Natabiri jaribio lolote la kubadilisha Katiba na ukomo wa Rais litaibua mazito

Kuna tatizo gani mtu/watu kusema "Magufuli anahadaa watu kwa kusema hataongeza muda", hasa tukijua asivyokuwa mtu muungwana katika mambo mengi. Mtu huyu mmoja ndiye amejitwalia madaraka yote nchini na yeyote anayejaribu kumpinga anakipata cha moto!
Kwa nini wewe udhani (utabiri) hataongeza muda, au wewe ndiye yeye?
Nimekueleza, hata mfumo uliokuwepo, pamoja na ubaya wake, lakini taifa halikuwahi kuwa na hali mbovu kama ilivyo hivi sasa.
Matumaini ya kubadilisha mfumo huo yalikuwepo na yangeweza kuendelea na hata kufanikiwa, chini ya huyu mtu mmoja unayemtetea kwa sababu uzijuazo wewe hakuna njia ya kubadilisha chochote; lakini wewe umekazania "watu wabadilishe mfumo"!

Ni nani kaandika "mjadala wa kubadilisha mfumo" ni tatizo. Ni wapi umesoma ikielezwa kwamba watu hawawezi kujadili kubadili mfumo kwa sababu tu wameandika kuhusu kutomwamini Magufuli juu ya kujiongezea muda?

Unazungukazunguka tu humo humo na vijimane hivi visivyokuwa na maana yoyote.

Watu watamzuia vipi "kujiongezea muda" kwa kujadili tu kwamba haaminiki kwa lolote analotamka kutokana na historia yake toka aingie kwenye utawala na kufanya mambo ambayo hayajawahi kufanywa na kiongozi mwingine aliyemtangulia. Kusema tu "kutamzuia"?

Hili unalozua la "...kupachika kibaraka wake...", mbona wewe unalisema..., hili ndilo litakalomzuia kujiongezea muda yeye?
Nikuulize wewe, kuna "makosa gani" watu kujadili hilo la kujiongezea muda, kiasi kwamba linakusumbua wewe na kusingizia kuwa wataishiwa nguvu za kufanya mambo mengine, kama "kubadili mfumo"?

'Assumption' yako ya kwamba kujadili Magufuli kuogeza muda kunasitisha mambo mengine yote ya kujikwamua na huyu mtu ni mbovu. Na hapo hapo una 'speculate" kuwa atamteua mtu mbaya zaidi yake, yote haya wewe unayatoa wapi?
Unaweza kumhukumu Magufuli leo kwamba atamuua Mbowe 2025?
 
sawa Mkuu, nilichofurahi hiyo attachment yako nimekutana na neno utawala wa Burundi (Maziwa makuu)
sasa tafuta mabandiko ya Christopher Mtikila kuhusu utawala wa BAHIMA na malengo yao katika Maziwa makuu, wewe ni mzoefu na tulichangia sana mada hiyo, licha ya Mtikila kufunikwa, karibu sana 2025 si mbali
Jambo muhimu ni kuutunza huu uzi mpaka 2025. Tukijaliwa tuurejee.

Magufuli asipoongeza muda utafanya nini?

Hizi habari watu wamesema tangu enzi za Kikwete angalau.
 
Natabiri yakuwa jaribio lolote la kubadili katiba na kurefusha ukomo wa Rais litazuwa Moto wa kisiasa ambao haukuwahi kutokea tangu kuwepo kwa Taifa hili.

Yani hamtoamini wala kudhania. Itakuwa ni siku mbaya na nzito kwa Taifa ndipo sote tutaamini kweli kuna deep state in side state.

Nasali Jambo hili lisitokee wala kusemwa tu. Madhara yake yatatutesa sana kama Taifa.

Mungu ibariki Tanzania.
Mmeporwa kura mchana kweupe mmetuliza Mbupu sembuse kuongeza muda? Tulieni mchezee kichapo...
 
Mmeporwa kura mchana kweupe mmetuliza Mbupu sembuse kuongeza muda? Tulieni mchezee kichapo...
Hawa watu wanawayawaya tu.

