Nicole
JF-Expert Member
- Sep 7, 2012
- 4,274
- 2,514
Ameanika ufisadi huo katika mkutano wa hadhara aliofanya sokoni tengeru jijini arusha leo. Amesema madiwani hao wa CCM wamekataa mpango wake wa kujenga stendi ya kimataifa hapo tengeru badala yake wamegawa vibanda kwenye eneo la soko na kuwauzia matajiri wachache. Amesema mfano diwani wa viti maalum ccm frida kaaya ana vibanda 4 alivyowauzia matajiri hapo tengeru. Amesema tengeru ni eneo zuri la uwekezaji kwani kuna taasis mbalimbali kama chuo cha Nelson mandela alichozindua kikwete hivi karibuni, hoteli za kitalii, taasisi ya maendeleo ya mifugo, ziwa duluti n.k hivyo basi ni vyema wakasubiri mwekezaji atakayejenga soko la kisasa tengeru ili kila mtu anayeishi tengeru anufaike badala ya kugombea eneo la ekari 4 ambalo litanufaisha matajiri wachache. Katika kufanikisha hilo amesema amezungumza na wawekezaji mbalimbali akiwemo mkurugenzi wa mfuko wa hifadhi ya jamii(NSSF) Ramadhan Dau.Ambaye alimweleza wako tayari kufanya uwekezaji sokoni hapo na kukusanya ushuru kwa miaka 5-10 halafu baada ya hapo soko litakuwa mali ya wana arumeru. Amesema amefanya mengi kwa wana arumeru ambayo ccm walishindwa kufanya, ilhali yeye kwa muda wa miezi 6 ya ubunge wake ameweza kufufua zahanati na vituo vya afya vilivyokuwa havifanyi kazi ikiwemo majengo na ngarananyuki, amesambaza vitabu kwenye shule 12 za sekondari za kata, amefanikisha kupatikana ambulance mbili zilizokuwa hazifanyi kazi, amezindua shule ya kwanza ya mchepuo wa kiingereza(ya serikali) arumeru, amechimba visima vya maji mfano kata ya maroroni na kwingineko ingawa wenyeviti wa vitongoji na vijiji walikuwanakataa kuwapa wataalam ushirikiano.Amesema wana ccm wanapiga kelele yeye kununua kiwanja cha ujazo wa 900 meru mbona lowasa ana ekari 20 hawasemi.Hivyo alisusa kikao cha madiwani cha halmashauri ya meru na posho ya laki moja na sabini kwani hakutaka kushiriki kwenye mpango huo wa kifisadi unaolenga kuwakandamiza wananchi wa arumeru. kwahiyo amerudi kwa wananchi kuwaeleza yanayotendeka ili wananchi waamue.
Lema pia alikuwepo kumsapoti Nasari na akasema CCM imeamua kuwaajir Kinana na Mangula ili waendeleze uzoefu wao wa wizi katika chama cha mapinduzi.
Lema pia alikuwepo kumsapoti Nasari na akasema CCM imeamua kuwaajir Kinana na Mangula ili waendeleze uzoefu wao wa wizi katika chama cha mapinduzi.