Natabiri kutokea kwa mambo haya manne kutokana na serikali kubana matumizi

Salary Slip

JF-Expert Member
Apr 3, 2012
46,888
143,985
Mosi,vigogo na watumishi wengi kwenye taasisi za umma kukimbilia kwenye mabenki kuchukua mikopo kukamilisha shughuli mbalimbali walizokuwa wamezianza au walikuwa wanaziendeleza katika awamu iliyopita kama vile shughuli za ujenzi wa nyumba za kuishi, kukamuilisha malipo ya ununuzi wa viwanja na miradi mingine ya binafsi waliyokuwa wakiiendesha kwa kutegema posho za safari, vikao, semina,makongamano na mambo mengine ya aina hiyo.

Pili, natabiri kudorora kwa kiasi kikubwa kwa shughuli za ujenzi kwenye maeneo mengi yenye shughuli za ujenzi.

Tatu,natabiri mapato ya serikali yanayotokana na kodi ya mauzo ya vifaa vya ujenzi kushuka sana.

Nne,natabiri mafundi wengi na vibarua wengi wa shughuli za ujenzi kukosa kazi maana wa kuwapa kazi nao mifuko imekauka.

Hii ni kutokana na ukweli kwamba watu wengi humudu kufanya shughuli za ujenzi,hasa ujenzi wa nyumba za kuishi, ununuzi wa viwanja,n.k, kwa kudunduliza hela za semina,safari,vikao, makongamano,madili ya maofisini na mikopo ya benki(sasa watalazimika kukopa zaidi).

Naomba kila mtu afanye tathimini ya speed na kiwango cha shughuli za ujenzi kwenye maeneo yaliyopimwa kwa ajili ya shughuli hizi kwa kulinganisha na miezi 7 iliyopita.
 
Sasa wewe ndugu huu ni utabiri gani wa mambo 2 halafu unataja mambo 4 wakati ambapo umezungumzia jambo 1 tu, ujenzi, ambalo umelinyumbua na kulizungumzia mara 4?
 
mimi ni mjenzi kusema kweli familia ya watoto wawili inataka kunishinda nafikiri tu kwenda kijijini tangia msukuma aingizwe ukuu mi sijapata hata tenda ya japo hta lak5 naishi kwa mikopo sa iv na maisha yanaelekea kunishinda sijajua wazo la kumpa urais nani alitoa jamani anaua watoto wetu na nja
 
Sasa hapo unatabiri nn hivi unawezaje kutabiri kitu kilichotokea na kinachoendelea kutokea"?nyinyi ndo watabiri hewa ambao tunawatafuta.
 
Vipi hutabiri elimu bure,afya,mishahara na miundombinu kuboreka? Au umespecialize kwenye ujenzi? Usemayo nikweli hatahivyo mana yamenikuta
 
kuna mtu nimemkopesha kahela fulani,sijui nilifikiria nini aisee, Mungu amsaidie anirudishie
 
Ndugu zangu watanzania, tutapata shida kwa muda mfupi lakini baada ya muda kupita Tanzania itakuwa ni nchi yenye kupiga hatua kubwa sana za maendeleo hasa katika miundombinu, afya, elimu nk.
 
Ndugu zangu watanzania, tutapata shida kwa muda mfupi lakini baada ya muda kupita Tanzania itakuwa ni nchi yenye kupiga hatua kubwa sana za maendeleo hasa katika miundombinu, afya, elimu nk.
sidhani kama rekodi ya jk ya miundo mbinu itavunjwa,wala ya elimu na pia afya,,kwa wakurugenzi wetu hawa wenye certificate za hoteli management...
 
Siku zote nilizoea kulala njaa mpaka nipende ila soon nahisi ntalala njaa bila kupenda., Ehee Mungu nisaidie.
 
8 Reactions
Reply
Back
Top Bottom