Nashindwa kujua ni nini hasa chanzo cha makazi ya polisi kuonekana duni karibu mikoa yote?

Samahani

JF-Expert Member
Oct 29, 2018
222
335
Wakuu,

Kwa muda mrefu nimekuwa nikijiuliza sana juu ya hili. Nashindwa kujua ni nini hasa chanzo cha makazi ya polisi kuonekana duni karibu mikoa yote. Sina shaka kuwa, baadhi yenu mtakuwa mashahidi kuwa, karibu mikoa yote ya Tanzania, nyumba za askari polisi zimekuwa duni MNO kiasi cha kutia aibu.

Awali, nilifikiri kuwa huenda ni kutokana na kutokukarabatiwa mara kwa mara. Lakini ajabu ni kuwa, zipo ambazo zimejengwa nikiwa naziona, na zilikuwa na ubora mzuri tu wakati zinaanza kutumika, lakini baada ya muda, mtazamo wa nyumba hizi unabadilika na kuwa mbaya mno na usioridhisha. Rangi hupauka na kuta kuwa chafu kupitiliza, mafaa huanza kunyofoka ovyo, zile ambazo ni za ghorofa huanza kuwa na leakage, Na mbaya zaidi, wao wenyewe huanza kubadili ramani kwa kuvuta vichumba kwa kutumia mabati chakavu, ceiling boards, nyavu kuu kuu n.k

Makazi haya ya mfumo wa kambi "servants Quarters" za polisi Tanzania, kwa mikoa yote, ni tofauti kabisa na ya taaluma zingine. Mathalani, Nyumba za walimu kwa shule kongwe nyingi za zamani kama vile Mwenge Singida, Moshi Tech Kilimanjaro, Pugu, Kibaha, Tosamaganga na zingine, nyumba hizi bado zina hali nzuri sana tofauti kabisa na muda ambao zimetumika. Nyumba za benki na taasisi zingine pia ni bora na zenye kuvutia!

Lakini cha ajabu, SERVANTS QUARTERS za Askari Polisi zimebaki kuwa chafu, zisizovutia, zilizoongezwa ongezwa vi structure visivyoeleweka na mambo mengine kibao. Ajabu ni kuwa, karibu kila mkoa kuna kundi kubwa la askari ambao ni mafundi waashi, na tena bado wanaweza kuwatumia wafungwa kuboresha, walau basi kupiga rangi, lakini bado nyumba hizi zimebaki kuwa na hali mbaya MNO..

Hii, hapa na pale, imeendelea kuzifanya hali za kimaisha za Askari Tanzania kuwa duni. Huenda uduni huu machoni kwa watu unatokana pia na makazi duni popote pale wanapoishi Askari Polisi.

Jamani, labda kuna wenye uzoefu juu ya hili.. NINI HASA TATIZO ZA MAKAZI YA ASKARI???
 
Sababu ni moja tu nayo ni hii
HAKUNA MTU WA KWENDA KUIBA CHOCHOTE KWENYE NYUMBA ZA POLISI.
Nyumba nyingi zinaonekana zimepambwa vizuri kwa madirisha ya nondo
zilizochongwa vizuri lakini mantiki ni ile ile ya kuzuia wezi.
Sijui ndani ya nyumba za polisi kukoje lakini nakshi ya nje
hakuna urembo uliotengenezwa kwa nondo ili kuzuia wezi.
 
Wakuu,

Kwa muda mrefu nimekuwa nikijiuliza sana juu ya hili. Nashindwa kujua ni nini hasa chanzo cha makazi ya polisi kuonekana duni karibu mikoa yote. Sina shaka kuwa, baadhi yenu mtakuwa mashahidi kuwa, karibu mikoa yote ya Tanzania, nyumba za askari polisi zimekuwa duni MNO kiasi cha kutia aibu.

