G Sam
JF-Expert Member
- Apr 20, 2013
- 11,555
- 35,880
Ndiyo nilikuwa mkweli na hoja zangu zilikuwa za moto hadi wenzangu wakahisi kuwa nina chuki binafsi na Rais hayati Magufuli.
Mwaka 2016 mapema mwezi wa nne nilimshauri ajiuzulu na nikajenga hoja. Nilishambuliwa sana hadi uzi ukatupwa kapuni. Nilimuonya kuwa hatokuwa na ushawishi wowote ule kimataifa. Labda kitaifa kwa kuwa atafanikiwa kudanganya na kuziba watu midomo. Leo iko wapi?
Niliupinga mradi wa Stiglers na nikasikitishwa na kukatwa kwa miti zaidi ya milioni tatu huku tukijua kuwa chanzo cha maji yale ni miti. Nikaonya kuwa Stiglers haitokaa izalishe megawati 2000 zinazotajwa na kuwa tulikuwa tunadanganywa. Napo nikanangwa.
Nikaja kwenye fly overs na nikafikia kusema kuwa siku nikiwa Rais nazivunja vunja. Niliziita fly overs uchwara!
Daraja la Salenda hadi nikaonya kuwa lilileta ugomvi kati yake na Ombeni hadi akafukuzwa. Daraja la kule Kigongo ndiyo uwiiiii! Yani sitaki hata kukumbuka.
Nikaonya ule mreli wa gharama kubwa upo kwa ajili ya nani? Napo nikabezwa na kubagazwa! Nikalia juu ya kuvunjwa kwa jengo la Tanesco pale Ubungo nikaitwa mpiga dili aliyetupwa sasa analia lia!
Nilitukanwa, nikabezwa na ilipofika baada ya uchaguzi mkuu mchafu wa mwaka 2020 nikajiapiza kuwa sitokuja kuzungumzia tena chochote kile atakachofanya hayati na ikawa hivyo.
Leo tunarudi ili tusimame kuhesabiwa!
Mwaka 2016 mapema mwezi wa nne nilimshauri ajiuzulu na nikajenga hoja. Nilishambuliwa sana hadi uzi ukatupwa kapuni. Nilimuonya kuwa hatokuwa na ushawishi wowote ule kimataifa. Labda kitaifa kwa kuwa atafanikiwa kudanganya na kuziba watu midomo. Leo iko wapi?
Niliupinga mradi wa Stiglers na nikasikitishwa na kukatwa kwa miti zaidi ya milioni tatu huku tukijua kuwa chanzo cha maji yale ni miti. Nikaonya kuwa Stiglers haitokaa izalishe megawati 2000 zinazotajwa na kuwa tulikuwa tunadanganywa. Napo nikanangwa.
Nikaja kwenye fly overs na nikafikia kusema kuwa siku nikiwa Rais nazivunja vunja. Niliziita fly overs uchwara!
Daraja la Salenda hadi nikaonya kuwa lilileta ugomvi kati yake na Ombeni hadi akafukuzwa. Daraja la kule Kigongo ndiyo uwiiiii! Yani sitaki hata kukumbuka.
Nikaonya ule mreli wa gharama kubwa upo kwa ajili ya nani? Napo nikabezwa na kubagazwa! Nikalia juu ya kuvunjwa kwa jengo la Tanesco pale Ubungo nikaitwa mpiga dili aliyetupwa sasa analia lia!
Nilitukanwa, nikabezwa na ilipofika baada ya uchaguzi mkuu mchafu wa mwaka 2020 nikajiapiza kuwa sitokuja kuzungumzia tena chochote kile atakachofanya hayati na ikawa hivyo.
Leo tunarudi ili tusimame kuhesabiwa!