Nimeuliza swali mara kadhaa hapa.

Wakiweza kumzuia Magufuli asiongeze muda, au Magufuli mwenyewe akiamua kutoongeza muda, halafu Magufuli akapachika kibaraka wake awe rais, na Magufuli aendelee kuendeleza sera zake kwa remote control, watafurahia kwamba wamemtoa Magufuli?

Mpaka sasa sijaona jibu.
 
Hawa watu wanawayawaya tu.

Nimeuliza swali mara kadhaa hapa.

Wakiweza kumzuia Magufuli asiongeze muda, au Magufuli mwenyewe akiamua kutoongeza muda, halafu Magufuli akapachika kibaraka wake awe rais, na Magufuli aendelee kuendeleza sera zake kwa remote control, watafurahia kwamba wamemtoa Magufuli?

Mpaka sasa sijaona jibu.
Leadership style Magufuli imeshajikita mizizi sana. Hakuna atakaye m-challenge wala la kukataa wala wa kumbishia tena hata akitaka saa saba mchana sote tuwe vitandani mwetu tumelala.
 
Leadership style Magufuli imeshajikita mizizi sana. Hakuna atakaye m-challenge wala la kukataa wala wa kumbishia tena hata akitaka saa saba mchana sote tuwe vitandani mwetu tumelala.
Watu ambao wameshindwa kutekeleza majukumu yao ya msingi, mara nyingi hujitungia vikazi kazi vya uongo na kweli vya kijingajinga ili waonekane wako busy.

Hiki ndicho kinachofanyika katika hoja hii.

Upinzani Tanzania umeshindwa mambo ya msingi.

1. Kuleta mabadiliko ya katiba.
2. Kuleta tume huru ya uchaguzi
3. Kuhakikisha kura haziibiwi
4. Kuhakikisha madaraka ya rais yanapunguzwa na haki za kikatiba kama za kuandamana na kukutana hazivunjwi.
5. Kuelimisha umma wa Tanzania na kuushirikisha kwenye kudai yote ya hapo juu.

Upinzani umeshindwa katika hayo matano ya muhimu yote.

Yani hata wizi wa kura wa 2020 umeshasahaulika.

Watu wanatutengenezea vita ya kijinga kuhusu mambo yatakayofanyika 2025.

Ni habari za kipumbavu sana.
 
.

Yani hata wizi wa kura wa 2020 umeshasahaulika.

.

Sio tu umesahaulika, Wapinzani wanalambishwa madaraka na fedha(Ruzuku). Huku kwetu tukio la akina Halima litakufa tu na watapeleka wabunge watake wasitake. Kule Zanzibar tamaa ya kuwa mkubwa na kukimbizwa na ving'ora imetamalaki, any time mzee mzima anageukia Quibla.

Hatuna upinzani Tanzania
 
Unaweza kumhukumu Magufuli leo kwamba atamuua Mbowe 2025?
Wewe unajua hawezi kufanya hivyo? Au ni lini ulisikia akitamka hawezi kufanya hivyo; na hata angetamka, kwa tabia zake alizokwishaonyesha ni watu kama wewe pekee ndio wangeamini anayosema.

Usitake kulazimisha watu wengine waamini unavyoamini wewe, hata ikiwa ni kwa sababu uzijuazo peke yako, au kwa utetezi tu usiokuwa na ushahidi wowote.
 
Sio tu umesahaulika, Wapinzani wanalambishwa madaraka na fedha(Ruzuku). Huku kwetu tukio la akina Halima litakufa tu na watapeleka wabunge watake wasitake. Kule Zanzibar tamaa ya kuwa mkubwa na kukimbizwa na ving'ora imetamalaki, any time mzee mzima anageukia Quibla.

Hatuna upinzani Tanzania
Kwa hoja zao hizi zisizo na kichwa wala mguu, wanaweza kuburuzwa mpaka 2035 angalau.

Kama si zaidi.
 
Kwa hiyo Magufuli akiwa hajasema hatamuua maana yake ni kwamba atamuua?

