Nasikitika sana Tanzania miaka ishirini (20) ijayo Tanzania itakuwaje

Abdul Mganyizi

JF-Expert Member
Oct 28, 2019
1,044
1,996
Nianze kwa kusalimia ndugu zangu wana JF itifaki imezingatiwa. Watanzania wote wanamshukuru Mh Rais kwa elimu bure kwa kuwa ameruhusu watanzania wengi kufika shule wale waliokuwa wanashindwa.

Lakini hii elimu bure inayotolewa ndio mada yangu yakujadili leo. Mimi ni Mwalimu wa shule ya msingi mkoa fulani na wilaya fulani jina kapuni. Wakati Mh mwenye nchi anaingia madarakani niliomba kwenda chuo kikuu.

Sasa nilivyorudi nilishangaa sana kuona mambo yamebadilika sana. Walimu wenzangu wakaniambia kuwa tuliambiwa hatakiwi mwanafunzi yoyote darasa la saba kufeli. Sasa mimi nikauliza sasa itawezekanaje maana Mwalimu kazi yako kufundisha tu ila mtihani anafanya mwanafunzi.

Nilichoelezwa kuwa mtihani anafanya Mwalimu na sasa hivi shule zinashindanisha walimu, ukiona shule imefelisha jua walimu ndio wamefeli. Sasa mwaka jana ndio nikashuhudia vizuri kwenye semina Afisa Elimu anavyotoa miongozo kwa wasimamizi kuhusu huko wanakoenda kusimamia wahakikishe wanashirikiana na wakuu matokeo kuwa mazuri.

Leo hii ukishapangiwa kusimamia unakuta walimu washajipanga muda mrefu, wanafunzi hawafanyi chachote wanasubiria waletewe mtihani mzima.

Inasikitisha kila nikiitazama Tanzania ijayo. Sasa baada ya matokeo ya mwaka jana Mkurugenzi anawaita maafisa elimu kata na Afisa elimu na kusema "nawapongeza sana sana, mbinu iendelee kuwa hiyo hiyo ila mwakani ufaulu uwe asilimia mia sio tena 93".

Sasa nikitazama wanafunzi ambao hata jina lao kuliandika ilkuwa mtihani lakini wamefaulu tena kwa alama nzuri nasikitika sana. Sasa afisa taaluma ni rafiki yangu nikawa nateta nae, namuuliza hii ni sahihi kweli hata kwa Mungu tunaenda kujibu nini, anasema hii ni sahihi kwa kuwa mwenye nchi ndicho anachokitaka.

Yeye anataka kusikia wamefaulu, wamefauluje hilo halimuhusu. Kila mmoja abebe mzigo wake naye miaka yake kumi ikiisha ataondoka ndicho anachokitaka Rais wa nchi.

Poleni watanzania pamoja na wazazi kwa ujumla sisi walimu tunachokifanya kwa wanao kwa kuwafanyia mtihani wa mwisho wakati wamekaa shuleni miaka saba wakisubiri kufanya mtihani wa mwisho. Mungu ibariki Afrika na Tanzania kwa ujumla.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Na mimi nimeshuhudia hayo yote uliyoyasema, kabla ya kuajiriwa serikalini nilikuwa nafundisha private.

Nimekuja huku nimeshangaa sana udanganyifu uliopo kwa kweli hali si nzuri na ninaomba walimu tubadilike hata kama kuna msukumo toka juu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Walimu wa shule za msingi mmekuwa wazembe sana.

Japo siitetei serikali kwenye hili, lakini haiwezekani mtoto anamaliza darasa la saba hajui kusoma! HAIWEZEKANI.

Hakuna mtu mwenye ujinga kiasi hicho. Hata mataahira wakifundishwa wanaelewa.

Kuna uzembe mkubwa sana na huenda pia uwezo wa walimu umeshuka kiwango. (hasa ukizingatia academic qualifications zao ni duni sana) - form four failures.

Ndio aina ya walimu tunaowaona humu wasiojua kutofautisha R na L.

Shida ipo kubwa sana upande wa waalimu. Kama ni lawama, basi asilimia tisini za lawama ziende kwao!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sasa unamhukumu mwalimu ambaye hapewi stahiki zake kwa wakati...???...matokeo ya mwalimu huyaoni hapo hapo subiri miaka 7 au zaidi kutofautisha na daktari au nesi na ndo Mana mwalimu mgomo wake ni kimya kimya Ila matokeo utayaona
 
Sasa unamhukumu mwalimu ambaye hapewi stahiki zake kwa wakati...???...matokeo ya mwalimu huyaoni hapo hapo subiri miaka 7 au zaidi kutofautisha na daktari au nesi na ndo Mana mwalimu mgomo wake ni kimya kimya Ila matokeo utayaona
Pamoja na hizo stahiki, lakini wengi wa walimu hawana weledi wa kazi. Hasa walimu wa shule ya msingi.

Wengi tu nawafahamu ni form four failures waliokimbilia ualimu. Ni vilaza ajabu.

Lakini kwa Tanzania hiyo sio issue sana maana hata professor ana ufahamu sawa sawa na form four failure. Ndio maana unakuta waziri wa elimu hawezi angalau kuongea sentensi moja inayoeleweka.

Poleni sana!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Pamoja na hizo stahiki, lakini wengi wa walimu hawana weledi wa kazi. Hasa walimu wa shule ya msingi.

Wengi tu nawafahamu ni form four failures waliokimbilia ualimu. Ni vilaza ajabu.

Lakini kwa Tanzania hiyo sio issue sana maana hata professor ana ufahamu sawa sawa na form four failure. Ndio maana unakuta waziri wa elimu hawezi angalau kuongea sentensi moja inayoeleweka.

Poleni sana!

Sent using Jamii Forums mobile app
Umeandika fact ....Sasa io pole unampa Nani....sisi watanzania au?
 
Twende hivo hivo tu,
Kufall mtihani sio kufall maisha.

Lazima kuwe na watu elimu zote..

Phd na masters- 15%
Degree- 15%
Diploma- 25%
Certificate kwenda chini- 25%
Wasiojua kusoma- 20%
 
Ndio maana siku hizi tunao wanafunzi wa darasa la saba waliofaulu na kwenda secondary lakini hawajui kusoma na kuandika!
 
Back
Top Bottom