Natabiri suala la mfumo wa Digitali Tanzania wabunge jiandaeni kupambana!

KIBURUDISHO

JF-Expert Member
Mar 28, 2011
1,002
274
Watanzania wenzangu pia wanaJF wenzangu nchi yetu ndio imebakia sehemu ya kufanyia majaribio kama sio majaribio sehemu ya kufanyia biashara.Mfumo huu tulioletewa tunadanganywa wa kidigitali kwa upeo wangu utakuja kutusumbua na utazua mjadala mkubwa Bungeni juu ya upatikanaji wa matangazo kwa wananchi wote na kwa nchi nzima.

Mfumo huu wa kianalogia kama wanavyodai wao japo sii wa kiananogia ni wa kidigitali tunaopata matangazo kwa njia ya satellite ni mzuri sana.Kwa sababu gani nasema utasumbua mfumo huo unafanya kazi sawa kabisa kama minara ya simu na makampuni ya simu yana ushindani sana lakini hayajaweza kuwafikia wananchi wote kwa Wilaya, kata na vijiji.

Sasa itakuwaje baada ya kufunga matangazo kwa njia ya satelite halafu tunaletewa mfumo huu wanaodai wao ni wa kidigitali,itakuwa kilio kwa watakaokuwa mbali na minara ya kurushia matangazo na hapo ndipo kila mbunge ataanza kukumbwa na maswali kutoka kwa wananchi wake na hapo ndipo ahadi zisizotimilika zitakapoanzia.

Utaanza kuambiwa hatuwezi kujenga mnara wa kurushia matangazo wa milioni kadhaa kwa ajili ya watumiaji wa tv wasiofikia hata 20,tofauti na sasa hata uwe peke yako vijijini ndani huko mabonde kuinama unao uwezo wa kununua tv na ungo wako na ukapata matangazo bila shida yoyote.Kwa hiyo watanzania wenzangu hivyo ndivyo nionavyo mimi!!!
 
teh teh wabongo bana yaan kila kitu wanarelate na siasa; sasa hapa wabunge wameingia vipi jamani, kwani wabunge kwenye kampeni zao ndo waliwaambia watu mambo ya digital.

halafu mimi nawasiwasi na uelewa wako kaka kwani sisi tu ndo tunachange mambo ya kidigital?? ni hivi world wide analogia itazimwa 2015 lakini sisi ili kujiweka sawa tutaizima december 2012. sasa tumekuwa wamajaribio wapi na wapi?

maswala ya teknologia waachie watalamu bana na usilete siasa humu.
 
Kama unatazama tv kwa njia ya sattellite basi ujue kuwa tayari unatumia digital na hutahitaji kufanya chochote. Tofauti itakuwa kwa wale ambao wanatumia antenna kupangalia tv, wao ndio itabidi kununua decoders (au tv zenye decoders tayari) ili waweze kutazama matangazo.
 
Kama unatazama tv kwa njia ya sattellite basi ujue kuwa tayari unatumia digital na hutahitaji kufanya chochote. Tofauti itakuwa kwa wale ambao wanatumia antenna kupangalia tv, wao ndio itabidi kununua decoders (au tv zenye decoders tayari) ili waweze kutazama matangazo.

Kama ni hivyo safi sana, maana nilidhani ukifika muda huo tunatupa nyungo zetu na receivers.
 
teh teh wabongo bana yaan kila kitu wanarelate na siasa; sasa hapa wabunge wameingia vipi jamani, kwani wabunge kwenye kampeni zao ndo waliwaambia watu mambo ya digital.

halafu mimi nawasiwasi na uelewa wako kaka kwani sisi tu ndo tunachange mambo ya kidigital?? ni hivi world wide analogia itazimwa 2015 lakini sisi ili kujiweka sawa tutaizima december 2012. sasa tumekuwa wamajaribio wapi na wapi?

maswala ya teknologia waachie watalamu bana na usilete siasa humu.

Ndugu yangu natumai wewe ndo uelewa wako ni mdogo kwani sasa hivi suala la umeme likoje,Pia usilinganishe mazingira na jiografia za nchi za wenzetu ukaja kulinganisha na Tanzania.Suala eti 2012 hizo ni ndoto kama zilivyo kwa shirika la umeme Kwa suala la digitali ili lifanikiwe wangesubiri hadi hapo tutakapopata umeme wa uhakika kabisa ndipo mfumo huo utafanya kazi vizuri tofauti na hapo tutapandishiwa gharama za kulipia matangazo hayo ili kufidia gharama wanazoingia kwenye suala zima la utumiaji wa majenereta.Usione jirani kafanikiwa na wewe asubuhi unakurupuka na taulo kiunoni bila hata kuvaa nguo unaanza kufukuzana nae!!!!
 