Na akisema hatamuua je, maana yake nini?
Mtu anapojulikana ni mwongo na hawezi kuaminika kwa lolote asemalo, na kukiwa na mifano ya aliyofanya kinyume na matakwa hata ya katiba, unazo sababu zipi kuonyesha kuwa hatafanya unalomtetea kuwa hatalifanya.

Umezua hili la Mbowe, kwa sababu zipi, kwa sababu hata kukana kuwa hatafanya hivyo hajawahi, kama alivyolaghai kuwa hataongeza muda.

Kama unataka mfano wako huo tuujadili kama tunavyojadili swala la kuongeza muda, basi kamwambie akane kuwa "Hatamuua Mbowe; halafu tutaanzia hapo kujadili hilo swala jipya.
 
Kwa hoja zao hizi zisizo na kichwa wala mguu, wanaweza kuburuzwa mpaka 2035 angalau.

Kama si zaidi.
Unajionyesha kutokuwa makini.
Maswala ya katiba na hayo unayoshikiia wapinzani wanayasahau kwa vile tu hawaamini kuwa Magufuli haaminiki kwa kudai hataongeza muda, ni maswala ya wananchi wote na wala siyo ya wapinzani peke yake. Hata CCM wanalo jukumu hilo. Kwa nini unalifanya lionekane ni la wapinzani peke yao?
 
Unajionyesha kutokuwa makini.
Maswala ya katiba na hayo unayoshikiia wapinzani wanayasahau kwa vile tu hawaamini kuwa Magufuli haaminiki kwa kudai hataongeza muda, ni maswala ya wananchi wote na wala siyo ya wapinzani peke yake. Hata CCM wanalo jukumu hilo. Kwa nini unalifanya lionekane ni la wapinzani peke yao?
Wananchi wengine na CCM wamewasusia hizi habari wapinzani.

Na wapinzani mnatapatapa.

Hamjui hata hoja ya kuanza nayo.

Mnarukia vioja vya kuzua kesi za makosa mnayobashiri yatafanyika 2025.

Kama vile hakuna makosa yaliyokwishafanyika 2020.

Just ridiculous.
 
Mtu anapojulikana ni mwongo na hawezi kuaminika kwa lolote asemalo, na kukiwa na mifano ya aliyofanya kinyume na matakwa hata ya katiba, unazo sababu zipi kuonyesha kuwa hatafanya unalomtetea kuwa hatalifanya.

Umezua hili la Mbowe, kwa sababu zipi, kwa sababu hata kukana kuwa hatafanya hivyo hajawahi, kama alivyolaghai kuwa hataongeza muda.

Kama unataka mfano wako huo tuujadili kama tunavyojadili swala la kuongeza muda, basi kamwambie akane kuwa "Hatamuua Mbowe; halafu tutaanzia hapo kujadili hilo swala jipya.
Akikanusha utamuamini?
 
Sio tu umesahaulika, Wapinzani wanalambishwa madaraka na fedha(Ruzuku). Huku kwetu tukio la akina Halima litakufa tu na watapeleka wabunge watake wasitake. Kule Zanzibar tamaa ya kuwa mkubwa na kukimbizwa na ving'ora imetamalaki, any time mzee mzima anageukia Quibla.

Hatuna upinzani Tanzania
Tanzania kuna wafanyabiashara wa siasa na sio wanasiasa.
 
Wananchi wengine na CCM wamewasusia hizi habari wapinzani.

Na wapinzani mnatapatapa.

Hamjui hata hoja ya kuanza nayo.

Mnarukia vioja vya kuzua kesi za makosa mnayobashiri yatafanyika 2025.

Kama vile hakuna makosa yaliyokwishafanyika 2020.

Just ridiculous.
Sijui maana yako ya 'wapinzani' ni ipi hasa katika mjadala huu. Unanijibu mimi unajua niko kwenye chama gani cha upinzani?

Ni wananchi wapi hasa waliowasusia hao unaowaita wapinzani? Wewe huoni wananchi hao na wapinzani, na hata CCM wenyewe ni mateka wa mtu unayemtetea?

Wewe unadhani wananchi hawaoni makosa yaliyokwishafanyika 2020?
 
Back
Top Bottom