zuberi Abraham
JF-Expert Member
- Feb 13, 2016
- 480
- 389
Sio kwa lowassa kuongoza Tanzania kwa maoni yangu
Kwa umri wa EL sidhani kama anaweza kufikia rekodi ya Seif ya kuwania urais.Mungu alimuumba Lowassa kusaidia Jakaya awe Rais wa Tanzania na alimuumba Jakaya kusaidia Lowassa asiwe Rais wa Tanzania.
Lowassa ataishia kuwa Kama Maalim Seif kushikilia record ya kuwania Urais mara nyingi zaid
Tabiri nyingine hizi...!!!Natabiri Dk Hussein Nwinyi atagombea kupitia CCM na atashindwa na Lowassa wa CHADEMA.Panapo majaaliwa kama kawaida Monduli mwisho wa mwaka.
Si Get valve ni non-return valve.CCM tumeshaweka Get Valve. Anayetoka ni ngumu kurejea tena. Lowasa akirudi CCM ni kwa mapenzi hake ila sisi hatumhitaji tena. Hata ujumbe wa nyumba kumi hawezi kupata
Ahsante Mkuu. Hata hivyo, kwa kawaida Get Vslve ikishafungwa, hairuhusu reverse. Ndio maana nimetumia neno hiloSi Get valve ni non-return valve.
Bora umewakumbusha. Wanasahau kuwa Julai 23, Magufuli anavalishwa kofia ya Mwenyekiti wa CCMHalafu atapitishwa na nani?wakati mwenyekit atakuwa---- mhuu!!mbona mnasahau
Hivi ni lazima huyo mzee wenu awe rais wa nchi hii?
Ameshindwa mwaka 2015 akiwa na mihela Kibao, ataweza 2020 akiwa na tambu na sukari tu?Yaani halikwepeke lazma mzee awe rais 2020
#HpaKaziTu imewavuruga wengiEndelea kuota ndoto za abunuwasi.... #HapaKaziTu
Wamekosa Hoja, wamebaki kuota ndoto Za Mchana..... Huyo wanaesema atakuwa rais 2020 labda aumbe nchi yake akiwa na Nyumbu wenzake akawe rais huko.... Ila sio kwa watanzania wenye Akili timamu.#HpaKaziTu imewavuruga wengi
Mungu alimuumba Lowassa kusaidia Jakaya awe Rais wa Tanzania na alimuumba Jakaya kusaidia Lowassa asiwe Rais wa Tanzania.
Lowassa ataishia kuwa Kama Maalim Seif kushikilia record ya kuwania Urais mara nyingi zaid
Lowassa kawania urais mara moja? 1995 ulikuwa ushazaliwa kama bado waulize Wakubwa zako nani alikakatwa kwa kosa la kuwa na Mali nyingi kuliko Umri na akili zake?Pohamba
Lowassa keshawania urais wa TZ mara moja tu, mwaka jana 2015.
By 2020 atakuwa almost 70yrs old kama atakuwa na afya na nguvu aweza kuwania tena kwa mara ya pili na hopefully ndo itakuwa ya mwisho
Sasa atawania akiwa CHADEMA/UKAWA tena au CCM au chama kingine au kama PC hilo mimi silijui, nadhani tumwachie mtabiri Mr Hero!!
Isipokuwa Maalim Seif Shariff Hamad yeye keshawania urais wa Zenj mara tano (na kwa tafsiri yako hii ndo mara nyingi) kwa maana ya 1995, 2000, 2005, 2010 & 2015 na mara zote hizo hudaiwa ameshinda lakini huwa hatangazwi!!
Hiyo ni sawia kabisa let's waitJamani mimi sio mpiga ramli wala mshirikina.
Kwa hali inayoendelea ndani ya serikali na ndani ya CCM, kuna uwezekano mkubwa sana Lowassa kurudi CCM kabla ya 2020 na kuja kupambana katika kuteuliwa Jina la kupeperusha bendera ya CCM 2020.
Ukweli ni ukweli tu japo wale wafia rangi ya kijani ukiwauliza utendaji wa Magufuli wanaonaje? Kwa unafiki watasema wanamkubali kwa 100% ukweli kuwa wapo kinyume, japo hawasemi, amewabana Kila sehemu ametaka kuonekana mtawala au mfalme, sasa ni dhahiri wamemchoka lakini hayo yatakuja baadae kudhihirika.
Lowassa bado ana ushawishi mkubwa ndani ya CCM, hata akirudi nguvu kubwa anayo kuzidi Magufuli ndani ya Chama.
Tuombe uzima na afya tufike hiyo 2020.
In shaa Allah!