Awali, nilifikiri kuwa huenda ni kutokana na kutokukarabatiwa mara kwa mara. Lakini ajabu ni kuwa, zipo ambazo zimejengwa nikiwa naziona, na zilikuwa na ubora mzuri tu wakati zinaanza kutumika, lakini baada ya muda, mtazamo wa nyumba hizi unabadilika na kuwa mbaya mno na usioridhisha. Rangi hupauka na kuta kuwa chafu kupitiliza, mafaa huanza kunyofoka ovyo, zile ambazo ni za ghorofa huanza kuwa na leakage, Na mbaya zaidi, wao wenyewe huanza kubadili ramani kwa kuvuta vichumba kwa kutumia mabati chakavu, ceiling boards, nyavu kuu kuu n.k

Makazi haya ya mfumo wa kambi "servants Quarters" za polisi Tanzania, kwa mikoa yote, ni tofauti kabisa na ya taaluma zingine. Mathalani, Nyumba za walimu kwa shule kongwe nyingi za zamani kama vile Mwenge Singida, Moshi Tech Kilimanjaro, Pugu, Kibaha, Tosamaganga na zingine, nyumba hizi bado zina hali nzuri sana tofauti kabisa na muda ambao zimetumika. Nyumba za benki na taasisi zingine pia ni bora na zenye kuvutia!

Lakini cha ajabu, SERVANTS QUARTERS za Askari Polisi zimebaki kuwa chafu, zisizovutia, zilizoongezwa ongezwa vi structure visivyoeleweka na mambo mengine kibao. Ajabu ni kuwa, karibu kila mkoa kuna kundi kubwa la askari ambao ni mafundi waashi, na tena bado wanaweza kuwatumia wafungwa kuboresha, walau basi kupiga rangi, lakini bado nyumba hizi zimebaki kuwa na hali mbaya MNO..

Hii, hapa na pale, imeendelea kuzifanya hali za kimaisha za Askari Tanzania kuwa duni. Huenda uduni huu machoni kwa watu unatokana pia na makazi duni popote pale wanapoishi Askari Polisi.

Jamani, labda kuna wenye uzoefu juu ya hili.. NINI HASA TATIZO ZA MAKAZI YA ASKARI???
Sasa wewe ukijenga mabanda ya unayawekea nkshi ya nini. Hayo ni mabanda bana kwa hivo hayawezi kabisa kutunzwa
 
MALI YAKO BINAFSI ULIYOTAFUTA KWA UHALALI NA JASHO, "Product as Assets" UTATUMIA KWA UANGALIFU MKUBWA NA KUITUNZA.

KWA NCHI ZA KIAFRIKA KAMA TZ UNADHANI KWA NINI MALI ZA SERIKALI HAZIDUMU..?

SASA MALI YA SERIKALI ISIYO NA MWENYEWE UNADHANI NANI ATAKUWA NA UCHUNGU NAYO KAMA ILIVYO YAKO BINAFSI ?
 
Daah...nazani Kuna polisi huku embu waone walivyo tengeneza chuki na jamii...hii platform inatosha kabisa kuelezea mawazo halisi ya watanzania huko uraiani. Ifike wakati nyie ndugu zetu muache kutumika kisiasa au kwa matakwa ya mtu fulani tendeni haki na tumieni taaluma zenu na Utashi wenu. Mwisho wa siku tutakutana Uraiani hata kama mnakaa kambini.

Daah sema mdau uliyesema ukimuona Polisi analiwa na simba utajitolea kumkatia katia kachumbari Simba ili ajinome vizuri Daah...Lakini hawa jamaa Kweli ndugu zangu Askari mmezidi embu jitambueni basi. Alafu nawaonea huruma mishahara yao na dhambi wanazo bebeshwa Daah ni vitu viwili tofauti.

