Natania
JF-Expert Member
- Dec 25, 2012
- 262
- 217
Lazima niseme ukweli kuwa mwanzoni niliweka matumaini ya kumpigia kura at least mmoja wa wagombea toka upinzani kwani CCM nilishaichukia toka enzi za akina Mrema miaka ya 90.
Lakini siku za hivi karibuni nimegundua kumbe hata upinzania ni walewale tu. Chadema na mikwara yao waliweza kunivutia mwanzoni ila kwa sasa hata nikiwa usingizini siwezi kumchangua kiongozi yeyote kutoka CHADEMA. Hili sakata la Zito, Kitila limeivua CHADEMA nguo zote na madudu mengi hayana majibu mpaka leo.
Yaani kwa sasa kama mtu ukiamua kuzingatia yaliyomo kwenye katiba bila kujali watendaji wake basi katiba ya CCM inamaneno mazuri na ya maendeleo -Tatizo ni hao wanaojiita viongozi wa CCM.
Nasema kwa sasa matumaini yangu YA KISIASA yamebakia kwenye wagombea binafsi -huenda hawa wakawa majasiri wa kufanya yale ya moyoni kuliko watu kama akina Slaa ambao wanakaa kimya kwenye madudu ya chama chao na kupigia kelele madudu ya chama tawala -hawa wakipewa nchi watakuwa hatari zaidi ya wanaChadema wanavyodhani.
Nimemaliza na haya ni maoni yangu, toa na wewe ya kwako!
Lakini siku za hivi karibuni nimegundua kumbe hata upinzania ni walewale tu. Chadema na mikwara yao waliweza kunivutia mwanzoni ila kwa sasa hata nikiwa usingizini siwezi kumchangua kiongozi yeyote kutoka CHADEMA. Hili sakata la Zito, Kitila limeivua CHADEMA nguo zote na madudu mengi hayana majibu mpaka leo.
Yaani kwa sasa kama mtu ukiamua kuzingatia yaliyomo kwenye katiba bila kujali watendaji wake basi katiba ya CCM inamaneno mazuri na ya maendeleo -Tatizo ni hao wanaojiita viongozi wa CCM.
Nasema kwa sasa matumaini yangu YA KISIASA yamebakia kwenye wagombea binafsi -huenda hawa wakawa majasiri wa kufanya yale ya moyoni kuliko watu kama akina Slaa ambao wanakaa kimya kwenye madudu ya chama chao na kupigia kelele madudu ya chama tawala -hawa wakipewa nchi watakuwa hatari zaidi ya wanaChadema wanavyodhani.
Nimemaliza na haya ni maoni yangu, toa na wewe ya kwako!