Huo mfumo wa digital hapa bongo bado aujahanza ila ao star time na wengine ni wezi tu leo ukiwa na tv yako ya digital uwezi kupata chanel yoyote eti mpaka uwe na king'amuzi .king'amuzi kwa maelezo ya tbc ni kitu cha kukomveti mawimbi ya digital kuwa analogi sasa mi tayari ninayo tv ya digital kwa nini niwe na icho kingamuzi ? Huo ndo wizi wenyewe basi kama chaneli zote tunalipia ata hii ya taifa ?TBC. Wana JF siku ukinunua tv ya digital alafu ukaweka antena tu ukapata tbc bure basi hapo ndo digitali ipo hewani sio hivyo vidude vya wachina huo wizi wa mchana heri tuendelehe na satelit zetu
 
Ndugu yangu natumai wewe ndo uelewa wako ni mdogo kwani sasa hivi suala la umeme likoje,Pia usilinganishe mazingira na jiografia za nchi za wenzetu ukaja kulinganisha na Tanzania.Suala eti 2012 hizo ni ndoto kama zilivyo kwa shirika la umeme Kwa suala la digitali ili lifanikiwe wangesubiri hadi hapo tutakapopata umeme wa uhakika kabisa ndipo mfumo huo utafanya kazi vizuri tofauti na hapo tutapandishiwa gharama za kulipia matangazo hayo ili kufidia gharama wanazoingia kwenye suala zima la utumiaji wa majenereta.Usione jirani kafanikiwa na wewe asubuhi unakurupuka na taulo kiunoni bila hata kuvaa nguo unaanza kufukuzana nae!!!!

kaka unaonekana unapenda siasa eeh lakini mimi si mwanasiasa ila nakuelekeza uelewe kama hutaki kuelewa shauri yako narudia tena maelezo yangu

' wewe kama mwananchi wala hujaambiwa uhame kutoka analogia kwenda digitali bali ifikapo mwaka 2012 TV station zote zitaacha kurusha mitambo yao ya analogia na kutumia mitambo ya digitali so wewe kama mpokeaji wa matangazo ya tv utakutana na changamoto flani flan.
kumbuka 98% ya all TV tunazotumia ni analogy tv which means hazina uwezo wa kupokea matangazo katika mfumo wa digital. kwa hiyo sasa kampuni kama STARTIMES, TING, BASIC TRANSIMITION (Under itv and startv ambayo bado haijaanza huduma) wao kazi yao ni ndogo tu ni 'KUUZA VINGAMUZI ambavyo vinaweza kupokea mawimbi ya digital na kuyabadili kuwa Analogia ambapo tv yako inauwezo wa kuyanyambua na wewe kupata picha.

so hakuna siasa hapa na wala hujalazimishwa nunua king'amuzi chochote.
 
Huo mfumo wa digital hapa bongo bado aujahanza ila ao star time na wengine ni wezi tu leo ukiwa na tv yako ya digital uwezi kupata chanel yoyote eti mpaka uwe na king'amuzi .king'amuzi kwa maelezo ya tbc ni kitu cha kukomveti mawimbi ya digital kuwa analogi sasa mi tayari ninayo tv ya digital kwa nini niwe na icho kingamuzi ? Huo ndo wizi wenyewe basi kama chaneli zote tunalipia ata hii ya taifa ?TBC. Wana JF siku ukinunua tv ya digital alafu ukaweka antena tu ukapata tbc bure basi hapo ndo digitali ipo hewani sio hivyo vidude vya wachina huo wizi wa mchana heri tuendelehe na satelit zetu

yaaah ni wazo lako ni zuri sana na kama huna uelewa uneweza ona ni better solution kuliko kununua ving'amuzi but naomba nikueleweshe kidogo

' pale ambapo analogia itapozimwa na digitali kuwa on nikweli all digital tv 'ZITAKUWA NA UWEZO WA KOPOKEA MAWIMBI YA CHANEL' za digital so challenge ambayo inakuja sasa ni hiii kwa kuwa hizi tv station zitakuwa zinarushwa hewani kwa gharama kubwa inamaana wale wote wataokuwa wanatoa huduma za digitali WATAZIDHIBITI TV zao station ili watu walipie kuchangia gharama za urushaji matangazo. hapo ndipo kazi ya vingamuzi inapoingia sasa, kwani vingamuzi vingi vina smart card

pia kumbuka kuwa 'ALL TV STATIONS KAZI YAO ITAKUWA KUTENGENEZA TU PICHA LAKINI HAWANA RUHUSA YA KURUSHA HEWANI MATANGAZO YAO ILA WATAYAUZA KWA KAMPUNI ZILIZOPEWA DHAMANA YA KURUSHA AMBAZO NI startimes, ting na basic transimition(hawa bado), sasa haya matangazo kila kampuni itayadhibiti kwa kutumia frequency zao, mfano startimes (578, 610...) sasa how do they restricts these? ni kwamba watatumia SMART CARD, au kadi janja. sasa tv zote digitali ambazo zipo sasa hazitakuwa na uwezo wa kukamata digital chanel zilizo dhibitiwa, (ndio maaana ukinunua leo samsung lcd ambayo ni digital huwezi ipata SIBUKA TV (TV pekeee tanzania ambayo ipo mfumo wa digital)) kwa kuwa sibuka wanauza matangazo yao startimes ambayo imeidhibiti sibuka,

so kwa zile DIGITAL tv ambazo zina port ya kuinsert smart card wao wanaowezo wa kupata authority kwa kuinsert smart card ya either ting, startimes au...., sasa UKISHAWEKA SMART CARD TU kwa tv yako ujue swala la kulipia halikwepeki na hapo dezo hutoisikia
 
Yote mliyoyasema nakubaliana nanyi wala sijakataa.Ila hoja yangu kubwa ni lini watakapokuwa na uwezo wa kumfikia kila mwananchi popote pale alipo ndani ya nchi hii?? Bila kujali yuko mlimani au bondeni kama ilivyo kwa satelite inavyofanya kazi sasa hivi?.Hiyo ndio hoja yangu kubwa.
 
Back
Top Bottom