KIBURUDISHO
JF-Expert Member
- Mar 28, 2011
- 1,002
- 274
Watanzania wenzangu pia wanaJF wenzangu nchi yetu ndio imebakia sehemu ya kufanyia majaribio kama sio majaribio sehemu ya kufanyia biashara.Mfumo huu tulioletewa tunadanganywa wa kidigitali kwa upeo wangu utakuja kutusumbua na utazua mjadala mkubwa Bungeni juu ya upatikanaji wa matangazo kwa wananchi wote na kwa nchi nzima.
Mfumo huu wa kianalogia kama wanavyodai wao japo sii wa kiananogia ni wa kidigitali tunaopata matangazo kwa njia ya satellite ni mzuri sana.Kwa sababu gani nasema utasumbua mfumo huo unafanya kazi sawa kabisa kama minara ya simu na makampuni ya simu yana ushindani sana lakini hayajaweza kuwafikia wananchi wote kwa Wilaya, kata na vijiji.
Sasa itakuwaje baada ya kufunga matangazo kwa njia ya satelite halafu tunaletewa mfumo huu wanaodai wao ni wa kidigitali,itakuwa kilio kwa watakaokuwa mbali na minara ya kurushia matangazo na hapo ndipo kila mbunge ataanza kukumbwa na maswali kutoka kwa wananchi wake na hapo ndipo ahadi zisizotimilika zitakapoanzia.
Utaanza kuambiwa hatuwezi kujenga mnara wa kurushia matangazo wa milioni kadhaa kwa ajili ya watumiaji wa tv wasiofikia hata 20,tofauti na sasa hata uwe peke yako vijijini ndani huko mabonde kuinama unao uwezo wa kununua tv na ungo wako na ukapata matangazo bila shida yoyote.Kwa hiyo watanzania wenzangu hivyo ndivyo nionavyo mimi!!!
Mfumo huu wa kianalogia kama wanavyodai wao japo sii wa kiananogia ni wa kidigitali tunaopata matangazo kwa njia ya satellite ni mzuri sana.Kwa sababu gani nasema utasumbua mfumo huo unafanya kazi sawa kabisa kama minara ya simu na makampuni ya simu yana ushindani sana lakini hayajaweza kuwafikia wananchi wote kwa Wilaya, kata na vijiji.
Sasa itakuwaje baada ya kufunga matangazo kwa njia ya satelite halafu tunaletewa mfumo huu wanaodai wao ni wa kidigitali,itakuwa kilio kwa watakaokuwa mbali na minara ya kurushia matangazo na hapo ndipo kila mbunge ataanza kukumbwa na maswali kutoka kwa wananchi wake na hapo ndipo ahadi zisizotimilika zitakapoanzia.
Utaanza kuambiwa hatuwezi kujenga mnara wa kurushia matangazo wa milioni kadhaa kwa ajili ya watumiaji wa tv wasiofikia hata 20,tofauti na sasa hata uwe peke yako vijijini ndani huko mabonde kuinama unao uwezo wa kununua tv na ungo wako na ukapata matangazo bila shida yoyote.Kwa hiyo watanzania wenzangu hivyo ndivyo nionavyo mimi!!!