mpaka 4 zinabeba vijana zinapeleka kufanya kazi kwa mchina wa kujenga, kuna kuchimba sijui, kuna kupiga mawe. Jioni zinawarudisha pale pale na hela zao kibindoni
Jaribu kufatilia pale
OK asante kwa ushauri sema ningepata taarifa zaidi ingekua poa maana siko Dar niko mbali kidogo so napenda nipate uhakika flani
 
Sisi tunaitwa Madrassatul Abraar, ni wadau wa ujenzi wa kisasa, tuna kiwanda cha kuzalisha bidhaa za ujenzi za kisasa na Tunahitaji mafundi ujenzi, kuanzia wa kiwandani kwenye uzalishaji mpaka kwenye ufundi wenyewe. Tuinahitaji mafundi wa viwango tofauti, kuanzia wanaohitaji kujifundisha ujenzi mpaka wale wazoefu wa kusimamia kazi. Tupo very strict kwa ubora. Kama unapenda kufanya kazi na watu wenye kujali ubora wa kazi za ufundi, nidhamu za kazi za ufundi na mwenye kujali miiko ya kazi za ufundi na sio uwingi wa kazi basi wasiliana nasi.

Pia tupo tayari kuongea na vikundi au makampuni na madalali wa mafundi ujenzi namna ya kushirikiana.

Kwa maelezo zaidi fika tuonane ana kwa ana au tuma WhatsApp 0625249605. Tupo, Mtaa wa Vitendo, Kata ya Misugusugu, Kibaha, Pwani. Tanzania.
 
Back
Top Bottom