Nasumbuliwa na Jinamizi hili kila nikilala naomba Msaaada na Ushauri

chugaa

Member
Nov 6, 2020
80
99
Habari za Jioni wakuu!

Mimi ni kijana mwenye umri wa miaka 28. Naomba ushauri kwa hili suala la kusumbuliwa na majinamizi haya wakati napokuwa nalala iwe mchana, asubuhi au usiku. Japokuwa hii hali huwa haitokei kila siku ila haipiti mwezi au wiki mbili ikajirudia.

Nakuwa nakabwa na Kinataka kuniingilia kinyume cha maumbile. Na nikiamka nasikia kama kuna mtu kanifanyia kitu kinyume na maumbile. Inauma sana!

Hii hali nimepambana nayo sana sio kwa Waganga wale wa mitishamba na wanaoutumia vitabu vya kiarabu pia kwa watumishi mbalimbali kuombewa. Ila mpaka sasa bado sijapata ufumbuzi. Nimepoteza pesa nyingi sana kwenye hili suala,nyingi!

Hali hii inanipa stress mpaka kuna kipindi natamani kujidhuru niondoke dunia hii.

Inaniumiza sana. Nifanyaje halii hii iishe.

Hali hii inasimbua tangu sijamaliza hata chuo, zaidi ya mwaka wa Saba. Kipato changu ni kizuri na najimudu vizuri na kuishi maisha mazuri tu. Hali hii pia huwa inanitokea hata nikiwa nimelala na mwanamke wangu.
 
Tafuta makanisa ya kilokole ya kiukweli wakuombee,ikiwezekana mkabidhi Mungu kabisa maisha yako kisha funga na kuomba kwa kushirikiana na watumishi wa ukweli tuone kama yatarudi, nguvu za giza zote kiboko yake ni YESU pekee,pole sana.
 
Tafuta makanisa ya kilokole ya kiukweli wakuombee,ikiwezekana mkabidhi Mungu kabisa maisha yako kisha funga na kuomba kwa kushirikiana na watumishi wa ukweli tuone kama yatarudi, nguvu za giza zote kiboko yake ni YESU pekee,pole sana.
Nimejitahidi sana kwenda mkuu. Inaniumiza sana kwa kweli,
 
8 Reactions
Reply
Back
Top Bottom