Nashindwa kuwaelewa Vodacom

man dunga

JF-Expert Member
Oct 13, 2013
3,179
5,513
Jana nimetuma 170000 pamoja na ada ya kutolea. Nimekatwa ada ya kutolea 3650 mpesa ada 1000 na tozo 2530.
Mpokeaji baada ya kutoa (katoa 174000 sababu alikuwa na akiba ya 11000 kabla ya mimi kumtumia) nae kakatwa ada ya kutolea 3650 na tozo 2530. Kwa hiyo ada ya kutolea imekatwa mara mbili.

Nimewapigia vodacom kwa namba 100 lakini sioni namna naweza kuongea nao zaidi wananiambia bonyeza namba ambazo hazina msaada .
 
Iko hivi Mkuu!.

Ukituma hela na ya kutolea, wao wanatuma hela nzima. Mfano umetuma 100,000 na ya kutolea 3,650 basi mteja wako atapokea 103,650.

Hapo sijaweka hela ya Tozo.

Sasa kuna uwezekano ndugu yako hakuwa na kiasi hicho kwenye simu yake kama akiba.
 
Iko hivi Mkuu!.

Ukituma hela na ya kutolea, wao wanatuma hela nzima. Mfano umetuma 100,000 na ya kutolea 3,650 basi mteja wako atapokea 103,650.

Hapo sijaweka hela ya Tozo.

Sasa kuna uwezekano ndugu yako hakuwa na kiasi hicho kwenye simu yake kama akiba.
Duuh hujaweka hela ya Tozo harafu atapokea nzima nzima umejichanganya hapo Mkuu..
 
Jana nimetuma 170000 pamoja na ada ya kutolea.Nimekatwa ada ya kutolea 3650 mpesa ada 1000 na tozo 2530.
Mpokeaji baada ya kutoa (katoa 174000 sababu alikuwa na akiba ya 11000 kabla ya mimi kumtumia) nae kakatwa ada ya kutolea 3650 na tozo 2530. Kwa hiyo ada ya kutolea imekatwa mara mbili.

Nimewapigia vodacom kwa namba 100 lakini sioni namna naweza kuongea nao zaidi wananiambia bonyeza namba ambazo hazina msaada .
WMEKULAMBA 7000..!:(
 
Iko hivi Mkuu!.

Ukituma hela na ya kutolea, wao wanatuma hela nzima. Mfano umetuma 100,000 na ya kutolea 3,650 basi mteja wako atapokea 103,650.

Hapo sijaweka hela ya Tozo.

Sasa kuna uwezekano ndugu yako hakuwa na kiasi hicho kwenye simu yake kama akiba.
Kabla ya mimi kumtumia alikuwa na akiba ya 11326.Kwa hiyo baada ya mimi kumtumia akawa na jumla ya 181326.

Alipotoa 174000 kabakiwa na akiba ya 1146 ambayo inathibitsisha kwamba kakatwa 3650 kama ada na 2530 kama tozo.Jumla kakatwa 6180. Sasa kwa nini akatwe tena 3650? Hata kama ametoa 174000 zaidi ya niliomtumia lakini kutoa 174000 makato ni yale yale 3650.
 
Naongea vipi na vodacom customer care maana nikipiga 100 naambiwa nibonyeze namba ambazo hazina msaada.
 
uenda alitakiwa kutoa kile kiwango ulichotuma tu hicho alichoongeza alipasa akitoe kivyake, kwa sasa watafute twitter wapo active zaidi.
 
Jana nimetuma 170000 pamoja na ada ya kutolea.Nimekatwa ada ya kutolea 3650 mpesa ada 1000 na tozo 2530.
Mpokeaji baada ya kutoa (katoa 174000 sababu alikuwa na akiba ya 11000 kabla ya mimi kumtumia) nae kakatwa ada ya kutolea 3650 na tozo 2530. Kwa hiyo ada ya kutolea imekatwa mara mbili.

Nimewapigia vodacom kwa namba 100 lakini sioni namna naweza kuongea nao zaidi wananiambia bonyeza namba ambazo hazina msaada .
Mbona ni sahihi mkuu.

Hujaonewa. Hii serikali ni ya majizi sana. Yaani yanapiga double payment. Yanakata ukituma yanakata ukitoa. Ni Huzuni.

Au Wacheki Whatsaap kwa msaada zaidi +255 754 100 100
 
3 Reactions
Reply
Back
Top Bottom