Drifter
JF-Expert Member
- Jan 4, 2010
- 4,428
- 4,127
Polisi wanatumika vibaya na kuzidi kudhalilishwa. Kwa hili wangeminya tu. Manake hivi sasa wanaonekana kufanya kazi kwa kuchagua kosa lipi lishughulikiwe, lipi liachwe kutegemeana na ama maagizo ya serikali ya CCM au wao wenyewe kuhangaika kujikomba kwa watawala. Mikutano ya kisiasa ya vyama vyote nchini haikosi kauli za "kufikirisha" na "kuchangamsha". Wala hazitishii amani yoyote zaidi ya manyanyaso na adha wazipatazo wananchi siku kwa siku toka kwa dola na vyombo vyake. Hivyo, kuwang'ang'ania akina Nassari huku unawagwaya akina Lusinde, Mkapa, Tyson, n.k. ni aibu!