Nirudi kwenye Mada...Makazi yao kuwa Duni na Yasiyo vutia na wengine wanaka nyumba za Full Bati...Nazani ni kwasababu Viongozi (Wanapo Pokea Amri) wanaona hawastaili au hawana thamini ya kukaa pazuri/kuwa na makazi Bora... yaani kwa kifupi wana wadharau labda kwa kuwa labda wanawaona hawajitambui wapo kama makondoo..Akiambiwa piga ye anapiga tuu bila kuuliza kosa gani/ au hii ndio njia pekee ya kumwajibisha huyu...yaani yeye ni kanyaga twende hata awe ndugu/rafiki/jamaa yake
 
Tatizo ni muajiri anaamini polisi wanaweza kujiendesha kwa zero budget pia wanachukiwa mpaka na viongozi wao lakini mbaya zaidi wao kwa wao wanabaguana wanachukiana.
Siyo tu hayo sisi raia hatuwapendi kwasababu kila siku lazima ukutane nao wakitekeleza majukumu tuliyowapa.
Maadui wao wapo pande mbili ambazo ni mtuhumiwa na mlalamikaji katika pande hizo mbili ni lazima waegemee upande mmoja hivyo kuwa vigumu kuridhisha pande zote kamwe hawatakuja kukubalika toka enzi za kristo.
 
MALI YAKO BINAFSI ULIYOTAFUTA KWA UHALALI NA JASHO, "Product as Assets" UTATUMIA KWA UANGALIFU MKUBWA NA KUITUNZA.

KWA NCHI ZA KIAFRIKA KAMA TZ UNADHANI KWA NINI MALI ZA SERIKALI HAZIDUMU..?

SASA MALI YA SERIKALI ISIYO NA MWENYEWE UNADHANI NANI ATAKUWA NA UCHUNGU NAYO KAMA ILIVYO YAKO BINAFSI ?
Kweli mzee hata magari ya ofisini kwetu wanalea kama kuruti wa jkt
 
Sema usemavyo wewe ushawahi ona simba kamla mmasai pale ngorongoro,

Tumekuskia kijana ila jua kazi yako hiyo inalaana ndo maana hata ukivaa sweta unachomekea, hata uvaaji wenu unaonesha jinsi ulivo failure
Wewe tangu utafute hiyo kazi ya upolisi ukaikosa basi una hasira naooooo
 
Serikali iruhusu watu binafsi wajenge nyumba maalum kwa ajili ya watumishi wake hususan polisi ili iwe rahisi kuzitunza na kuweka tozo maalum sambamba na pango.

Hivyo nyumba hizo zitakuwa zikitunzwa na kuwa chini ya uangalizi wa watu wa nje na sio serikali.

Gharama zitakuwa ni kubwa lakini polisi watanawiri na kupendeza na kujisikia wanaishi kwenye nyumba za maana.

Ila sidhani kama serikali ina fedha za aina hiyo za kuwalipia polisi waishi kwenye mazingira mazuri.
 
Sababu ni moja tu nayo ni hii
HAKUNA MTU WA KWENDA KUIBA CHOCHOTE KWENYE NYUMBA ZA POLISI.
Nyumba nyingi zinaonekana zimepambwa vizuri kwa madirisha ya nondo
zilizochongwa vizuri lakini mantiki ni ile ile ya kuzuia wezi.
Sijui ndani ya nyumba za polisi kukoje lakini nakshi ya nje
hakuna urembo uliotengenezwa kwa nondo ili kuzuia wezi.
Na hakuna cha kuiba kwa polisi mwizi ataiba nini kwa polisi tu ?
 
kantalambaz Hapana Mkuu...nimesema kwa maoni ya wadau kadhaa waliochangia mada...ni dhahiri kuna chuki dhidi ya polisi na raia..Au kwa mawazo yako naweza sema pia wote walio changia kuwadis polisi ni wahalifu. Ndicho unacho taka kusikia sio?
 
Chuki ipo sana tu. ndani ya polisi kuna askari werevu na wapumbav wapo. The thing is werevu na wenye busara ni wachache.. wapumbav ndio wengi.
Hii inasababisha ufanisi wao kuwa wa mashaka.. polis wangekuwa kama wa nchi zingine.. wangejiweka karib zaid na jamii kantalambaz
 
Back
Top Bottom