Hawa ni kawaida yao kususia kila kitu. Tumeshawazoea.
sialiwaahidi akiwa mbunge atahakikisha ardhi inagawiwa kwa masikini wanaarumeru. sasa atekeleze ahadi yake, aache kutafuta kuonewa huruma.viwanja hivi wanapeana mafisadi tu na kuwaacha wananchi na wafanyakazi wa kipato cha kati wilayani arumeru bila ardhi
Kuna Shamba la Burka Ekari maelfu vigogo na Halmashauri wanalitolea macho. Mzungu amemaliza 99 years na anataka kubadilisha matumizi, mwanzo ilikuwa kilimo cha kahawa. Sasa manispaa imegoma na inataka kulichukua.
Nimepata tetesi, sina taarifa nyingi. Naomba mwenye habari hii kamili tuambiwe hapa JF.
Naomba pia Mh. Nasari ama Lema wafuatilie hii ishue ama Mh. Mdee.
Kama mna kumbukumbu ya Lile shamba lingine la Burka vigogo walivyogawana viwanja na kuwaacha wananchi njia panda. Wananchi waliambiwa watagaiwa, wakalipia ada.... hatimae vigogo wakagawana.